سوره: TWAHA 

آيه : 1

طه

Twaahaa!



سوره: TWAHA 

آيه : 2

مَآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡقُرۡءَانَ لِتَشۡقَىٰٓ

Hatukukuteremshia Qur’an ili upate mashaka



سوره: TWAHA 

آيه : 3

إِلَّا تَذۡكِرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰ

Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea



سوره: TWAHA 

آيه : 4

تَنزِيلٗا مِّمَّنۡ خَلَقَ ٱلۡأَرۡضَ وَٱلسَّمَٰوَٰتِ ٱلۡعُلَى

(Hii Qur’ani ni) uteremsho kutoka kwa Allah Ambaye Ameum-ba ardhi na mbingu zilizo juu



سوره: TWAHA 

آيه : 5

ٱلرَّحۡمَٰنُ عَلَى ٱلۡعَرۡشِ ٱسۡتَوَىٰ

Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliyestawi juu ya Kiti cha Enzi



سوره: TWAHA 

آيه : 6

لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَمَا تَحۡتَ ٱلثَّرَىٰ

Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi



سوره: TWAHA 

آيه : 7

وَإِن تَجۡهَرۡ بِٱلۡقَوۡلِ فَإِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلسِّرَّ وَأَخۡفَى

Na ukinyanyua sauti kwa kusema... basi hakika Yeye anajua siri na kilichofichikana zaidi kuliko siri



سوره: TWAHA 

آيه : 8

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ لَهُ ٱلۡأَسۡمَآءُ ٱلۡحُسۡنَىٰ

Allah! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa



سوره: TWAHA 

آيه : 9

وَهَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Na je! Imekufikia habari ya Mussa?



سوره: TWAHA 

آيه : 10

إِذۡ رَءَا نَارٗا فَقَالَ لِأَهۡلِهِ ٱمۡكُثُوٓاْ إِنِّيٓ ءَانَسۡتُ نَارٗا لَّعَلِّيٓ ءَاتِيكُم مِّنۡهَا بِقَبَسٍ أَوۡ أَجِدُ عَلَى ٱلنَّارِ هُدٗى

Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka (katika) huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto



سوره: TWAHA 

آيه : 11

فَلَمَّآ أَتَىٰهَا نُودِيَ يَٰمُوسَىٰٓ

Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Mussa!



سوره: TWAHA 

آيه : 12

إِنِّيٓ أَنَا۠ رَبُّكَ فَٱخۡلَعۡ نَعۡلَيۡكَ إِنَّكَ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوٗى

Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la Tuwa



سوره: TWAHA 

آيه : 13

وَأَنَا ٱخۡتَرۡتُكَ فَٱسۡتَمِعۡ لِمَا يُوحَىٰٓ

Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa



سوره: TWAHA 

آيه : 14

إِنَّنِيٓ أَنَا ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱعۡبُدۡنِي وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ لِذِكۡرِيٓ

Hakika Mimi ndiye Allah. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi



سوره: TWAHA 

آيه : 15

إِنَّ ٱلسَّاعَةَ ءَاتِيَةٌ أَكَادُ أُخۡفِيهَا لِتُجۡزَىٰ كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا تَسۡعَىٰ

Hakika Saa (Kiyama) kitakuja bila ya shaka. Nimekaribia kukificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyo yafanya



سوره: TWAHA 

آيه : 16

فَلَا يَصُدَّنَّكَ عَنۡهَا مَن لَّا يُؤۡمِنُ بِهَا وَٱتَّبَعَ هَوَىٰهُ فَتَرۡدَىٰ

Kwa hivyo asikukengeushe nacho (Kiyama) yule ambaye hakiamini na akafuata matamanio yake ukaja kuangamia



سوره: TWAHA 

آيه : 17

وَمَا تِلۡكَ بِيَمِينِكَ يَٰمُوسَىٰ

Na nini hicho kilichomo katika mkono wako wa kulia, ewe Mussa?



سوره: TWAHA 

آيه : 18

قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّؤُاْ عَلَيۡهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَـَٔارِبُ أُخۡرَىٰ

Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine



سوره: TWAHA 

آيه : 19

قَالَ أَلۡقِهَا يَٰمُوسَىٰ

(Allah) Akasema: Basi iangushe ewe Mussa



سوره: TWAHA 

آيه : 20

فَأَلۡقَىٰهَا فَإِذَا هِيَ حَيَّةٞ تَسۡعَىٰ

Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio



سوره: TWAHA 

آيه : 21

قَالَ خُذۡهَا وَلَا تَخَفۡۖ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا ٱلۡأُولَىٰ

Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza



سوره: TWAHA 

آيه : 22

وَٱضۡمُمۡ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٍ ءَايَةً أُخۡرَىٰ

Na ukumbatie mkono wako kwenye ubavu wako. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine



سوره: TWAHA 

آيه : 23

لِنُرِيَكَ مِنۡ ءَايَٰتِنَا ٱلۡكُبۡرَى

Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa



سوره: TWAHA 

آيه : 24

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka



سوره: TWAHA 

آيه : 25

قَالَ رَبِّ ٱشۡرَحۡ لِي صَدۡرِي

(Mussa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,



سوره: TWAHA 

آيه : 26

وَيَسِّرۡ لِيٓ أَمۡرِي

Na uifanye kazi yangu (kuwa) nyepesi,



سوره: TWAHA 

آيه : 27

وَٱحۡلُلۡ عُقۡدَةٗ مِّن لِّسَانِي

Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,



سوره: TWAHA 

آيه : 28

يَفۡقَهُواْ قَوۡلِي

Wapate kufahamu maneno yangu



سوره: TWAHA 

آيه : 29

وَٱجۡعَل لِّي وَزِيرٗا مِّنۡ أَهۡلِي

Na nipe waziri katika watu wangu,



سوره: TWAHA 

آيه : 30

هَٰرُونَ أَخِي

Harun, ndugu yangu