Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 151

وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Wala msitii amri za walio pindukia mipaka,



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 152

ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ

Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 153

قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 154

مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 155

قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٞ لَّهَا شِرۡبٞ وَلَكُمۡ شِرۡبُ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 156

وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَظِيمٖ

Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 157

فَعَقَرُوهَا فَأَصۡبَحُواْ نَٰدِمِينَ

Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 158

فَأَخَذَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 159

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 160

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Watu wa Lutwi waliwakanusha Mitume



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 161

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia ndugu yao, Lutwi: Je! Hamumchi Allah?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 162

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 163

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah na nitiini mimi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 164

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 165

أَتَأۡتُونَ ٱلذُّكۡرَانَ مِنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Je! mnawaingilia wanaume katika walimwengu?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 166

وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّنۡ أَزۡوَٰجِكُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٌ عَادُونَ

Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 167

قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُخۡرَجِينَ

Wakasema: Ewe Lutwi! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 168

قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلۡقَالِينَ

Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 169

رَبِّ نَجِّنِي وَأَهۡلِي مِمَّا يَعۡمَلُونَ

Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 170

فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 171

إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 172

ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengine



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 173

وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Na tukawanyeshea mvua, basi ni mbaya mno mvua ya waliyoonywa



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 174

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 175

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 176

كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ لۡـَٔيۡكَةِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 177

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ شُعَيۡبٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamcha Allah?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 178

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 179

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah, na nitiini mimi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 180

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote