Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 31

مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيٗا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 32

وَلَقَدِ ٱخۡتَرۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ عِلۡمٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 33

وَءَاتَيۡنَٰهُم مِّنَ ٱلۡأٓيَٰتِ مَا فِيهِ بَلَـٰٓؤٞاْ مُّبِينٌ

Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 34

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ

Hakika hawa wanasema:



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 35

إِنۡ هِيَ إِلَّا مَوۡتَتُنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُنشَرِينَ

Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 36

فَأۡتُواْ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 37

أَهُمۡ خَيۡرٌ أَمۡ قَوۡمُ تُبَّعٖ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ أَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ

Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa’ na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 38

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا لَٰعِبِينَ

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 39

مَا خَلَقۡنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 40

إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ مِيقَٰتُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 41

يَوۡمَ لَا يُغۡنِي مَوۡلًى عَن مَّوۡلٗى شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 42

إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Isipo kuwa atakaye mrehemu Allah. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 43

إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ

Hakika Mti wa Zaqqum



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 44

طَعَامُ ٱلۡأَثِيمِ

Ni chakula cha mwenye dhambi



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 45

كَٱلۡمُهۡلِ يَغۡلِي فِي ٱلۡبُطُونِ

Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 46

كَغَلۡيِ ٱلۡحَمِيمِ

Kama kutokota kwa maji ya moto



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 47

خُذُوهُ فَٱعۡتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 48

ثُمَّ صُبُّواْ فَوۡقَ رَأۡسِهِۦ مِنۡ عَذَابِ ٱلۡحَمِيمِ

Kisha mwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 49

ذُقۡ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡكَرِيمُ

Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 50

إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمۡتَرُونَ

Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 51

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 52

فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani na chemchem



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 53

يَلۡبَسُونَ مِن سُندُسٖ وَإِسۡتَبۡرَقٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 54

كَذَٰلِكَ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurulaini



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 55

يَدۡعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ

Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 56

لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰۖ وَوَقَىٰهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Allah) atawalinda na adhabu ya Jahannamu



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 57

فَضۡلٗا مِّن رَّبِّكَۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 58

فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Basi tumeifanya nyepesi hii Qur’ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka



Sura: ADDUKHAAN 

Aya : 59

فَٱرۡتَقِبۡ إِنَّهُم مُّرۡتَقِبُونَ

Ngoja tu, na wao wangoje pia