سوره: AL-BURUJI 

آيه : 1

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 2

وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ

Na kwa siku iliyo ahidiwa!



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 3

وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 4

قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ

Wameangamizwa watu wa mahandaki



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 5

ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ

Yenye moto wenye kuni nyingi,



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 6

إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ

Walipo kuwa wamekaa hapo,



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 7

وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 8

وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Allah, Mwenye nguvu, Msifiwa,



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 9

ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Allah ni shaahidi wa kila kitu



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 11

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 12

إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 13

إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejesha tena,



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 14

وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 15

ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ

Mwenye Kiti cha Enzi,



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 16

فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ

Atendaye ayatakayo



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 17

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ

Je! Zimekufikia khabari za majeshi?



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 18

فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ

Ya Firauni na Thamudi?



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 19

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 20

وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ

Na Allah nyuma yao amewazunguka



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 21

بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ

Bali hii ni Qur’ani tukufu



سوره: AL-BURUJI 

آيه : 22

فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa