سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 1

حمٓ

Haamiim



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 2

وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Nina apa kwa Kitabu kinacho bainisha



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 3

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةٖ مُّبَٰرَكَةٍۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ

Hakika, tumekiteremsha (kitabu hiki cha Qur’ani) katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi tumekuwa waonyaji



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 4

فِيهَا يُفۡرَقُ كُلُّ أَمۡرٍ حَكِيمٍ

Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hekima



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 5

أَمۡرٗا مِّنۡ عِندِنَآۚ إِنَّا كُنَّا مُرۡسِلِينَ

Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 6

رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Ni rehema kutoka kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ndiye tu Mwenye kusikia sana, Mwenye kujua



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 7

رَبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyopo baina yake, ikiwa nyinyi mna yakini



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 8

لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 9

بَلۡ هُمۡ فِي شَكّٖ يَلۡعَبُونَ

Lakini wao wanacheza katika shaka



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 10

فَٱرۡتَقِبۡ يَوۡمَ تَأۡتِي ٱلسَّمَآءُ بِدُخَانٖ مُّبِينٖ

Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapoleta moshi ulio dhahiri



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 11

يَغۡشَى ٱلنَّاسَۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٞ

Utakaowafunika watu: Hii ni adhabu chungu!



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 12

رَّبَّنَا ٱكۡشِفۡ عَنَّا ٱلۡعَذَابَ إِنَّا مُؤۡمِنُونَ

Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 13

أَنَّىٰ لَهُمُ ٱلذِّكۡرَىٰ وَقَدۡ جَآءَهُمۡ رَسُولٞ مُّبِينٞ

Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwishawafikia Mtume mwenye kubainisha



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 14

ثُمَّ تَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ وَقَالُواْ مُعَلَّمٞ مَّجۡنُونٌ

Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 15

إِنَّا كَاشِفُواْ ٱلۡعَذَابِ قَلِيلًاۚ إِنَّكُمۡ عَآئِدُونَ

Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 16

يَوۡمَ نَبۡطِشُ ٱلۡبَطۡشَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ إِنَّا مُنتَقِمُونَ

Siku tutakayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 17

۞وَلَقَدۡ فَتَنَّا قَبۡلَهُمۡ قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَ وَجَآءَهُمۡ رَسُولٞ كَرِيمٌ

Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 18

أَنۡ أَدُّوٓاْ إِلَيَّ عِبَادَ ٱللَّهِۖ إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Akasema: Nipeni waja wa Allah; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 19

وَأَن لَّا تَعۡلُواْ عَلَى ٱللَّهِۖ إِنِّيٓ ءَاتِيكُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ

Na msimfanyie kiburi Allah; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 20

وَإِنِّي عُذۡتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمۡ أَن تَرۡجُمُونِ

Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 21

وَإِن لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ لِي فَٱعۡتَزِلُونِ

Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 22

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ قَوۡمٞ مُّجۡرِمُونَ

Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 23

فَأَسۡرِ بِعِبَادِي لَيۡلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Allah akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 24

وَٱتۡرُكِ ٱلۡبَحۡرَ رَهۡوًاۖ إِنَّهُمۡ جُندٞ مُّغۡرَقُونَ

Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 25

كَمۡ تَرَكُواْ مِن جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 26

وَزُرُوعٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ

Na mimea na vyeo vitukufu!



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 27

وَنَعۡمَةٖ كَانُواْ فِيهَا فَٰكِهِينَ

Na neema walizokuwa wakiji-stareheshea!



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 28

كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا قَوۡمًا ءَاخَرِينَ

Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 29

فَمَا بَكَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَا كَانُواْ مُنظَرِينَ

Hazikuwalilia mbingu wala ardhi, wala hawakupewa muhula



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 30

وَلَقَدۡ نَجَّيۡنَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ مِنَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡمُهِينِ

Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha