Sura: TWAHA 

Aya : 1

طه

Twaahaa!



Sura: TWAHA 

Aya : 2

مَآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡقُرۡءَانَ لِتَشۡقَىٰٓ

Hatukukuteremshia Qur’an ili upate mashaka



Sura: TWAHA 

Aya : 3

إِلَّا تَذۡكِرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰ

Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea



Sura: TWAHA 

Aya : 4

تَنزِيلٗا مِّمَّنۡ خَلَقَ ٱلۡأَرۡضَ وَٱلسَّمَٰوَٰتِ ٱلۡعُلَى

(Hii Qur’ani ni) uteremsho kutoka kwa Allah Ambaye Ameum-ba ardhi na mbingu zilizo juu



Sura: TWAHA 

Aya : 5

ٱلرَّحۡمَٰنُ عَلَى ٱلۡعَرۡشِ ٱسۡتَوَىٰ

Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliyestawi juu ya Kiti cha Enzi



Sura: TWAHA 

Aya : 6

لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَمَا تَحۡتَ ٱلثَّرَىٰ

Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi



Sura: TWAHA 

Aya : 7

وَإِن تَجۡهَرۡ بِٱلۡقَوۡلِ فَإِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلسِّرَّ وَأَخۡفَى

Na ukinyanyua sauti kwa kusema... basi hakika Yeye anajua siri na kilichofichikana zaidi kuliko siri



Sura: TWAHA 

Aya : 8

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ لَهُ ٱلۡأَسۡمَآءُ ٱلۡحُسۡنَىٰ

Allah! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa



Sura: TWAHA 

Aya : 9

وَهَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Na je! Imekufikia habari ya Mussa?



Sura: TWAHA 

Aya : 10

إِذۡ رَءَا نَارٗا فَقَالَ لِأَهۡلِهِ ٱمۡكُثُوٓاْ إِنِّيٓ ءَانَسۡتُ نَارٗا لَّعَلِّيٓ ءَاتِيكُم مِّنۡهَا بِقَبَسٍ أَوۡ أَجِدُ عَلَى ٱلنَّارِ هُدٗى

Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka (katika) huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto



Sura: TWAHA 

Aya : 11

فَلَمَّآ أَتَىٰهَا نُودِيَ يَٰمُوسَىٰٓ

Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Mussa!



Sura: TWAHA 

Aya : 12

إِنِّيٓ أَنَا۠ رَبُّكَ فَٱخۡلَعۡ نَعۡلَيۡكَ إِنَّكَ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوٗى

Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la Tuwa



Sura: TWAHA 

Aya : 13

وَأَنَا ٱخۡتَرۡتُكَ فَٱسۡتَمِعۡ لِمَا يُوحَىٰٓ

Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa



Sura: TWAHA 

Aya : 14

إِنَّنِيٓ أَنَا ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱعۡبُدۡنِي وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ لِذِكۡرِيٓ

Hakika Mimi ndiye Allah. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi



Sura: TWAHA 

Aya : 15

إِنَّ ٱلسَّاعَةَ ءَاتِيَةٌ أَكَادُ أُخۡفِيهَا لِتُجۡزَىٰ كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا تَسۡعَىٰ

Hakika Saa (Kiyama) kitakuja bila ya shaka. Nimekaribia kukificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyo yafanya



Sura: TWAHA 

Aya : 16

فَلَا يَصُدَّنَّكَ عَنۡهَا مَن لَّا يُؤۡمِنُ بِهَا وَٱتَّبَعَ هَوَىٰهُ فَتَرۡدَىٰ

Kwa hivyo asikukengeushe nacho (Kiyama) yule ambaye hakiamini na akafuata matamanio yake ukaja kuangamia



Sura: TWAHA 

Aya : 17

وَمَا تِلۡكَ بِيَمِينِكَ يَٰمُوسَىٰ

Na nini hicho kilichomo katika mkono wako wa kulia, ewe Mussa?



Sura: TWAHA 

Aya : 18

قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّؤُاْ عَلَيۡهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَـَٔارِبُ أُخۡرَىٰ

Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine



Sura: TWAHA 

Aya : 19

قَالَ أَلۡقِهَا يَٰمُوسَىٰ

(Allah) Akasema: Basi iangushe ewe Mussa



Sura: TWAHA 

Aya : 20

فَأَلۡقَىٰهَا فَإِذَا هِيَ حَيَّةٞ تَسۡعَىٰ

Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio



Sura: TWAHA 

Aya : 21

قَالَ خُذۡهَا وَلَا تَخَفۡۖ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا ٱلۡأُولَىٰ

Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza



Sura: TWAHA 

Aya : 22

وَٱضۡمُمۡ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٍ ءَايَةً أُخۡرَىٰ

Na ukumbatie mkono wako kwenye ubavu wako. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine



Sura: TWAHA 

Aya : 23

لِنُرِيَكَ مِنۡ ءَايَٰتِنَا ٱلۡكُبۡرَى

Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa



Sura: TWAHA 

Aya : 24

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka



Sura: TWAHA 

Aya : 25

قَالَ رَبِّ ٱشۡرَحۡ لِي صَدۡرِي

(Mussa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,



Sura: TWAHA 

Aya : 26

وَيَسِّرۡ لِيٓ أَمۡرِي

Na uifanye kazi yangu (kuwa) nyepesi,



Sura: TWAHA 

Aya : 27

وَٱحۡلُلۡ عُقۡدَةٗ مِّن لِّسَانِي

Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,



Sura: TWAHA 

Aya : 28

يَفۡقَهُواْ قَوۡلِي

Wapate kufahamu maneno yangu



Sura: TWAHA 

Aya : 29

وَٱجۡعَل لِّي وَزِيرٗا مِّنۡ أَهۡلِي

Na nipe waziri katika watu wangu,



Sura: TWAHA 

Aya : 30

هَٰرُونَ أَخِي

Harun, ndugu yangu