Sura: QAAF 

Aya : 30

يَوۡمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ ٱمۡتَلَأۡتِ وَتَقُولُ هَلۡ مِن مَّزِيدٖ

Siku Tutakapoiambia Jahannam: Je, umeshajaa? Nayo itasema: Je, kuna ziada yoyote?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 43

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi mnene wa joto kali mno



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 44

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si cha baridi na wala si cha kunufaisha



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 51

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha hakika nyinyi enyi wapotovu mnaokadhibisha



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 52

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Hakika mtakula chakula kitokanacho na mti wa mzakoum



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 53

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi mtajaza kutokana na mti huo matumbo yenu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 54

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na mtakunywa juu yake maji ya moto ya chemkayo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 55

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa unywaji wa ngamia mwenye kiu kubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 56

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Haya ndio mapokezi yao Siku ya Malipo! (Kiyama)



Sura: ATTAHRIIM 

Aya : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ وَأَهۡلِيكُمۡ نَارٗا وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُ عَلَيۡهَا مَلَـٰٓئِكَةٌ غِلَاظٞ شِدَادٞ لَّا يَعۡصُونَ ٱللَّهَ مَآ أَمَرَهُمۡ وَيَفۡعَلُونَ مَا يُؤۡمَرُونَ

Enyi walioamini! Jikingeni nafsi zenu na ahli zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe; Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Allah kwa yale Anayowaamrisha na wanafanya yale wanayoamrishwa



Sura: AL-MULK 

Aya : 6

وَلِلَّذِينَ كَفَرُواْ بِرَبِّهِمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Na kwa walio mkufuru Mola wao Mlezi ipo adhabu ya Jahanamu. Na ni marejeo maovu yalioje hayo!



Sura: AL-MULK 

Aya : 7

إِذَآ أُلۡقُواْ فِيهَا سَمِعُواْ لَهَا شَهِيقٗا وَهِيَ تَفُورُ

Watakapotupwa humo watausikia mngurumo wake na huku inafoka



Sura: AL-MULK 

Aya : 8

تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ ٱلۡغَيۡظِۖ كُلَّمَآ أُلۡقِيَ فِيهَا فَوۡجٞ سَأَلَهُمۡ خَزَنَتُهَآ أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ نَذِيرٞ

Unakaribia kupasuka kwa hasira. Kila mara litakapotupwa humo kundi, walinzi wake watawauliza: Je, hakukufikieni muonyaji?



Sura: ALHAAQQA 

Aya : 31

ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ

Kisha kwenye moto uwakao vikali mtupeni humo!



Sura: ALHAAQQA 

Aya : 32

ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ

Mkamateni Na Mtieni Minyororo Shingoni Mwake,



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 15

كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

Sio hivyo (Hayawezekani hayo). Kwa hakika, huo ni Moto mkali kabisa



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 16

نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ

Unaobabua kwa nguvu ngozi ya kichwani na mwilini



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 17

تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Unamwita yule aliyegeuza mgongo (aliyepuuza muongozo wa Allah) na akakengeuka



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 18

وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ

Na akakusanya (mali) kisha akayahifadhi (katika makasha)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 26

سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ

Nitamuingiza (na kumuunguza) kwenye Moto wa saqar



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 27

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ

Na ni nini kitakujuulisha nini huo Moto wa Saqar?



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 28

لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ

Haubakishi wala hauachi, (kitu chochote)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 29

لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ

Wenye kubabua vikali ngozi, (iwe nyeusi)



Sura: AL-INSAAN

Aya : 4

إِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ سَلَٰسِلَاْ وَأَغۡلَٰلٗا وَسَعِيرًا

Hakika sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na moto mkali



Sura: ALMURSALAAT 

Aya : 30

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ

Nendeni kwenye kivuli chenye sehemu tatu!



Sura: ALMURSALAAT 

Aya : 31

لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ

Hakiwafuniki, na wala hakiwa-kingi na muwako wa moto



Sura: ALMURSALAAT 

Aya : 32

إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ

Hakika Moto huo hurusha macheche Kama majumba!



Sura: ALMURSALAAT 

Aya : 33

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ

Kana kwamba ni ngamia waku-bwa wa rangi ya manjano!



Sura: ANNABAI 

Aya : 21

إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا

Hakika moto wa Jahannamu utakuwa ni wenye kuvizia