Sura: AL-AALAA 

Aya : 1

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى

Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,



Sura: AL-AALAA 

Aya : 2

ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ

Aliye umba, na akaweka sawa,



Sura: AL-AALAA 

Aya : 3

وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ

Na ambaye amekadiria na akaongoa,



Sura: AL-AALAA 

Aya : 4

وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ

Na aliye otesha malisho,



Sura: AL-AALAA 

Aya : 5

فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ

Kisha akayafanya makavu, meusi



Sura: AL-AALAA 

Aya : 6

سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ

Tutakusomesha wala hutasahau,



Sura: AL-AALAA 

Aya : 7

إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ

Ila akipenda Allah. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana



Sura: AL-AALAA 

Aya : 8

وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ

Na tutakusahilishia yawe mepesi



Sura: AL-AALAA 

Aya : 9

فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ

Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa



Sura: AL-AALAA 

Aya : 10

سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ

Atakumbuka mwenye kuogopa



Sura: AL-AALAA 

Aya : 11

وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى

Na atajitenga mbali nayo mpotovu,



Sura: AL-AALAA 

Aya : 12

ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Ambaye atauingia Moto mkubwa



Sura: AL-AALAA 

Aya : 13

ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ

Tena humo hatakufa wala hawi hai



Sura: AL-AALAA 

Aya : 14

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ

Hakika amekwisha fanikiwa aliyejitakasa



Sura: AL-AALAA 

Aya : 15

وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali



Sura: AL-AALAA 

Aya : 16

بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Lakini nyinyi mnakhiari (mnapenda sana) maisha ya dunia!



Sura: AL-AALAA 

Aya : 17

وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi



Sura: AL-AALAA 

Aya : 18

إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,



Sura: AL-AALAA 

Aya : 19

صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ

Vitabu vya Ibrahimu na Mussa