Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 91

مَا ٱتَّخَذَ ٱللَّهُ مِن وَلَدٖ وَمَا كَانَ مَعَهُۥ مِنۡ إِلَٰهٍۚ إِذٗا لَّذَهَبَ كُلُّ إِلَٰهِۭ بِمَا خَلَقَ وَلَعَلَا بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ

Allah hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeliwashinda wengine. Allah ameepukana na sifa wanazo msifu



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 92

عَٰلِمِ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِ فَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Mjuzi wa siri na dhaahiri, na ametukuka juu ya hayo wanayo mshirikisha nayo



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 93

قُل رَّبِّ إِمَّا تُرِيَنِّي مَا يُوعَدُونَ

Sema: Mola wangu Mlezi! Unionyeshapo adhabu waliyo ahidiwa,



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 94

رَبِّ فَلَا تَجۡعَلۡنِي فِي ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Mola wangu Mlezi! Usinijaalie katika watu madhalimu hao



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 95

وَإِنَّا عَلَىٰٓ أَن نُّرِيَكَ مَا نَعِدُهُمۡ لَقَٰدِرُونَ

Na hakika Sisi ni waweza wa kukuonyesha tuliyo waahidi



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 96

ٱدۡفَعۡ بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ ٱلسَّيِّئَةَۚ نَحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَا يَصِفُونَ

Kinga maovu kwa kutenda yaliyo mema zaidi. Sisi tunajua wayasemayo



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 97

وَقُل رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنۡ هَمَزَٰتِ ٱلشَّيَٰطِينِ

Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashetani



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 98

وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحۡضُرُونِ

Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 99

حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَ أَحَدَهُمُ ٱلۡمَوۡتُ قَالَ رَبِّ ٱرۡجِعُونِ

Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 100

لَعَلِّيٓ أَعۡمَلُ صَٰلِحٗا فِيمَا تَرَكۡتُۚ كَلَّآۚ إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَآئِلُهَاۖ وَمِن وَرَآئِهِم بَرۡزَخٌ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watakapo fufuliwa



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 101

فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ فَلَآ أَنسَابَ بَيۡنَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ وَلَا يَتَسَآءَلُونَ

Basi litakapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 102

فَمَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 103

وَمَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فِي جَهَنَّمَ خَٰلِدُونَ

Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia hasara nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 104

تَلۡفَحُ وُجُوهَهُمُ ٱلنَّارُ وَهُمۡ فِيهَا كَٰلِحُونَ

Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 105

أَلَمۡ تَكُنۡ ءَايَٰتِي تُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فَكُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Je! Hazikuwa Aya zangu mkiso-mewa, na nyinyi mkizikanusha?



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 106

قَالُواْ رَبَّنَا غَلَبَتۡ عَلَيۡنَا شِقۡوَتُنَا وَكُنَّا قَوۡمٗا ضَآلِّينَ

Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 107

رَبَّنَآ أَخۡرِجۡنَا مِنۡهَا فَإِنۡ عُدۡنَا فَإِنَّا ظَٰلِمُونَ

Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 108

قَالَ ٱخۡسَـُٔواْ فِيهَا وَلَا تُكَلِّمُونِ

Atasema Allah: Tokomeeni humo, wala msinisemeshe



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 109

إِنَّهُۥ كَانَ فَرِيقٞ مِّنۡ عِبَادِي يَقُولُونَ رَبَّنَآ ءَامَنَّا فَٱغۡفِرۡ لَنَا وَٱرۡحَمۡنَا وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلرَّـٰحِمِينَ

Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 110

فَٱتَّخَذۡتُمُوهُمۡ سِخۡرِيًّا حَتَّىٰٓ أَنسَوۡكُمۡ ذِكۡرِي وَكُنتُم مِّنۡهُمۡ تَضۡحَكُونَ

Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 111

إِنِّي جَزَيۡتُهُمُ ٱلۡيَوۡمَ بِمَا صَبَرُوٓاْ أَنَّهُمۡ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ

Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 112

قَٰلَ كَمۡ لَبِثۡتُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ عَدَدَ سِنِينَ

Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hesabu ya miaka?



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 113

قَالُواْ لَبِثۡنَا يَوۡمًا أَوۡ بَعۡضَ يَوۡمٖ فَسۡـَٔلِ ٱلۡعَآدِّينَ

Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hesabu



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 114

قَٰلَ إِن لَّبِثۡتُمۡ إِلَّا قَلِيلٗاۖ لَّوۡ أَنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti mngelikuwa mnajua



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 115

أَفَحَسِبۡتُمۡ أَنَّمَا خَلَقۡنَٰكُمۡ عَبَثٗا وَأَنَّكُمۡ إِلَيۡنَا لَا تُرۡجَعُونَ

Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 116

فَتَعَٰلَى ٱللَّهُ ٱلۡمَلِكُ ٱلۡحَقُّۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ رَبُّ ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡكَرِيمِ

Ametukuka Allah, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A’rshi Tukufu



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 117

وَمَن يَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ لَا بُرۡهَٰنَ لَهُۥ بِهِۦ فَإِنَّمَا حِسَابُهُۥ عِندَ رَبِّهِۦٓۚ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلۡكَٰفِرُونَ

Na anaye muomba - pamoja na Allah - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hesabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi



Sura: ALMUUMINUUN 

Aya : 118

وَقُل رَّبِّ ٱغۡفِرۡ وَٱرۡحَمۡ وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلرَّـٰحِمِينَ

Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu