Sura: A’BASA

Aya : 31

وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا

Na matunda na majani ya malisho ya wanyama



Sura: A’BASA

Aya : 32

مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu wa mifugo



Sura: A’BASA

Aya : 33

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ

Basi utakapokuja ukelele mkali, (wenye kuumiza masikio)



Sura: A’BASA

Aya : 34

يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ

Siku ambayo, Mtu atakapomkimbia ndugu yake



Sura: A’BASA

Aya : 35

وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ

Na mama yake na baba yake



Sura: A’BASA

Aya : 36

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ

Na mkewe na wanae



Sura: A’BASA

Aya : 37

لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ

(Kwasababu) Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha yeye mwenyewe



Sura: A’BASA

Aya : 38

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ

Siku hiyo ziko nyuso zitakazo nawiri



Sura: A’BASA

Aya : 39

ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ

Zikicheka na kufurahika, (na zitachangamka)



Sura: A’BASA

Aya : 40

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ

Na ziko nyuso siku hiyo zitakuwa na vumbi juu yake



Sura: A’BASA

Aya : 41

تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ

Zitafunikwa na giza zito



Sura: A’BASA

Aya : 42

أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ

Hao ndio makafiri watenda maovu