Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 1

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Wakati kitakapotokea Kiyama



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 2

لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ

Hakuna mpingaji wa kutokea kwake



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 3

خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ

Ni chenye kuwashusha hadhi (makafiri) na kuwanyanyua hadhi (waumini)



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 4

إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا

Wakati ardhi itakapotikiswa mtikiso mkubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 5

وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا

Na milima ikapondwa pondwa upondwaji mkubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 6

فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا

(Kwa sababu ya kupondwa pondwa huko, milima) ikawa vumbi lenye kutawanyika



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 7

وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ

Na nyinyi (watu) mtakuwa namna tatu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 8

فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Basi watakuwepo watu wa kuliani. Je, ni kina nani watu wa kuliani?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 9

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Na (watakuwepo) watu wa kushotoni. Je, ni kina nani watu wa kushotoni?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 10

وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ

Na (watakuwepo) waliotangulia mbele, (basi) watakua mbele.[1]


1- - Hawa ni wale ambao walitangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya akhera.


Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 11

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakao kurubishwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 12

فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

katika pepo zenye neema



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 13

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika wa mwanzo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 14

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na wachache katika wa mwishoni.[1]


1- - Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yalio tangulia na Manabii wao, na wachache katika Umma wa Muhammad rehma na amani ziwe juu yake ukilinganishwa na hao.


Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 15

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ

watakua juu ya vitanda vilivyofumwa vizuri



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 16

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ

hali wakiwa wameviegemea huku wakitazamana



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 17

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ

Watazungukiwa na vijana wenye kudumu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 18

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ

Kwa bilauri na mabirika na vikombe vya mvinyo kutoka kwenye chemchemu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 19

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Hawatapata maumivu ya kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawa-tatokwa na akili



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 20

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Na matunda watakayo pendelea wao



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 21

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na nyama za ndege katika wata-kazozitamani



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 22

وَحُورٌ عِينٞ

Na wanawake wenye macho makubwa yaliyo meupe sana na weusi sana



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 23

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Kama mfano wa lulu zilizohi-fadhiwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 24

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ikiwa ni malipo kwa ambayo walikuwa wanatenda (duniani)



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 25

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Hawatasikia humo maneno ya upuuzi wala yanayopelekea kupata madhambi



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 26

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipokuwa itasemwa: Salama, na Amani!



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 27

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na watu wa kuliani, ni wepi hao watu wa kuliani?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 28

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 29

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 30

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotandazwa