سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 1

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ

Nina apa kwa Siku ya Kiyama



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 2

وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ

Na nina apa kwa nafsi inayolaumu sana



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 3

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ

Je, mwanadamu anadhani kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 4

بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ

Ndio (tutaikusanya tu na) Tunao uwezo wa kuzifanya ziwe sawa sawa ncha za vidole vyake



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 5

بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ

Lakini mwanadamu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilizoko mbele yake



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 6

يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ

Anauliza: Ni lini hiyo Siku ya Kiyama?



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 7

فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ

Basi jicho litakapoduwaa (kwa kupatwa na bumbuwazi na fadhaa)



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 8

وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ

Na mwezi utakapo patwa,



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 9

وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ

Na vikakusanywa jua na mwezi ((Katika Kupatwa),



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 10

يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ

Atasema Mwanadamu siku hiyo: Wapi pa kukimbilia?



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 11

كَلَّا لَا وَزَرَ

La! Hapana mahala pa kukimbilia!



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 12

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ

Kwa Mola wako siku hiyo ndio makazi ya (ya kutulia)



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 13

يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ

Siku hiyo ataambiwa Mtu yale aliyo yatanguliza na aliyo yakawiza



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 14

بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ

Bali Mtu anajijua Vizuri Sana yeye mwenyewe



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 15

وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ

Ingawa atatoa nyudhuru chungu nzima



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 16

لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ

Usiutikisie ulimi wako huu wahyi (ufunuo) kwa kuufanyia haraka



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 17

إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ

Hakika ni juu Yetu kuikusanya na kukuwezesha kuisoma kwake



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 18

فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ

Basi Tunapoisoma (kupitia Jibrili), fuata kusomwa kwake



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 19

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ

Kisha ni juu yetu kuubainisha



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 20

كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 21

وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Na mnaacha maisha ya Akhera, (kwa kutoijali Akhera)



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 22

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ

Zipo Nyuso siku hiyo zitanawiri, (zitang’aa)



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 23

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ

Zikimtazama Mola wake



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 24

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ

Na nyuso (nyenginezo) siku hiyo zitakunjana



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 25

تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ

Zikiwa na yakini kuwa zitafikiwa na msiba unaovunja uti wa mgongo



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 26

كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ

Sivyo! Itakapofika (roho) kwenye mafupa ya koo, (mitulinga)



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 27

وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ

Na itasemwa: Ni nani tabibu wa kumponya?



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 28

وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 29

وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ

Na utakapo ambatanishwa muundi kwa muundi



سوره: ALQIYAAMA 

آيه : 30

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ

Siku hiyo ndiyo (ya) kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako! (ama Peponi au Motoni)