Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 1

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ

Ewe mwenye kujigubika



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 2

قُمۡ فَأَنذِرۡ

Simama uonye



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 3

وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ

Na Mola wako Mlezi mtukuze



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 4

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ

Na nguo zako zisafishe



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 5

وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ

Na (mambo) machafu yahame (yaache)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 6

وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ

Wala usitoe (usifanye hisani) kwa kutaraji kuzidishiwa (kupata kingi Zaidi)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 7

وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ

Na kwa ajili ya Mola wako tu kuwa na subira (kuwa mvumilivu)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 8

فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ

Basi litakapopulizwa baragumu (Tarumbeta)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 9

فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ

Basi siku hiyo itakuwa ni siku ngumu sana



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 10

عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ

Kwa makafiri haitakuwa nyepesi



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 11

ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا

Niache Mimi peke yangu na yule niliye muumba



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 12

وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا

Na nikamjaalia awe na mali nyingi



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 13

وَبَنِينَ شُهُودٗا

Na watoto wanao onekana



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 14

وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا

Na nikamtengenezea mambo vizuri kabisa



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 15

ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ

Kisha anatumai Nimuongezee!



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 16

كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا

Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi (Na umpinzani) Aya zetu!



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 17

سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا

Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 18

إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ

Kwani hakika yeye alifikiri na akapima



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 19

فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Basi ameangamia! Namna alivyo pima



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 20

ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Tena ameangamia! Namna alivyo pima!



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 21

ثُمَّ نَظَرَ

Kisha akatazama



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 22

ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ

Kisha akakunja paji (la uso) na akafinya uso kwa ghadhabu



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 23

ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ

Kisha akageuka nyuma, na akaipa kisogo haki, na akatakabari



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 24

فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ

Na akasema: Hii (Qurani) si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 25

إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ

Hii si chochote isipokuwa ni kauli ya binadamu



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 26

سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ

Nitamuingiza (na kumuunguza) kwenye Moto wa saqar



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 27

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ

Na ni nini kitakujuulisha nini huo Moto wa Saqar?



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 28

لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ

Haubakishi wala hauachi, (kitu chochote)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 29

لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ

Wenye kubabua vikali ngozi, (iwe nyeusi)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 30

عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ

Juu yake wako (walinzi) kumi na tisa