سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 1

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Wakati kitakapotokea Kiyama



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 2

لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ

Hakuna mpingaji wa kutokea kwake



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 3

خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ

Ni chenye kuwashusha hadhi (makafiri) na kuwanyanyua hadhi (waumini)



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 4

إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا

Wakati ardhi itakapotikiswa mtikiso mkubwa



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 5

وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا

Na milima ikapondwa pondwa upondwaji mkubwa



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 6

فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا

(Kwa sababu ya kupondwa pondwa huko, milima) ikawa vumbi lenye kutawanyika



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 7

وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ

Na nyinyi (watu) mtakuwa namna tatu



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 8

فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Basi watakuwepo watu wa kuliani. Je, ni kina nani watu wa kuliani?



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 9

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Na (watakuwepo) watu wa kushotoni. Je, ni kina nani watu wa kushotoni?



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 10

وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ

Na (watakuwepo) waliotangulia mbele, (basi) watakua mbele.[1]


1- - Hawa ni wale ambao walitangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya akhera.


سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 11

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakao kurubishwa



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 12

فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

katika pepo zenye neema



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 13

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika wa mwanzo



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 14

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na wachache katika wa mwishoni.[1]


1- - Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yalio tangulia na Manabii wao, na wachache katika Umma wa Muhammad rehma na amani ziwe juu yake ukilinganishwa na hao.


سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 15

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ

watakua juu ya vitanda vilivyofumwa vizuri



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 16

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ

hali wakiwa wameviegemea huku wakitazamana



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 17

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ

Watazungukiwa na vijana wenye kudumu



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 18

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ

Kwa bilauri na mabirika na vikombe vya mvinyo kutoka kwenye chemchemu



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 19

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Hawatapata maumivu ya kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawa-tatokwa na akili



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 20

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Na matunda watakayo pendelea wao



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 21

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na nyama za ndege katika wata-kazozitamani



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 22

وَحُورٌ عِينٞ

Na wanawake wenye macho makubwa yaliyo meupe sana na weusi sana



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 23

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Kama mfano wa lulu zilizohi-fadhiwa



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 24

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ikiwa ni malipo kwa ambayo walikuwa wanatenda (duniani)



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 25

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Hawatasikia humo maneno ya upuuzi wala yanayopelekea kupata madhambi



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 26

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipokuwa itasemwa: Salama, na Amani!



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 27

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na watu wa kuliani, ni wepi hao watu wa kuliani?



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 28

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 29

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa



سوره: AL-WAAQIA’H 

آيه : 30

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotandazwa