سوره: ANNAJMI 

آيه : 1

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ

Nina apa kwa nyota zinapozama



سوره: ANNAJMI 

آيه : 2

مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ

Hakupotoka swahibu wenu na wala hakupotoka



سوره: ANNAJMI 

آيه : 3

وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ

Na hasemi (neno lolote lile) kwa utashi wa nafsi (yake)



سوره: ANNAJMI 

آيه : 4

إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ

Hayakuwa hayo (anayaoyasema) isipokuwa tu ni Wahy unaofunuliwa



سوره: ANNAJMI 

آيه : 5

عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ

Amemfundisha (Malaika Jibrili) Mwenye nguvu kubwa



سوره: ANNAJMI 

آيه : 6

ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ

Mwenye nguvu na hekima na akakaa katika umbile lake halisi



سوره: ANNAJMI 

آيه : 7

وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Naye yuko juu kabisa katika upeo wa macho



سوره: ANNAJMI 

آيه : 8

ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ

Kisha akakurubia na akashuka



سوره: ANNAJMI 

آيه : 9

فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ

Kisha akawa kiasi cha umbali wa mipinde miwili au karibu zaidi



سوره: ANNAJMI 

آيه : 10

فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ

(Allah) Akamfunulia Wahy mja Wake yale Aliyomfunulia Wahy



سوره: ANNAJMI 

آيه : 11

مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ

Moyo (wake) haukukadhibisha yale aliyoyaona



سوره: ANNAJMI 

آيه : 12

أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Je, mnambishia kuhusu yale aliyoyaona?



سوره: ANNAJMI 

آيه : 13

وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ

Na hakika alimuona (Jibriyl) kwa mara nyingine



سوره: ANNAJMI 

آيه : 14

عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Kwenye mkunazi wa mpaka wa mwisho kabisa



سوره: ANNAJMI 

آيه : 15

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ

Karibu yake kuna Jannatu Al-Ma-waa



سوره: ANNAJMI 

آيه : 16

إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ

Ulipoufunika mkunazi huo hicho kilicho ufinika



سوره: ANNAJMI 

آيه : 17

مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Jicho lake halikukengeuka wala halikupindukia mipaka



سوره: ANNAJMI 

آيه : 18

لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ

Kwa yakini aliona miongoni mwa Aayaat (ishara, dalili) za Bwana wake kubwa kabisa



سوره: ANNAJMI 

آيه : 19

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّـٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ

Je, mmeona (masanamu) Laata na ‘Uzzaa?



سوره: ANNAJMI 

آيه : 20

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ

Na Manaata mwengine wa tatu?



سوره: ANNAJMI 

آيه : 21

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ

Je, nyinyi mna wana wa kiume Naye Ana wana wa kike?



سوره: ANNAJMI 

آيه : 22

تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ

Huo basi ni mgao wa dhulma!



سوره: ANNAJMI 

آيه : 23

إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ

Hayo si chochote isipokuwa ni majina mmeyaita nyinyi na baba zenu, wala Allah Hakuyateremshia dalili yoyote. Hawafuati isipokuwa dhana na yale yanayotamani nafsi (zao), na hali imekwishawajia kutoka kwa Bwana wao mwongozo



سوره: ANNAJMI 

آيه : 24

أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ

Kwani kila Mtu anapata kila anayoyatamani?



سوره: ANNAJMI 

آيه : 25

فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ

Na Allah ndiye mmiliki wa Akhera na Dunia



سوره: ANNAJMI 

آيه : 26

۞وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ

Na kuna malaika wengi mbinguni hainufaishi chochote uombezi wao ila baada ya kupewa idhini na Allah kwa amtakaye na amridhie



سوره: ANNAJMI 

آيه : 27

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ

Hakika wale wasioamini Aakhirah bila shaka wanawaita Malaika kwa majina ya kike



سوره: ANNAJMI 

آيه : 28

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا

Na wala hawana ujuzi wowote ule wa hayo; hawafuati isipokuwa dhana, na hakika dhana haifai kitu chochote mbele ya haki



سوره: ANNAJMI 

آيه : 29

فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Basi achana naye ambaye ameupa mgongo ukumbusho Wetu na wala hataki isipokuwa maisha ya dunia



سوره: ANNAJMI 

آيه : 30

ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ

Huo ndio upeo wao wa elimu. Hakika Bwana wako ni Mjuzi zaidi wa ambaye amepotoka njia Yake, Naye Mjuzi zaidi wa ambaye ameongoka