Sura: AN-FAL 

Aya : 31

وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُنَا قَالُواْ قَدۡ سَمِعۡنَا لَوۡ نَشَآءُ لَقُلۡنَا مِثۡلَ هَٰذَآ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na (Washirikina) wanaposomewa Aya zetu, husema: “Tumesikia; laiti tungetaka (nasi) tungesema kama hii (Qur’ani). Hii (Qur’an) si chochote ila ni ngano za watu wa kale tu”



Sura: AN-FAL 

Aya : 32

وَإِذۡ قَالُواْ ٱللَّهُمَّ إِن كَانَ هَٰذَا هُوَ ٱلۡحَقَّ مِنۡ عِندِكَ فَأَمۡطِرۡ عَلَيۡنَا حِجَارَةٗ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ أَوِ ٱئۡتِنَا بِعَذَابٍ أَلِيمٖ

Na (kumbuka) wakati (washirikina) waliposema: Ewe Allah, ikiwa ni kweli hii (Qur’an) inatoka kwako, basi tushushie (mvua ya) mawe kutoka mbinguni (kama ulivyowafanyia watu wa Nabii Luti) au tuletee adhabu (yoyote) inayoumiza sana



Sura: AN-FAL 

Aya : 33

وَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيُعَذِّبَهُمۡ وَأَنتَ فِيهِمۡۚ وَمَا كَانَ ٱللَّهُ مُعَذِّبَهُمۡ وَهُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ

Na Allah hakuwa Mwenye kuwaadhibu (kuwaangamiza washirikina kama walivyoomba) ilhali nawe upo nao, na Allah si mwenye kuwaadhibu na ilhali wanaomba msamaha



Sura: AN-FAL 

Aya : 34

وَمَا لَهُمۡ أَلَّا يُعَذِّبَهُمُ ٱللَّهُ وَهُمۡ يَصُدُّونَ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ وَمَا كَانُوٓاْ أَوۡلِيَآءَهُۥٓۚ إِنۡ أَوۡلِيَآؤُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُتَّقُونَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na (Washirikina) wana jambo gani (jema) hata Allah asiwaadhibu (asiwaangamize), na ilhali wanauwekea vikwazo Msikiti Mtukufu (kwa kuwazuia watu kwenda kutekeleza ibada) na wala wao hawakuwa waangalizi wake? Hawakuwa waangalizi wake ila wachaMungu tu, lakini wengi wao hawajui (kuwa hawana haki hiyo ya uangalizi wa Msikiti Mtukufu)



Sura: AN-FAL 

Aya : 35

وَمَا كَانَ صَلَاتُهُمۡ عِندَ ٱلۡبَيۡتِ إِلَّا مُكَآءٗ وَتَصۡدِيَةٗۚ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ

Na haikuwa (Swala) ibada yao kwenye Nyumba (Al Kaaba) ila ni kupiga miruzi na makofi tu. Basi (enyi Washirikina) onjeni adhabu (ya duniani kwa kupigwa kwenye vita vya Badri) (na adhabu ya huko Akhera inawangojeni) kwa vile mlivyokuwa mnakufuru



Sura: AN-FAL 

Aya : 36

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمۡ لِيَصُدُّواْ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ فَسَيُنفِقُونَهَا ثُمَّ تَكُونُ عَلَيۡهِمۡ حَسۡرَةٗ ثُمَّ يُغۡلَبُونَۗ وَٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِلَىٰ جَهَنَّمَ يُحۡشَرُونَ

Hakika wale waliokufuru hutoa mali zao ili kuzuia (kuiwekea vikwazo) njia ya Allah (Uislamu usimakinike na watu wasiufuate). Basi watazitoa (mali zao hizo), kisha zitakuwa majuto kwao, kisha watashindwa. Na waliokufuru watakusanywa katika Jahanamu tu



Sura: AN-FAL 

Aya : 37

لِيَمِيزَ ٱللَّهُ ٱلۡخَبِيثَ مِنَ ٱلطَّيِّبِ وَيَجۡعَلَ ٱلۡخَبِيثَ بَعۡضَهُۥ عَلَىٰ بَعۡضٖ فَيَرۡكُمَهُۥ جَمِيعٗا فَيَجۡعَلَهُۥ فِي جَهَنَّمَۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Allah (aliyafanya hayo) ili awapambanue waovu dhidi ya wema, na kuwaweka waovu juu ya waovu wengine warundikane wote pamoja, na kisha awatumbukize katika Jahanamu. Hao ndio waliohasirika (duniani na Akhera)



Sura: AN-FAL 

Aya : 38

قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِن يَنتَهُواْ يُغۡفَرۡ لَهُم مَّا قَدۡ سَلَفَ وَإِن يَعُودُواْ فَقَدۡ مَضَتۡ سُنَّتُ ٱلۡأَوَّلِينَ

(Ewe Nabii Muhammad) Waambie waliokufuru kwamba: Iwapo watakoma (Washirikina, kuwafanyia uadui Waislamu na kuwapiga vita) watasamehewa yaliyokwishapita. Na wakirudi (kwenye maovu yao hayo) basi imekwishapita mifano (kama hii ya kuangamiza) kwa watu wa kale (nao wangoje kuangamizwa kama wenzao waliopita)



Sura: AN-FAL 

Aya : 39

وَقَٰتِلُوهُمۡ حَتَّىٰ لَا تَكُونَ فِتۡنَةٞ وَيَكُونَ ٱلدِّينُ كُلُّهُۥ لِلَّهِۚ فَإِنِ ٱنتَهَوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِمَا يَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Na piganeni nao (Washirikina) mpaka fitina (mateso dhidi ya Waislamu) yasiwepo, na Dini yote iwe ya Allah. Basi wakiacha, hakika Allah anayaona wanayoyatenda



Sura: AN-FAL 

Aya : 40

وَإِن تَوَلَّوۡاْ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ مَوۡلَىٰكُمۡۚ نِعۡمَ ٱلۡمَوۡلَىٰ وَنِعۡمَ ٱلنَّصِيرُ

Na kama wakigeuka (na kuamua kuendelea na uadui wao) basi jueni kwamba, Allah ndiye Mtetezi wenu. Mtetezi bora kabisa na Msaidizi bora kabisa ni yeye



Sura: AN-FAL 

Aya : 41

۞وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا غَنِمۡتُم مِّن شَيۡءٖ فَأَنَّ لِلَّهِ خُمُسَهُۥ وَلِلرَّسُولِ وَلِذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِ إِن كُنتُمۡ ءَامَنتُم بِٱللَّهِ وَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَىٰ عَبۡدِنَا يَوۡمَ ٱلۡفُرۡقَانِ يَوۡمَ ٱلۡتَقَى ٱلۡجَمۡعَانِۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Na jueni ya kwamba, ngawira[1] yoyote mnayoipata, basi khumsi (moja ya tano 1/5) ni ya Allah na Mtume na jamaa (wa Mtume) na mayatima na masikini na msafiri, ikiwa nyinyi mmemuamini Allah na tuliyoyateremsha kwa mja wetu siku ya upambanuzi (siku ya vita vya Badri), siku yalipokutana majeshi mawili. Na Allah ni Muweza wa kila kitu


1- - Ngawira ni mali ya makafiri itekwayo na wapiganaji wa Kiislamu katika vita vya Jihadi na ambayo
hugawanya mafungu matano, mafungu manne ni ya wapiganaji na fungu la tano “Khumsi” ndio la Allah
na Mtumewe na ambalo hugawanywa mafungu matano...


Sura: AN-FAL 

Aya : 42

إِذۡ أَنتُم بِٱلۡعُدۡوَةِ ٱلدُّنۡيَا وَهُم بِٱلۡعُدۡوَةِ ٱلۡقُصۡوَىٰ وَٱلرَّكۡبُ أَسۡفَلَ مِنكُمۡۚ وَلَوۡ تَوَاعَدتُّمۡ لَٱخۡتَلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡمِيعَٰدِ وَلَٰكِن لِّيَقۡضِيَ ٱللَّهُ أَمۡرٗا كَانَ مَفۡعُولٗا لِّيَهۡلِكَ مَنۡ هَلَكَ عَنۢ بَيِّنَةٖ وَيَحۡيَىٰ مَنۡ حَيَّ عَنۢ بَيِّنَةٖۗ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَسَمِيعٌ عَلِيمٌ

