Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 1

طسٓمٓ

Twaa Siin Miim



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 2

تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Hizo ni Aya za Kitabu kinacho-bainisha



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 3

لَعَلَّكَ بَٰخِعٞ نَّفۡسَكَ أَلَّا يَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ

Huenda ukaiumiza nafsi yako kwa kuwa (watu) hawawi Waumini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 4

إِن نَّشَأۡ نُنَزِّلۡ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةٗ فَظَلَّتۡ أَعۡنَٰقُهُمۡ لَهَا خَٰضِعِينَ

Tukitaka tutateremsha kutoka mbinguni muujiza ili shingo zao ziunyenyekee



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 5

وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ مُحۡدَثٍ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهُ مُعۡرِضِينَ

Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema) ila wao wana-jitenga nao



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 6

فَقَدۡ كَذَّبُواْ فَسَيَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَـٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Kwa yakini wamekanusha, kwa hivyo zitawajia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia mzaha



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 7

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَمۡ أَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ

Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 8

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 9

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 10

وَإِذۡ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئۡتِ ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Mussa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 11

قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَۚ أَلَا يَتَّقُونَ

Watu wa Firauni. Hawaogopi?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 12

قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ

Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 13

وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ

Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 14

وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ

Na wao wana kisasi juu yangu, kwahivyo naogopa wasije kuniuwa



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 15

قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ

Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 16

فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 17

أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Waachilie Wana wa Israili waende nasi



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 18

قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ

(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 19

وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 20

قَالَ فَعَلۡتُهَآ إِذٗا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

(Mussa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 21

فَفَرَرۡتُ مِنكُمۡ لَمَّا خِفۡتُكُمۡ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكۡمٗا وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Basi nikakumbieni nilipokuo-gopeni tena Mola wangu mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa mitume



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 22

وَتِلۡكَ نِعۡمَةٞ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنۡ عَبَّدتَّ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Na hiyo ndiyo neema ya kuni-sumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 23

قَالَ فِرۡعَوۡنُ وَمَا رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Firauni akasema: Ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 24

قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 25

قَالَ لِمَنۡ حَوۡلَهُۥٓ أَلَا تَسۡتَمِعُونَ

(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 26

قَالَ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

(Mussa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 27

قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ

(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 28

قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ

(Mussa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 29

قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ

(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani



Sura: ASH-SHUARAA 

Aya : 30

قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ

Akasema: Je! Ijapokuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?