Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 211

وَمَا يَنۢبَغِي لَهُمۡ وَمَا يَسۡتَطِيعُونَ

Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 212

إِنَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّمۡعِ لَمَعۡزُولُونَ

Hakika hao wametengwa na kusikia



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 213

فَلَا تَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُعَذَّبِينَ

Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Allah ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 214

وَأَنذِرۡ عَشِيرَتَكَ ٱلۡأَقۡرَبِينَ

Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 215

وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 216

فَإِنۡ عَصَوۡكَ فَقُلۡ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تَعۡمَلُونَ

Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 217

وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 218

ٱلَّذِي يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ

Ambaye anakuona unapo simama,



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 219

وَتَقَلُّبَكَ فِي ٱلسَّـٰجِدِينَ

Na mageuko yako kati ya wanao sujudu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 220

إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 221

هَلۡ أُنَبِّئُكُمۡ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ

Je! Nikwambieni nani wana-washukia Mashet’ani?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 222

تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٖ

Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 223

يُلۡقُونَ ٱلسَّمۡعَ وَأَكۡثَرُهُمۡ كَٰذِبُونَ

Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 224

وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلۡغَاوُۥنَ

Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 225

أَلَمۡ تَرَ أَنَّهُمۡ فِي كُلِّ وَادٖ يَهِيمُونَ

Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 226

وَأَنَّهُمۡ يَقُولُونَ مَا لَا يَفۡعَلُونَ

Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 227

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَذَكَرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا وَٱنتَصَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا ظُلِمُواْۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَيَّ مُنقَلَبٖ يَنقَلِبُونَ

Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Allah kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka