سوره: AL-QALAM 

آيه : 1

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ

Nuun. Nina apa kwa kalamu na yale wayoyaandika



سوره: AL-QALAM 

آيه : 2

مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ

(Kwamba) Wewe (Muhammad) kwa neema ya Mola wako Mlezi (aliyokupa) sio mwendawazimu



سوره: AL-QALAM 

آيه : 3

وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ

Na kwa hakika wewe una malipo (makubwa) yasiyo katika



سوره: AL-QALAM 

آيه : 4

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ

Na hakika wewe uko juu ya tabia njema sana



سوره: AL-QALAM 

آيه : 5

فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ

Basi hivi karibuni utaona, na wao wataona



سوره: AL-QALAM 

آيه : 6

بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ

(Kwamba) Ni nani mwenye kichaa miongoni mwenu



سوره: AL-QALAM 

آيه : 7

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Hakika, Mola wako Mlezi ndiye amjuae zaidi aliyepotea njia yake, ndiye awajuae zaidi walioongoka



سوره: AL-QALAM 

آيه : 8

فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Basi usiwatii wanao kadhibisha



سوره: AL-QALAM 

آيه : 9

وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ

Wangependa uwe laini (ulegeze msimamo wako), nao wawe laini (walegeze msimamo wao na wakufuate)



سوره: AL-QALAM 

آيه : 10

وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ

Wala usimtii kila mwapaji sana, aliye dhalili,



سوره: AL-QALAM 

آيه : 11

هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ

Mwingi wa kusengenya, mpitaji huku na kule kwa kufitinisha



سوره: AL-QALAM 

آيه : 12

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Mwingi wa kuzuia ya kheri, aliyependukia katika kuwadhulumu (Watu) mwingi wa kutenda dhambi



سوره: AL-QALAM 

آيه : 13

عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

Mkavu, na juu ya hayo ni mwana haramu (kujipachika tu kabila)



سوره: AL-QALAM 

آيه : 14

أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ

Kwakuwa tu ni mwenye kumiliki mali na watoto?



سوره: AL-QALAM 

آيه : 15

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!



سوره: AL-QALAM 

آيه : 16

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ

Karibuni tutamtia kovu juu ya pua



سوره: AL-QALAM 

آيه : 17

إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ

Hakika sisi Tumewajaribu (Maquraysh) kama Tulivyowajaribu watu wa shamba pale walipo apa kuwa bila shaka watayavuna (matunda yake) watakapo pambaukiwa asubuhi



سوره: AL-QALAM 

آيه : 18

وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ

Na wala hawakusema In-Shaa Allaah (Allah akipenda)!



سوره: AL-QALAM 

آيه : 19

فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ

Basi (shamba lao) likazungukwa na (moto) kutoka kwa mola wako ilihali wao wamelala



سوره: AL-QALAM 

آيه : 20

فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ

Likawa kama lilovunwa (ilion-g’olewa mimea yake)



سوره: AL-QALAM 

آيه : 21

فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ

Wakaitana, pale walipopam-baukiwa asubuhi



سوره: AL-QALAM 

آيه : 22

أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ

Kwamba nendeni asubuhi mapema shambani mwenu, mkiwa mnataka kuvuna



سوره: AL-QALAM 

آيه : 23

فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ

Wakatoka na huku wanakwenda kimya kimya wakinong’onezana



سوره: AL-QALAM 

آيه : 24

أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ

Wakisema kwamba:: leo Maskini asiingie humo mwenu kinyume cha utashi wenu



سوره: AL-QALAM 

آيه : 25

وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ

Wakatoka asubuhi mapema kwa kusudio la nguvu, wakidhani wana uwezo (wa kuwazuia maskini)



سوره: AL-QALAM 

آيه : 26

فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Basi walipoliona (shamba lao) wakasema: Hakika sisi bila shaka Tumepotea



سوره: AL-QALAM 

آيه : 27

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

(Walivyo tanabahi!): wakasema Bali sisi tumenyimwa (mavuno yake)!



سوره: AL-QALAM 

آيه : 28

قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Allah (kuiacha nia yenu mbaya)?



سوره: AL-QALAM 

آيه : 29

قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Wakasema: utukufu ni wa mola wetu, hakika tulikuwa wenye kudhulumu



سوره: AL-QALAM 

آيه : 30

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ

Basi Wakakabiliana wenyewe kwa wenyewe wakilaumiana