Sura: AL-ASWRI 

Aya : 1

وَٱلۡعَصۡرِ

Naapa kwa Zama!



Sura: AL-ASWRI 

Aya : 2

إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَفِي خُسۡرٍ

Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara,



Sura: AL-ASWRI 

Aya : 3

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡحَقِّ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ

Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri