Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 91

وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِلۡغَاوِينَ

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 92

وَقِيلَ لَهُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ

Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 93

مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلۡ يَنصُرُونَكُمۡ أَوۡ يَنتَصِرُونَ

Badala ya Allah? Je! Wanaku-saidieni, au wanajisaidia wenyewe?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 94

فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ

Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 95

وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ

Na majeshi ya Ibilisi yote



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 96

قَالُواْ وَهُمۡ فِيهَا يَخۡتَصِمُونَ

Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 97

تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 98

إِذۡ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 99

وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Na hawakupoteza ila wale wakosefu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 100

فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ

Basi hatuna waombezi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 101

وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٖ

Wala rafiki wa dhati



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 102

فَلَوۡ أَنَّ لَنَا كَرَّةٗ فَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Laiti tungelipata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 103

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 104

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 105

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 106

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamumuogopi Allah?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 107

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 108

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi Mcheni Allah, na nitiini mimi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 109

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 110

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi Mcheni Allah, na nitiini mimi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 111

۞قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ

Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanaokufuata ni watu wa chini?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 112

قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 113

إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ

Hesabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 114

وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 115

إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Mimi si chochote ila ni Muonyaji wa dhahiri



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 116

قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ

Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 117

قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 118

فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 119

فَأَنجَيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ

Kwahivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 120

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا بَعۡدُ ٱلۡبَاقِينَ

Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia