Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 151

أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ

Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 152

وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ

Allah amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 153

أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ

Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 154

مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ

Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 155

أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Hamkumbuki?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 156

أَمۡ لَكُمۡ سُلۡطَٰنٞ مُّبِينٞ

Au mnayo hoja iliyo wazi?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 157

فَأۡتُواْ بِكِتَٰبِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 158

وَجَعَلُواْ بَيۡنَهُۥ وَبَيۡنَ ٱلۡجِنَّةِ نَسَبٗاۚ وَلَقَدۡ عَلِمَتِ ٱلۡجِنَّةُ إِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ

Na wameweka mahusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 159

سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ

Subhana ‘Llah Ametakasika Allah na hayo wanayo msingizia



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 160

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa waja wa Allah walio safishwa



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 161

فَإِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ

Basi hakika nyinyi na mnao waabudu



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 162

مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ بِفَٰتِنِينَ

Hamwezi kuwapoteza



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 163

إِلَّا مَنۡ هُوَ صَالِ ٱلۡجَحِيمِ

Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 164

وَمَامِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٞ مَّعۡلُومٞ

Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 165

وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلصَّآفُّونَ

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 166

وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡمُسَبِّحُونَ

Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 167

وَإِن كَانُواْ لَيَقُولُونَ

Na walikuwapo walio kuwa wakisema:



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 168

لَوۡ أَنَّ عِندَنَا ذِكۡرٗا مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Tungelikuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 169

لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Allah wenye ikhlasi



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 170

فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ

Lakini waliukataa. Basi watakuja jua



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 171

وَلَقَدۡ سَبَقَتۡ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 172

إِنَّهُمۡ لَهُمُ ٱلۡمَنصُورُونَ

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 173

وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ

Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 174

فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ

Basi waachilie mbali kwa muda



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 175

وَأَبۡصِرۡهُمۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ

Na watazame, nao wataona



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 176

أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ

Je! Wanaihimiza adhabu yetu?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 177

فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمۡ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 178

وَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ

Na waache kwa muda



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 179

وَأَبۡصِرۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ

Na tazama, na wao wataona



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 180

سُبۡحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلۡعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ

Subhana Rabbi’l’Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia