Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 61

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Kwamba Tuwabadilishe wengine mfano wenu, na Tukuumbeni katika umbo msilolijua



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 62

وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ

Na bila shaka mmejua umbo la kwanza, basi kwanini hamkumbuki?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 63

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ

Je, mnaona mbegu mnazo-zipanda?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 64

ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّـٰرِعُونَ

Je, ni nyinyi ndio mnaziotesha, au Sisi ndio Wenye kuotesha mimea?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 65

لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ

Lau Tungelitaka, Tungelifanya mabua yaliyonyauka na mkabaki mnashangaa na kusikitika



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 66

إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ

(Mkisema): Hakika sisi tumegharimika



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 67

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

Bali sisi tumenyimwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 68

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ

Je, mnaona maji ambayo mnakunywa?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 69

ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ

Je, ni nyinyi ndio mliyoyateremsha kutoka katika mawingu ya mvua au Sisi ndio Wateremshaji?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 70

لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ

Lau Tungelitaka, Tungeliyafanya ya chumvi kali chungu basi kwa nini hamshukuru?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 71

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ

Je, mnaona moto ambao mnauwasha?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 72

ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ

Je, ni nyinyi ndio mliouumba mti wake, au Sisi ndio Waumbaji wa mti huo?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 73

نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ

Sisi Tumeufanya kuwa ni ukumbusho na manufaa kwa wasafiri



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 74

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako aliyetukuka



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 75

۞فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 76

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ

Hakika hicho ni kiapo kikubwa lau mnaelewa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 77

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika ya hiyo ni Kurani tukufu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 78

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilichohifadhiwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 79

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa (Walio twahara)



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 80

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho kutoka kwa Mola wa walimwengu wote



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 81

أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ

Hivi kwa maneno haya nyinyi mnapuuza na kuikanusha?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 82

وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ

Na mnafanya (badala ya kushu-kuru) kwa riziki mnayopata, nyinyi ndio mnakad hibisha



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 83

فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ

Itakuaje basi pale roho itaka-pofika kwenye koo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 84

وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ

Na nyinyi wakati huo mnatazama tu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 85

وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ

Nasi Tuko karibu naye zaidi kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuoni



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 86

فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ

Na lau kuwa nyinyi hammo katika mamlaka yangu.[1]


1- - Basi kama lau kusingekua na kufufuliwa.


Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 87

تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Kwanini hamuirudishi hiyo roho (mwilini mwake), mkiwa ni wakweli?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 88

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Basi akiwa (mwenye roho hiyo) ni miongoni mwa waliokurubishwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 89

فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ

Basi ni raha, na manukato, na mabustani zenye kila aina ya neema



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 90

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ama ikiwa mwenye roho hiyo ni miongoni mwa watu wa kuliani