Sura: AL-MASAD

Aya : 1

تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ

Imeangamia mikono ya Abulahab na yeye (kwa maana hiyo) ameangamia



Sura: AL-MASAD

Aya : 2

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ

Haitamfaa mali yake na (vitendo) alivyovichuma (alivyovifanya)



Sura: AL-MASAD

Aya : 3

سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ

Atauingia moto wenye muwako



Sura: AL-MASAD

Aya : 4

وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ

(Ataingia Motoni yeye) Na mkewe, mchukuzi mkubwa wa kuni



Sura: AL-MASAD

Aya : 5

فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ

Shingoni mwake iko kamba ya kusokotwa