سوره: YAASIIN 

آيه : 1

يسٓ

Yaasiin



سوره: YAASIIN 

آيه : 2

وَٱلۡقُرۡءَانِ ٱلۡحَكِيمِ

Nina apa kwa Qur’ani yenye hekima (nyingi)



سوره: YAASIIN 

آيه : 3

إِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

(Kwamba) Hakika kabisa, wewe ni miongoni mwa Mitume



سوره: YAASIIN 

آيه : 4

عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

(Uko) Juu ya njia iliyo nyooka



سوره: YAASIIN 

آيه : 5

تَنزِيلَ ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

(Ni) Uteremsho wa (Allah) Mwenye nguvu kubwa, Mwenye kurehemu sana



سوره: YAASIIN 

آيه : 6

لِتُنذِرَ قَوۡمٗا مَّآ أُنذِرَ ءَابَآؤُهُمۡ فَهُمۡ غَٰفِلُونَ

(Wewe ni Mtume uliyetumwa) Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, na kwa hiyo basi wao wamekuwa wenye kughafilika



سوره: YAASIIN 

آيه : 7

لَقَدۡ حَقَّ ٱلۡقَوۡلُ عَلَىٰٓ أَكۡثَرِهِمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Bila ya shaka yoyote, kauli imekwisha thibiti juu ya wengi wao sana, kwa hivyo hawaamini



سوره: YAASIIN 

آيه : 8

إِنَّا جَعَلۡنَا فِيٓ أَعۡنَٰقِهِمۡ أَغۡلَٰلٗا فَهِيَ إِلَى ٱلۡأَذۡقَانِ فَهُم مُّقۡمَحُونَ

Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu



سوره: YAASIIN 

آيه : 9

وَجَعَلۡنَا مِنۢ بَيۡنِ أَيۡدِيهِمۡ سَدّٗا وَمِنۡ خَلۡفِهِمۡ سَدّٗا فَأَغۡشَيۡنَٰهُمۡ فَهُمۡ لَا يُبۡصِرُونَ

Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni



سوره: YAASIIN 

آيه : 10

وَسَوَآءٌ عَلَيۡهِمۡ ءَأَنذَرۡتَهُمۡ أَمۡ لَمۡ تُنذِرۡهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini



سوره: YAASIIN 

آيه : 11

إِنَّمَا تُنذِرُ مَنِ ٱتَّبَعَ ٱلذِّكۡرَ وَخَشِيَ ٱلرَّحۡمَٰنَ بِٱلۡغَيۡبِۖ فَبَشِّرۡهُ بِمَغۡفِرَةٖ وَأَجۡرٖ كَرِيمٍ

Hakika wewe unamuonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema



سوره: YAASIIN 

آيه : 12

إِنَّا نَحۡنُ نُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰ وَنَكۡتُبُ مَا قَدَّمُواْ وَءَاثَٰرَهُمۡۚ وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ فِيٓ إِمَامٖ مُّبِينٖ

Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha



سوره: YAASIIN 

آيه : 13

وَٱضۡرِبۡ لَهُم مَّثَلًا أَصۡحَٰبَ ٱلۡقَرۡيَةِ إِذۡ جَآءَهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia waliotumwa



سوره: YAASIIN 

آيه : 14

إِذۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَيۡهِمُ ٱثۡنَيۡنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزۡنَا بِثَالِثٖ فَقَالُوٓاْ إِنَّآ إِلَيۡكُم مُّرۡسَلُونَ

Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazi-dishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu



سوره: YAASIIN 

آيه : 15

قَالُواْ مَآ أَنتُمۡ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَمَآ أَنزَلَ ٱلرَّحۡمَٰنُ مِن شَيۡءٍ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا تَكۡذِبُونَ

Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu!



سوره: YAASIIN 

آيه : 16

قَالُواْ رَبُّنَا يَعۡلَمُ إِنَّآ إِلَيۡكُمۡ لَمُرۡسَلُونَ

Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu



سوره: YAASIIN 

آيه : 17

وَمَا عَلَيۡنَآ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi



سوره: YAASIIN 

آيه : 18

قَالُوٓاْ إِنَّا تَطَيَّرۡنَا بِكُمۡۖ لَئِن لَّمۡ تَنتَهُواْ لَنَرۡجُمَنَّكُمۡ وَلَيَمَسَّنَّكُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٞ

Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu



سوره: YAASIIN 

آيه : 19

قَالُواْ طَـٰٓئِرُكُم مَّعَكُمۡ أَئِن ذُكِّرۡتُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٞ مُّسۡرِفُونَ

Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka



سوره: YAASIIN 

آيه : 20

وَجَآءَ مِنۡ أَقۡصَا ٱلۡمَدِينَةِ رَجُلٞ يَسۡعَىٰ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱتَّبِعُواْ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa



سوره: YAASIIN 

آيه : 21

ٱتَّبِعُواْ مَن لَّا يَسۡـَٔلُكُمۡ أَجۡرٗا وَهُم مُّهۡتَدُونَ

Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali yakuwa wenyewe wameongoka



سوره: YAASIIN 

آيه : 22

وَمَالِيَ لَآ أَعۡبُدُ ٱلَّذِي فَطَرَنِي وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Na kwanini nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?



سوره: YAASIIN 

آيه : 23

ءَأَتَّخِذُ مِن دُونِهِۦٓ ءَالِهَةً إِن يُرِدۡنِ ٱلرَّحۡمَٰنُ بِضُرّٖ لَّا تُغۡنِ عَنِّي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا يُنقِذُونِ

Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa



سوره: YAASIIN 

آيه : 24

إِنِّيٓ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri



سوره: YAASIIN 

آيه : 25

إِنِّيٓ ءَامَنتُ بِرَبِّكُمۡ فَٱسۡمَعُونِ

Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!



سوره: YAASIIN 

آيه : 26

قِيلَ ٱدۡخُلِ ٱلۡجَنَّةَۖ قَالَ يَٰلَيۡتَ قَوۡمِي يَعۡلَمُونَ

Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua



سوره: YAASIIN 

آيه : 27

بِمَا غَفَرَ لِي رَبِّي وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُكۡرَمِينَ

Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio heshimiwa



سوره: YAASIIN 

آيه : 28

۞وَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَىٰ قَوۡمِهِۦ مِنۢ بَعۡدِهِۦ مِن جُندٖ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَمَا كُنَّا مُنزِلِينَ

Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha



سوره: YAASIIN 

آيه : 29

إِن كَانَتۡ إِلَّا صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَإِذَا هُمۡ خَٰمِدُونَ

Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!



سوره: YAASIIN 

آيه : 30

يَٰحَسۡرَةً عَلَى ٱلۡعِبَادِۚ مَا يَأۡتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli