سوره: ATTUR 

آيه : 1

وَٱلطُّورِ

Nina apa kwa mlima wa Tur



سوره: ATTUR 

آيه : 2

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na kwa kitabu kilichoandikwa



سوره: ATTUR 

آيه : 3

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika karatasi ya ngozi nyembamba iliyokunjuliwa



سوره: ATTUR 

آيه : 4

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na (nina apa) kwa Nyumba iliyoimarishwa (iliyojengwa imara)



سوره: ATTUR 

آيه : 5

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na (nina apa) kwa sakafu (za mbingu) zilizonyanyuliwa



سوره: ATTUR 

آيه : 6

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na (nina apa) kwa bahari yenye kuwashwa moto)



سوره: ATTUR 

آيه : 7

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

(Nina apa kwamba) Hakika, adhabu ya Mola wako Mlezi bila ya shaka yoyote itatokea



سوره: ATTUR 

آيه : 8

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia



سوره: ATTUR 

آيه : 9

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku hiyo mbingu itatikisika kutikisika kikweli



سوره: ATTUR 

آيه : 10

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na majabali yatatembea mwendo wa kasi



سوره: ATTUR 

آيه : 11

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao Siku hiyo kwa wakadhibishao



سوره: ATTUR 

آيه : 12

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wamo katika kushughulika na upuuzi wakicheza



سوره: ATTUR 

آيه : 13

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku watasukumwa katika Moto wa Jahannam kwa msukumo wa nguvu



سوره: ATTUR 

آيه : 14

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Huu ndio ule moto ambao mlikuwa mkiukadhibisha



سوره: ATTUR 

آيه : 15

أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ

Je, hivi ni uchawi huu au nyinyi hamuoni?



سوره: ATTUR 

آيه : 16

ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Ingieni muungue humo kwenye Jahannam, mkistahamili au msistahamili ni sawasawa kwenu, hakika hapana ila mnalipwa yale mliyokuwa mkiyatenda



سوره: ATTUR 

آيه : 17

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَعِيمٖ

Hakika ya wacha mungu watakua katika bustani na neema



سوره: ATTUR 

آيه : 18

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Wakifurahia kwa ambayo Amewapa Mola wao, na Akawaokoa na adhabu ya moto uwakao vikali mno



سوره: ATTUR 

آيه : 19

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa raha kwa sababu ya mliyokuwa mnatenda



سوره: ATTUR 

آيه : 20

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hali ya kuegemea juu ya makochi ya fakhari yaliyopangwa safu safu, na Tutawaozesha huwr ‘ayn, (wanawake weupe) wazuri wenye macho makubwa ya kupendeza



سوره: ATTUR 

آيه : 21

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ

Na wale walioamini na wakafuatwa na dhuriya wao kwa Imani Tutawakutanisha nao dhuriya wao na Hatutawapunguzia katika ‘amali zao kitu chochote. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma



سوره: ATTUR 

آيه : 22

وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na Tutawapa matunda na nyama katika ambavyo wanatamani



سوره: ATTUR 

آيه : 23

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ

Watabadilishana humo gilasi za mvinyo usiosababisha maneno ya upuuzi na wala ya dhambi



سوره: ATTUR 

آيه : 24

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ

Na watawazungukia watumishi vijana kwa ajili yao kana kwamba ni lulu zilizohifadhiwa



سوره: ATTUR 

آيه : 25

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Na watakabiliana baadhi yao kwa wengine wakiulizana



سوره: ATTUR 

آيه : 26

قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ

Watasema hakika sisi tulikua kabla ya hapa kwa watu wetu wenye kuwafanyia upole



سوره: ATTUR 

آيه : 27

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Basi Allah Akatufadhilisha, na Akatuokoa na adhabu ya mvuke wa moto (unaobabua)



سوره: ATTUR 

آيه : 28

إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Hakika sisi tulikuwa tunamuabudu kabla ya hapa hakika yeye ni mwema mwingi wa rehma



سوره: ATTUR 

آيه : 29

فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ

Basi kumbusha (Ewe Muhammad) na haukua wewe kwa neema ya mola wako mlezi kuhani wala mwendawazimu



سوره: ATTUR 

آيه : 30

أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ

Au wanasema (huyu Muhammad þ ni) mshairi, tunamtarajia kupatikana maafa ya dahari