(Kumbukeni) Wakati nyinyi mlipokuwa kando ya bonde la karibu (na Madina), na wao (makafiri) walikuwa upande wa bonde la mbali (na Madina), na ilhali msafara (wa Abu Sufiyan) ukiwa chini zaidi yenu. Na ingelikuwa mmeagana (nyinyi na majeshi ya Makureishi) bila shaka mngetafautiana katika miadi (ya kufika Badri). Lakini (mkakutana) ili Allah atimize jambo lililokuwa lazima litendeke, ili aangamie wa kuangamia kwa dalili zilizo wazi, na asalimike wa kusalimika kwa dalili zilizo wazi. Na kwa hakika kabisa, Allah ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua



Sura: AN-FAL 

Aya : 43

إِذۡ يُرِيكَهُمُ ٱللَّهُ فِي مَنَامِكَ قَلِيلٗاۖ وَلَوۡ أَرَىٰكَهُمۡ كَثِيرٗا لَّفَشِلۡتُمۡ وَلَتَنَٰزَعۡتُمۡ فِي ٱلۡأَمۡرِ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ سَلَّمَۚ إِنَّهُۥ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ

(Kumbuka) Wakati Allah ana-kuonyesha usingizini mwako (kabla ya vita) kwamba wao (makafiri ni) wachache. Na lau angekuonyesha kuwa (makafiri) ni wengi, kwa yakini kabisa mngeingiwa na woga na mngelizozana katika jambo (hilo). Lakini Allah akaleta salama. Hakika, Yeye (Allah) ni Mwenye kuyajua yaliyomo nyoyoni



Sura: AN-FAL 

Aya : 44

وَإِذۡ يُرِيكُمُوهُمۡ إِذِ ٱلۡتَقَيۡتُمۡ فِيٓ أَعۡيُنِكُمۡ قَلِيلٗا وَيُقَلِّلُكُمۡ فِيٓ أَعۡيُنِهِمۡ لِيَقۡضِيَ ٱللَّهُ أَمۡرٗا كَانَ مَفۡعُولٗاۗ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ

Na (kumbukeni) wakati (Allah) anakuonyesheni machoni mwenu mlipokutana (nao) kuwa wao ni wachache mno, na anakufanyeni nyinyi wachache machoni mwao, ili Allah atimize jambo lililokuwa liwe[1]. Na kwa Allah tu hurejeshwa mambo yote


1- - Allah amelizungumzia tukio hili pia katika Sura Al-imran (3) 13: “Hakika imepetikana Aya kubwa
kwenu katika yale makundi mawili yaliyokutana (Siku ya Badri); kundi moja likipigana katika njia ya Allah
na jingine limekufuru. (Makafiri wakawaona (Waislamu) wapo zaidi kuliko wao mara mbili kwa kuona
kwa macho; na Allah humtia nguvu amtakaye kwa nusra yake. Kwa yakini katika hayo yapo mazingatio
kwa mwenye upeo.”


Sura: AN-FAL 

Aya : 45

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا لَقِيتُمۡ فِئَةٗ فَٱثۡبُتُواْ وَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا لَّعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ

Enyi mlioamini, mkikutana na jeshi (la makafiri), basi kuweni thabiti (kuweni imara na msikimbie), na mtajeni sana Allah (muombeni) ili mpate kufanikiwa



Sura: AN-FAL 

Aya : 46

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَا تَنَٰزَعُواْ فَتَفۡشَلُواْ وَتَذۡهَبَ رِيحُكُمۡۖ وَٱصۡبِرُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Na mtiini Allah na Mtume wake, wala msizozane mtasambaratika (na woga utakutawaleni) na nguvu zenu zitatoweka. Na vumilieni. Hakika Allah yupo pamoja na wavumilivu



Sura: AN-FAL 

Aya : 47

وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ خَرَجُواْ مِن دِيَٰرِهِم بَطَرٗا وَرِئَآءَ ٱلنَّاسِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ بِمَا يَعۡمَلُونَ مُحِيطٞ

Na msiwe kama wale (washi-rikina) waliotoka majumbani mwao (chini ya ujemedari wa Abu Jahali) kwa mbwembwe na kujionyesha kwa watu (ili wasifiwe)[1], na wanawazuia (watu) kwenye njia ya Allah (wasijiunge na Uislamu). Na Allah anayajua vyema yote wayafanyayo


1- - Kuwa nguvu za kuwapiga Waislamu wanazo, uwezo wanao na nia wanayo.


