Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 39

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika watu wa mwanzo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 40

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na kundi kubwa katika watu wa mwishoni



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 43

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi mnene wa joto kali mno



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 44

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si cha baridi na wala si cha kunufaisha



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 45

إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ

Hakika walikua kabla ya hapo kwenye maisha ya neema na anasa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 46

وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ

Na walikuwa wakishikilia kufanya dhambi kubwa mno



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 47

وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Na walikuwa wakisema: Je, hivi tutakapo kufa na tukawa udongo na mifupa, je hivi sisi hakika tutafufuliwa?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 48

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Au na wazee wetu wa mwanzo?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 49

قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ

Sema; Hakika wa mwanzo na wa mwisho,



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 50

لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Hakika watakusanywa kwenye wakati na siku maalumu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 51

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha hakika nyinyi enyi wapotovu mnaokadhibisha



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 52

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Hakika mtakula chakula kitokanacho na mti wa mzakoum



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 53

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi mtajaza kutokana na mti huo matumbo yenu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 54

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na mtakunywa juu yake maji ya moto ya chemkayo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 55

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa unywaji wa ngamia mwenye kiu kubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 56

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Haya ndio mapokezi yao Siku ya Malipo! (Kiyama)



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 57

نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ

Sisi Tumekuumbeni, basi kwa nini hamsadikishi hilo?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 58

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ

Je, mnaona mbegu ya uzazi mnayo imwagia kwa nguvu?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 59

ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Je, nyinyi ndio mnaiumba au sisi ndio Waumbaji?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 60

نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ

Sisi tumekadiria kati yenu umauti na haikua sisi wenye kukimbiwa