Sura: SWAAD 

Aya : 61

قَالُواْ رَبَّنَا مَن قَدَّمَ لَنَا هَٰذَا فَزِدۡهُ عَذَابٗا ضِعۡفٗا فِي ٱلنَّارِ

Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusababishia haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni



Sura: SWAAD 

Aya : 62

وَقَالُواْ مَا لَنَا لَا نَرَىٰ رِجَالٗا كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ ٱلۡأَشۡرَارِ

Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahesabu ndio katika waovu?



Sura: SWAAD 

Aya : 63

أَتَّخَذۡنَٰهُمۡ سِخۡرِيًّا أَمۡ زَاغَتۡ عَنۡهُمُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ

Tulikosea tulipo wafanyia mas-khara, au macho yetu tu hayawaoni?



Sura: SWAAD 

Aya : 64

إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقّٞ تَخَاصُمُ أَهۡلِ ٱلنَّارِ

Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni



Sura: SWAAD 

Aya : 65

قُلۡ إِنَّمَآ أَنَا۠ مُنذِرٞۖ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّا ٱللَّهُ ٱلۡوَٰحِدُ ٱلۡقَهَّارُ

Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Allah Mmoja, Mwenye nguvu,



Sura: SWAAD 

Aya : 66

رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفَّـٰرُ

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe



Sura: SWAAD 

Aya : 67

قُلۡ هُوَ نَبَؤٌاْ عَظِيمٌ

Sema: Hii ni habari kubwa kabisa



Sura: SWAAD 

Aya : 68

أَنتُمۡ عَنۡهُ مُعۡرِضُونَ

Ambayo nyinyi mnaipuuza



Sura: SWAAD 

Aya : 69

مَا كَانَ لِيَ مِنۡ عِلۡمِۭ بِٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰٓ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ

Sikuwa na elimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipokuwa wakishindana



Sura: SWAAD 

Aya : 70

إِن يُوحَىٰٓ إِلَيَّ إِلَّآ أَنَّمَآ أَنَا۠ نَذِيرٞ مُّبِينٌ

Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhahiri



Sura: SWAAD 

Aya : 71

إِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن طِينٖ

Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo



Sura: SWAAD 

Aya : 72

فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ

Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumtii



Sura: SWAAD 

Aya : 73

فَسَجَدَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ

Basi Malaika wakatii wote pamoja



Sura: SWAAD 

Aya : 74

إِلَّآ إِبۡلِيسَ ٱسۡتَكۡبَرَ وَكَانَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri



Sura: SWAAD 

Aya : 75

قَالَ يَـٰٓإِبۡلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسۡجُدَ لِمَا خَلَقۡتُ بِيَدَيَّۖ أَسۡتَكۡبَرۡتَ أَمۡ كُنتَ مِنَ ٱلۡعَالِينَ

Allah akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumtii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?



Sura: SWAAD 

Aya : 76

قَالَ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡهُ خَلَقۡتَنِي مِن نَّارٖ وَخَلَقۡتَهُۥ مِن طِينٖ

Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo



Sura: SWAAD 

Aya : 77

قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ

Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika



Sura: SWAAD 

Aya : 78

وَإِنَّ عَلَيۡكَ لَعۡنَتِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo



Sura: SWAAD 

Aya : 79

قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe



Sura: SWAAD 

Aya : 80

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

Allah akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,



Sura: SWAAD 

Aya : 81

إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ

Mpaka siku ya wakati maalumu



Sura: SWAAD 

Aya : 82

قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,



Sura: SWAAD 

Aya : 83

إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio chaguliwa



Sura: SWAAD 

Aya : 84

قَالَ فَٱلۡحَقُّ وَٱلۡحَقَّ أَقُولُ

Akasema: Haki! Na haki ninaisema



Sura: SWAAD 

Aya : 85

لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكَ وَمِمَّن تَبِعَكَ مِنۡهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao



Sura: SWAAD 

Aya : 86

قُلۡ مَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُتَكَلِّفِينَ

Sema (Ewe Mtume): Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu



Sura: SWAAD 

Aya : 87

إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote



Sura: SWAAD 

Aya : 88

وَلَتَعۡلَمُنَّ نَبَأَهُۥ بَعۡدَ حِينِۭ

Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda