Sura: ATTUR 

Aya : 1

وَٱلطُّورِ

Nina apa kwa mlima wa Tur



Sura: ATTUR 

Aya : 2

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na kwa kitabu kilichoandikwa



Sura: ATTUR 

Aya : 3

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika karatasi ya ngozi nyembamba iliyokunjuliwa



Sura: ATTUR 

Aya : 4

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na (nina apa) kwa Nyumba iliyoimarishwa (iliyojengwa imara)



Sura: ATTUR 

Aya : 5

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na (nina apa) kwa sakafu (za mbingu) zilizonyanyuliwa



Sura: ATTUR 

Aya : 6

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na (nina apa) kwa bahari yenye kuwashwa moto)



Sura: ATTUR 

Aya : 7

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

(Nina apa kwamba) Hakika, adhabu ya Mola wako Mlezi bila ya shaka yoyote itatokea



Sura: ATTUR 

Aya : 8

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia



Sura: ATTUR 

Aya : 9

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku hiyo mbingu itatikisika kutikisika kikweli



Sura: ATTUR 

Aya : 10

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na majabali yatatembea mwendo wa kasi



Sura: ATTUR 

Aya : 11

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao Siku hiyo kwa wakadhibishao



Sura: ATTUR 

Aya : 12

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wamo katika kushughulika na upuuzi wakicheza



Sura: ATTUR 

Aya : 13

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku watasukumwa katika Moto wa Jahannam kwa msukumo wa nguvu



Sura: ATTUR 

Aya : 14

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Huu ndio ule moto ambao mlikuwa mkiukadhibisha



Sura: ATTUR 

Aya : 15

أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ

Je, hivi ni uchawi huu au nyinyi hamuoni?



Sura: ATTUR 

Aya : 16

ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Ingieni muungue humo kwenye Jahannam, mkistahamili au msistahamili ni sawasawa kwenu, hakika hapana ila mnalipwa yale mliyokuwa mkiyatenda



Sura: ATTUR 

Aya : 17

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَعِيمٖ

Hakika ya wacha mungu watakua katika bustani na neema



Sura: ATTUR 

Aya : 18

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Wakifurahia kwa ambayo Amewapa Mola wao, na Akawaokoa na adhabu ya moto uwakao vikali mno



Sura: ATTUR 

Aya : 19

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa raha kwa sababu ya mliyokuwa mnatenda



Sura: ATTUR 

Aya : 20

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hali ya kuegemea juu ya makochi ya fakhari yaliyopangwa safu safu, na Tutawaozesha huwr ‘ayn, (wanawake weupe) wazuri wenye macho makubwa ya kupendeza



Sura: ATTUR 

Aya : 21

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ

Na wale walioamini na wakafuatwa na dhuriya wao kwa Imani Tutawakutanisha nao dhuriya wao na Hatutawapunguzia katika ‘amali zao kitu chochote. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma



Sura: ATTUR 

Aya : 22

وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na Tutawapa matunda na nyama katika ambavyo wanatamani



Sura: ATTUR 

Aya : 23

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ

Watabadilishana humo gilasi za mvinyo usiosababisha maneno ya upuuzi na wala ya dhambi



Sura: ATTUR 

Aya : 24

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ

Na watawazungukia watumishi vijana kwa ajili yao kana kwamba ni lulu zilizohifadhiwa



Sura: ATTUR 

Aya : 25

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Na watakabiliana baadhi yao kwa wengine wakiulizana



Sura: ATTUR 

Aya : 26

قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ

Watasema hakika sisi tulikua kabla ya hapa kwa watu wetu wenye kuwafanyia upole



Sura: ATTUR 

Aya : 27

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Basi Allah Akatufadhilisha, na Akatuokoa na adhabu ya mvuke wa moto (unaobabua)



Sura: ATTUR 

Aya : 28

إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Hakika sisi tulikuwa tunamuabudu kabla ya hapa hakika yeye ni mwema mwingi wa rehma



Sura: ATTUR 

Aya : 29

فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ

Basi kumbusha (Ewe Muhammad) na haukua wewe kwa neema ya mola wako mlezi kuhani wala mwendawazimu



Sura: ATTUR 

Aya : 30

أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ

Au wanasema (huyu Muhammad þ ni) mshairi, tunamtarajia kupatikana maafa ya dahari