Sura: AN-FAL 

Aya : 48

وَإِذۡ زَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَعۡمَٰلَهُمۡ وَقَالَ لَا غَالِبَ لَكُمُ ٱلۡيَوۡمَ مِنَ ٱلنَّاسِ وَإِنِّي جَارٞ لَّكُمۡۖ فَلَمَّا تَرَآءَتِ ٱلۡفِئَتَانِ نَكَصَ عَلَىٰ عَقِبَيۡهِ وَقَالَ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّنكُمۡ إِنِّيٓ أَرَىٰ مَا لَا تَرَوۡنَ إِنِّيٓ أَخَافُ ٱللَّهَۚ وَٱللَّهُ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Na (kumbukeni) wakati Shetani alipowapambia (alipowaaminisha makafiri kwamba) amali zao (ni nzuri) na akawaambia: Leo hii hakuna watu wa kukushindeni, na hakika mimi nipo bega kwa bega na nyinyi (nitakunusuruni). Basi yalipoona na majeshi mawili (na kukabiliana macho kwa macho), (shetani) alirudi nyuma na akasema: Mimi sipo pamoja nanyi. Mimi naona msiyoyaona. Mimi namuogopa Allah, na Allah ni mkali wa kuadhibu



Sura: AN-FAL 

Aya : 49

إِذۡ يَقُولُ ٱلۡمُنَٰفِقُونَ وَٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ غَرَّ هَـٰٓؤُلَآءِ دِينُهُمۡۗ وَمَن يَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِ فَإِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ

(Kumbuka) Wakati wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao (watu wapya katika Uislamu) wanasema (kuwa): Hawa (Waislamu) dini yao imewadanganya (kwamba watashinda pamoja na uchache wao). Na Mwenye kumtegemea Allah, basi hakika Allah ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima



Sura: AN-FAL 

Aya : 50

وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ يَتَوَفَّى ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَضۡرِبُونَ وُجُوهَهُمۡ وَأَدۡبَٰرَهُمۡ وَذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡحَرِيقِ

Na laiti (ewe Muhammad ungekuwa) unaona wakati Malaika wanawaua makafiri huku wakizipiga nyuso zao na migongo yao na (kuwaambia): Onjeni adhabu ya kuungua (ungeona jambo kubwa la kutisha)



Sura: AN-FAL 

Aya : 51

ذَٰلِكَ بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيكُمۡ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَيۡسَ بِظَلَّـٰمٖ لِّلۡعَبِيدِ

Hilo (la kuwafanyia hivyo makafiri kwenye vita vya Badri) ni kwasababu ya yale yaliyotangulizwa (yaliyofanywa) na mikono yenu (nyinyi makafiri kwa kuwanyanyasa Waislamu), na hakika Allah kamwe si Mwenye kuwadhulumu waja



Sura: AN-FAL 

Aya : 52

كَدَأۡبِ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ فَأَخَذَهُمُ ٱللَّهُ بِذُنُوبِهِمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ قَوِيّٞ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

(Ada hii ya kuwaadhibu makafiri ni endelevu na ni) Kama ada ya (kuangamizwa kwa) watu wa Firauni na (makafiri wengine) waliokuwepo kabla yao; walizikufuru Aya za Allah, basi Allah aliwachukulia hatua (ya kuwaangamiza) kwasababu ya dhambi zao. Hakika, Allah ni Mwenye nguvu kubwa, Mkali wa kuadhibu



Sura: AN-FAL 

Aya : 53

ذَٰلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ لَمۡ يَكُ مُغَيِّرٗا نِّعۡمَةً أَنۡعَمَهَا عَلَىٰ قَوۡمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُواْ مَا بِأَنفُسِهِمۡ وَأَنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٞ

Hiyo (ada ya kuwaadhibu makafiri au kuchukua neema zake) ni kwasababu Allah habadilishi neema zozote alizo waneemesha watu, mpaka wao wabadilishe yaliyomo nafsini mwao. Na hakika Allah ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua



