Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 1

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ

Mbingu itakapo chanika,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 2

وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ

Na nyota zitakapo tawanyika,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 3

وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ

Na bahari zitakapo pasuliwa,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 4

وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ

Na makaburi yatakapo fukuliwa,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 5

عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ

Hapo kila nafsi itajua ilichotanguliza, na ilicho bakisha nyuma



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ

Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 7

ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ

Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 8

فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ

Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 9

كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 10

وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 11

كِرَامٗا كَٰتِبِينَ

Waandishi wenye hishima,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 12

يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ

Wanayajua mnayo yatenda



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 13

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 14

وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 15

يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Wataingia humo Siku ya Malipo



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 16

وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ

Na hawatoacha kuwamo humo



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 17

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 18

ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 19

يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ

(Ni) Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu