Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 1

سَأَلَ سَآئِلُۢ بِعَذَابٖ وَاقِعٖ

Muulizaji ameuliza kuhusu adhabu itakayotokea



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 2

لِّلۡكَٰفِرِينَ لَيۡسَ لَهُۥ دَافِعٞ

Kwa makafiri, hapana wa kuizuia



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 3

مِّنَ ٱللَّهِ ذِي ٱلۡمَعَارِجِ

Kutoka kwa Allah Mwenye madaraja ya juu (Mwenye mbingu za daraja)



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 4

تَعۡرُجُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيۡهِ فِي يَوۡمٖ كَانَ مِقۡدَارُهُۥ خَمۡسِينَ أَلۡفَ سَنَةٖ

Malaika na Roho (Jibrili) wanapanda kwenda kwake katika siku ambayo makadirio yake ni miaka hamsini elfu



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 5

فَٱصۡبِرۡ صَبۡرٗا جَمِيلًا

Basi subiri subira njema



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 6

إِنَّهُمۡ يَرَوۡنَهُۥ بَعِيدٗا

Hakika, wao wanaiona (siku hiyo) iko mbali



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 7

وَنَرَىٰهُ قَرِيبٗا

Nasi tunaiona iko karibu



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 8

يَوۡمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلۡمُهۡلِ

Siku ambayo mbingu zitakuwa kama shaba iliyo yeyushwa



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 9

وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ

Na milima itakuwa kama sufi (iliyo chambuliwa)



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 10

وَلَا يَسۡـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمٗا

Na rafiki hatomuuliza rafiki yake



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 11

يُبَصَّرُونَهُمۡۚ يَوَدُّ ٱلۡمُجۡرِمُ لَوۡ يَفۡتَدِي مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِئِذِۭ بِبَنِيهِ

Watafanywa waonane. Mkosefu atatamani (kujikomboa) ajitolee fidia kutokana na adhabu Siku hiyo kwa kuwatoa watoto wake



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 12

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ

Na mke wake na nduguye



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 13

وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِي تُـٔۡوِيهِ

Na jamaa zake wa karibu ambao wanamlinda



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 14

وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ يُنجِيهِ

Na (pia atatamani kutoa fidia kwa kulipa) vyote vilivyomo ardhini (duniani) kisha (ili) vimuokoe



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 15

كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

Sio hivyo (Hayawezekani hayo). Kwa hakika, huo ni Moto mkali kabisa



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 16

نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ

Unaobabua kwa nguvu ngozi ya kichwani na mwilini



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 17

تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Unamwita yule aliyegeuza mgongo (aliyepuuza muongozo wa Allah) na akakengeuka



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 18

وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ

Na akakusanya (mali) kisha akayahifadhi (katika makasha)



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 19

۞إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا

Hakika, mwanadamu ameumbwa akiwa mwenye pupa (mwenye kukosa subira)



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 20

إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعٗا

Inapomgusa shari anakuwa mwingi wa kupapatika (kulalamika na kuhuzunika)



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 21

وَإِذَا مَسَّهُ ٱلۡخَيۡرُ مَنُوعًا

Na inapomgusa kheri (anakuwa) mwingi wa kuzuia (bahili)



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 22

إِلَّا ٱلۡمُصَلِّينَ

Isipokuwa wenye kuswali



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 23

ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ

Ambao wenye kudumisha Sala zao



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 24

وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ

Na wale ambao katika Mali zao kuna haki maalumu



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 25

لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Kwa (Masikini) mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 26

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na ambao wanasadikisha Siku ya Malipo, (siku ya Kiyama)



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 27

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 28

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ

Hakika adhabu ya Mola wao si ya kusalimika nayo



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 29

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ

Na ambao wanahifadhi tupu zao



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 30

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ

Isipokuwa kwa wake zao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao si wenye kulaumiwa