Sura: AN-FAL 

Aya : 54

كَدَأۡبِ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ فَأَهۡلَكۡنَٰهُم بِذُنُوبِهِمۡ وَأَغۡرَقۡنَآ ءَالَ فِرۡعَوۡنَۚ وَكُلّٞ كَانُواْ ظَٰلِمِينَ

(Hali ya Makafiri wa Kikureshi) Ni kama desturi ya watu wa Firauni na waliokuwepo kabla yao; walizipinga Aya za Mola wao Mlezi, basi tuliwaangamiza kwasababu ya dhambi zao na tuliwazamisha majini watu wa Firauni. Na wote walikuwa madhalimu



Sura: AN-FAL 

Aya : 55

إِنَّ شَرَّ ٱلدَّوَآبِّ عِندَ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hakika viumbe waovu mno mbele ya Allah ni wale waliokufuru, kwasababu hawaamini (upekee wa Allah na uweza wake)



Sura: AN-FAL 

Aya : 56

ٱلَّذِينَ عَٰهَدتَّ مِنۡهُمۡ ثُمَّ يَنقُضُونَ عَهۡدَهُمۡ فِي كُلِّ مَرَّةٖ وَهُمۡ لَا يَتَّقُونَ

Ambao miongoni mwao umeingia[1] nao maafikiano (mikataba) kwamba wasiwasaidie makafiri), kisha wanavunja maafikiano yao kila mara, na hawaogopi (wala hawajali)


1- - Wayahudi wa kabila la Quraidha


Sura: AN-FAL 

Aya : 57

فَإِمَّا تَثۡقَفَنَّهُمۡ فِي ٱلۡحَرۡبِ فَشَرِّدۡ بِهِم مَّنۡ خَلۡفَهُمۡ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ

Basi ukiwakuta vitani wafurushe (kisawa sawa ili uwaogopeshe (makafiri wengine) walioko nyuma yao ili wapate kukumbuka (wasithubutu tena kukuchezea na kuuchezea Uislamu)



Sura: AN-FAL 

Aya : 58

وَإِمَّا تَخَافَنَّ مِن قَوۡمٍ خِيَانَةٗ فَٱنۢبِذۡ إِلَيۡهِمۡ عَلَىٰ سَوَآءٍۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡخَآئِنِينَ

Na ukihofu (ukibaini) khiyana kwa watu wowote, basi watupie (mbali) ahadi yao (na wapige ili wewe na wao) muwe sawa (katika kuvunja ahadi). Hakika, Allah hawapendi wafanyao khiyana



Sura: AN-FAL 

Aya : 59

وَلَا يَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ سَبَقُوٓاْۚ إِنَّهُمۡ لَا يُعۡجِزُونَ

Na wasidhani wale waliokufuru (ambao walinusurika katika vita vya Badri) kwamba, wametangulia mbele (hawapatikani na hawaadhibiwi). Hakika, hawamshindi (yeyote kuwapata)



Sura: AN-FAL 

Aya : 60

وَأَعِدُّواْ لَهُم مَّا ٱسۡتَطَعۡتُم مِّن قُوَّةٖ وَمِن رِّبَاطِ ٱلۡخَيۡلِ تُرۡهِبُونَ بِهِۦ عَدُوَّ ٱللَّهِ وَعَدُوَّكُمۡ وَءَاخَرِينَ مِن دُونِهِمۡ لَا تَعۡلَمُونَهُمُ ٱللَّهُ يَعۡلَمُهُمۡۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِن شَيۡءٖ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ يُوَفَّ إِلَيۡكُمۡ وَأَنتُمۡ لَا تُظۡلَمُونَ

Na (Enyi Waislamu) waandalieni (maadui zenu) nguvu yoyote muiwezayo, na kwa farasi walioandaliwa (kwa Jihadi) ili kwa maandalizi hayo muwatishe maadui wa Allah na maadui zenu na (maadui) wengine tofauti na hao ambao nyinyi hamuwajui, (lakini) Allah anawajua. Na chochote mnachokitoa katika njia ya Allah kitalipwa kwa ukamilifu nanyi hamtadhulumiwa