Sura: ANNAHLI 

Aya : 121

شَاكِرٗا لِّأَنۡعُمِهِۚ ٱجۡتَبَىٰهُ وَهَدَىٰهُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

(Ibrahimu alikuwa) daima mwenye kushukuru neema zake (Allah) akamchagua na akamuon-goza kwenye njia iliyonyooka



Sura: ANNAHLI 

Aya : 122

وَءَاتَيۡنَٰهُ فِي ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٗۖ وَإِنَّهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ لَمِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tukampa wema duniani, na hakika yeye Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema



Sura: ANNAHLI 

Aya : 123

ثُمَّ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ أَنِ ٱتَّبِعۡ مِلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۖ وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Kisha tukakufunulia (ewe Muhammad) kwamba ufuate mila (dini) ya Ibrahimu (aliyekuwa) mtiifu kamili, wala hakuwa miongoni mwa washirikina



Sura: ANNAHLI 

Aya : 124

إِنَّمَا جُعِلَ ٱلسَّبۡتُ عَلَى ٱلَّذِينَ ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِۚ وَإِنَّ رَبَّكَ لَيَحۡكُمُ بَيۡنَهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فِيمَا كَانُواْ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ

Hakika siku ya Sabato (jumamosi) iliwekwa kwa wale waliohitilafiana kuhusu yeye (Ibrahimu) na dini yake. Na kwa hakika Mola wako atahukumu baina yao Siku ya Kiyama kuhusu yale waliyokuwa wakihitilafiana



Sura: ANNAHLI 

Aya : 125

ٱدۡعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِٱلۡحِكۡمَةِ وَٱلۡمَوۡعِظَةِ ٱلۡحَسَنَةِۖ وَجَٰدِلۡهُم بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Waite (walinganie watu) katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha mazuri, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora. Hakika Mola wako mlezi yeye anamjua zaidi aliyepotea katika njia yake, na yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka



Sura: ANNAHLI 

Aya : 126

وَإِنۡ عَاقَبۡتُمۡ فَعَاقِبُواْ بِمِثۡلِ مَا عُوقِبۡتُم بِهِۦۖ وَلَئِن صَبَرۡتُمۡ لَهُوَ خَيۡرٞ لِّلصَّـٰبِرِينَ

Na mkilipiza (kisasi), basi lipizeni sawa na vile mlivyoonewa, na kama mkisubiri, hakika hilo ni bora kwa wanaosubiri



Sura: ANNAHLI 

Aya : 127

وَٱصۡبِرۡ وَمَا صَبۡرُكَ إِلَّا بِٱللَّهِۚ وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَلَا تَكُ فِي ضَيۡقٖ مِّمَّا يَمۡكُرُونَ

Na subiri, na haiwi subira yako isipokuwa ni kwa ajili Allah tu, na usihuzunike kwa ya ajili yao, na usiwe katika dhiki kwa sababu ya vitimbi wanavyovifanya



Sura: ANNAHLI 

Aya : 128

إِنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَواْ وَّٱلَّذِينَ هُم مُّحۡسِنُونَ

Kwa hakika Allah yupo pamoja na wale wanaomcha (Allah), na wale wafanyao wema