Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 31

قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 32

فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 33

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ

Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 34

قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ

(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 35

يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ

Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 36

قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 37

يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 38

فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 39

وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ

Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 40

لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 41

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 42

قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 43

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ

Mussa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 44

فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ

Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 45

فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ

Mussa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 46

فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

Hapo wachawi walipinduka wakasujudu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 47

قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 48

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Mola Mlezi wa Mussa na Harun



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 49

قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Firauni) akasema: Je! Mme-muamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 50

قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ

Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 51

إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 52

۞وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Na tulimuamrisha Mussa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 53

فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 54

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ

(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 55

وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ

Nao wanatuudhi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 56

وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ

Na sisi ni wengi, wenye kuchukua tahadhari



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 57

فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 58

وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ

Na makhazina, na vyeo vya heshima



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 59

كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 60

فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ

Basi wakawafuata lilipo chomoza jua