Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 1

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ

Itapo chanika mbingu,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 2

وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapaswa kumsikiliza,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 3

وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ

Na ardhi itakapo tanuliwa,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 4

وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ

Na kuvitoa vilivyokuwa ndani yake, ikawa tupu,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 5

وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapaswa kumsikiliza,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ

Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 7

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 8

فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا

Basi huyo atahesabiwa hisabu nyepesi,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 9

وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا

Na arudi kwa watu wake na furaha



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 10

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 11

فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا

Basi huyo ataomba kuteketea



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 12

وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا

Na ataingia Motoni



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 13

إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا

Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 14

إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ

Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 15

بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا

Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 16

فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ

Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 17

وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ

Na kwa usiku na unavyo vikusanya,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 18

وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ

Na kwa mwezi unapo pevuka,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 19

لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ

Lazima mtapanda tabaka kwa tabaka!



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 20

فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Basi wana nini hawaamini?



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 21

وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩

Na wanapo somewa Qur’ani hawasujudu?



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 22

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ

Bali walio kufuru wanakanusha tu



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 23

وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ

Na Allah anajua wanayo yadhamiria



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 24

فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

Basi wabashirie adhabu chungu!



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 25

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ

Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika