سوره: YUNUS 

آيه : 1

الٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡحَكِيمِ

Alif laam raa. Hizo ni Aya za kitabu chenye hekima nyingi



سوره: YUNUS 

آيه : 2

أَكَانَ لِلنَّاسِ عَجَبًا أَنۡ أَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ رَجُلٖ مِّنۡهُمۡ أَنۡ أَنذِرِ ٱلنَّاسَ وَبَشِّرِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَنَّ لَهُمۡ قَدَمَ صِدۡقٍ عِندَ رَبِّهِمۡۗ قَالَ ٱلۡكَٰفِرُونَ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٞ مُّبِينٌ

Hivi, imekuwa ajabu kwa watu kwamba tumemshushia Wahyi (ufunuo) mtu miongoni mwao (na kumpa ujumbe kwamba): Waonye watu na wape bishara wale walioamini kwamba watakua na cheo cha juu kwa Mola wao? Makafiri walisema: “Hakika kabisa, huyu (Muhammad) ni Mchawi aliye dhahiri



سوره: YUNUS 

آيه : 3

إِنَّ رَبَّكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يُدَبِّرُ ٱلۡأَمۡرَۖ مَا مِن شَفِيعٍ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ إِذۡنِهِۦۚ ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُوهُۚ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Hakika, Mola wenu Mlezi ni Allah ambaye ameumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha akalingana sawa juu ya Arshi, anaendesha mambo yote, hakuna muombezi yeyote (atakayekubaliwa uombezi wake) isipokuwa baada ya idhini yake tu. Huyo, kwenu nyie, ndiye Allah, Mola wenu mlezi, basi muabuduni. Hivi hamuonyeki?



سوره: YUNUS 

آيه : 4

إِلَيۡهِ مَرۡجِعُكُمۡ جَمِيعٗاۖ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقًّاۚ إِنَّهُۥ يَبۡدَؤُاْ ٱلۡخَلۡقَ ثُمَّ يُعِيدُهُۥ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ بِٱلۡقِسۡطِۚ وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَهُمۡ شَرَابٞ مِّنۡ حَمِيمٖ وَعَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ

Kwake tu ndio marejeo yenu nyote. Hii ni ahadi ya kweli ya Allah. Hakika yeye (Allah) anaanza kuumba kisha anarudisha (kuumba) ili awalipe kwa uadilifu wale walioamini na wakatenda mema. Na wale waliokufuru watapata kinywaji cha maji ya moto sana na adhabu iumizayo mno kwa sababu ya ukafiri waliokuwa wakiufanya



سوره: YUNUS 

آيه : 5

هُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ ٱلشَّمۡسَ ضِيَآءٗ وَٱلۡقَمَرَ نُورٗا وَقَدَّرَهُۥ مَنَازِلَ لِتَعۡلَمُواْ عَدَدَ ٱلسِّنِينَ وَٱلۡحِسَابَۚ مَا خَلَقَ ٱللَّهُ ذَٰلِكَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۚ يُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

Ni yeye ambaye amelifanya jua lenye kuangaza na mwezi kuwa na nuru na ameuwekea (mwezi) vituo ili (kwa kutumia mwezi) mjue idadi ya miaka na hesabu. Allah hakuviumba hivyo isipokuwa kwa haki tu, anazifafanua Aya (zake) kwa watu wanaojua



سوره: YUNUS 

آيه : 6

إِنَّ فِي ٱخۡتِلَٰفِ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ وَمَا خَلَقَ ٱللَّهُ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يَتَّقُونَ

Hakika, katika kubadilishana kwa usiku na mchana na (katika vitu vingine) alivyoviumba Allah katika mbingu na ardhi kuna ishara (za wazi juu ya uwepo wake na uwezo wake) kwa watu wanao ogopa



سوره: YUNUS 

آيه : 7

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يَرۡجُونَ لِقَآءَنَا وَرَضُواْ بِٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَٱطۡمَأَنُّواْ بِهَا وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِنَا غَٰفِلُونَ

Hakika, wale wasiotaraji kukutana nasi na wameridhika na maisha ya duniani na wamebweteka nayo, na wale ambao Aya zetu wameghafilika nazo,



سوره: YUNUS 

آيه : 8

أُوْلَـٰٓئِكَ مَأۡوَىٰهُمُ ٱلنَّارُ بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Hao makazi yao ni motoni kwa sababu ya yale waliyokuwa wakiyachuma



سوره: YUNUS 

آيه : 9

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ يَهۡدِيهِمۡ رَبُّهُم بِإِيمَٰنِهِمۡۖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهِمُ ٱلۡأَنۡهَٰرُ فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Hakika, wale walioamini na wakatenda matendo mema, Mola wao Mlezi atawaongoza kwa imani yao (kwenda) kwenye pepo za neema mbali mbali ikipita mito mbele yao



سوره: YUNUS 

آيه : 10

دَعۡوَىٰهُمۡ فِيهَا سُبۡحَٰنَكَ ٱللَّهُمَّ وَتَحِيَّتُهُمۡ فِيهَا سَلَٰمٞۚ وَءَاخِرُ دَعۡوَىٰهُمۡ أَنِ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Dua yao humo ni: “Utakatifu ni wako ewe Mola wetu Mlezi, na maamkizi yao humo (watasema): Amani (Assalaamu Alaykum), na mwisho Dua yao (watasema): Alhamdu Lillaahi Rabbil-aalamiin (Sifa zote njema anazistahiki Allah, Mola Mlezi wa walimwengu wote)



سوره: YUNUS 

آيه : 11

۞وَلَوۡ يُعَجِّلُ ٱللَّهُ لِلنَّاسِ ٱلشَّرَّ ٱسۡتِعۡجَالَهُم بِٱلۡخَيۡرِ لَقُضِيَ إِلَيۡهِمۡ أَجَلُهُمۡۖ فَنَذَرُ ٱلَّذِينَ لَا يَرۡجُونَ لِقَآءَنَا فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

Na lau kama Allah angewaha-rakishia watu shari kama wao wanavyoharakisha kheri, bila shaka muda wao (wa kuishi) ungekatishwa (wangekuwa wameangamizwa zamani). Basi tunawaacha wale wasioamini kukutana nasi (Siku ya Kiyama) wakitangatanga katika upotevu wao



سوره: YUNUS 

آيه : 12

وَإِذَا مَسَّ ٱلۡإِنسَٰنَ ٱلضُّرُّ دَعَانَا لِجَنۢبِهِۦٓ أَوۡ قَاعِدًا أَوۡ قَآئِمٗا فَلَمَّا كَشَفۡنَا عَنۡهُ ضُرَّهُۥ مَرَّ كَأَن لَّمۡ يَدۡعُنَآ إِلَىٰ ضُرّٖ مَّسَّهُۥۚ كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلۡمُسۡرِفِينَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Na yanapomgusa (yanapompata) mtu madhara yoyote, anatuomba akiwa amelalia ubavu wake au akiwa amekaa au akiwa amesimama. Basi tunapo muondolea madhara yake hupita kana kwamba hakutuomba kutokana na madhara yaliyomgusa. Hivyo ndivyo wachupao mipaka walivyopambiwa yale waliyokuwa wakiyatenda



سوره: YUNUS 

آيه : 13

وَلَقَدۡ أَهۡلَكۡنَا ٱلۡقُرُونَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَمَّا ظَلَمُواْ وَجَآءَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَمَا كَانُواْ لِيُؤۡمِنُواْۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Na kwa hakika kabisa, tuliangamiza (vizazi vya) karine nyingi kabla yenu pale walipofanya dhuluma, na walijiwa na Mitume wao kwa dalili za wazi na kamwe hawakuamini. Hivi ndivyo tunavyowalipa watu waovu



سوره: YUNUS 

آيه : 14

ثُمَّ جَعَلۡنَٰكُمۡ خَلَـٰٓئِفَ فِي ٱلۡأَرۡضِ مِنۢ بَعۡدِهِمۡ لِنَنظُرَ كَيۡفَ تَعۡمَلُونَ

Kisha tumekufanyeni warithi (mnaopishana; wakiondoka hawa wanakuja wengine) ardhini baada yao, ili tuone jinsi mtakavyofanya



سوره: YUNUS 

آيه : 15

وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَاتُنَا بَيِّنَٰتٖ قَالَ ٱلَّذِينَ لَا يَرۡجُونَ لِقَآءَنَا ٱئۡتِ بِقُرۡءَانٍ غَيۡرِ هَٰذَآ أَوۡ بَدِّلۡهُۚ قُلۡ مَا يَكُونُ لِيٓ أَنۡ أُبَدِّلَهُۥ مِن تِلۡقَآيِٕ نَفۡسِيٓۖ إِنۡ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّۖ إِنِّيٓ أَخَافُ إِنۡ عَصَيۡتُ رَبِّي عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ

Na wakati wanaposomewa Aya zetu zilizo wazi, wale wasiotaraji (wasioamini) kukutana nasi wana-sema: “lete Qur’ani (nyingine) isiyokuwa hii au ibadilishe. Sema: “Haiwezekani kwangu kuibadili kwa utashi wangu. Sifuati isipokuwa tu yanayofunuliwa kwangu. Hakika mimi naogopa adhabu ya Siku iliyo kubwa sana ikiwa nitamuasi Mola wangu Mlezi



سوره: YUNUS 

آيه : 16

قُل لَّوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا تَلَوۡتُهُۥ عَلَيۡكُمۡ وَلَآ أَدۡرَىٰكُم بِهِۦۖ فَقَدۡ لَبِثۡتُ فِيكُمۡ عُمُرٗا مِّن قَبۡلِهِۦٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Sema: Lau kama Allah angetaka nisingekusomeeni (hii Qur’ani), na (Allah) asingekujulisheni (kuwa hiyo Qur’ani ni haki), kwa sababu bila ya shaka yoyote nimekaa nanyi umri mwingi kabla yake (kabla ya kuletewa hii Qur’ani na wala sikukuambieni kuwa mimi nimeleta Qur’ani). Je, hamtumii akili?



سوره: YUNUS 

آيه : 17

فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ كَذَّبَ بِـَٔايَٰتِهِۦٓۚ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Basi ni nani aliye dhalimu (zaidi katika kuzua uongo) kuliko yule amtungiaye uongo Allah au anayekadhibisha Aya zake? Hakika, ilivyo ni kwamba watu waovu hawafaulu



سوره: YUNUS 

آيه : 18

وَيَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَضُرُّهُمۡ وَلَا يَنفَعُهُمۡ وَيَقُولُونَ هَـٰٓؤُلَآءِ شُفَعَـٰٓؤُنَا عِندَ ٱللَّهِۚ قُلۡ أَتُنَبِّـُٔونَ ٱللَّهَ بِمَا لَا يَعۡلَمُ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَلَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ سُبۡحَٰنَهُۥ وَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Na wanaabudu badala ya Allah vitu visivyo wadhuru wala kuwanufaisha na wanasema: “Hawa ni waombezi wetu mbele ya Allah”. Sema: Hivi mnamwambia Allah mambo asiyoyajua mbinguni na ardhini[1]? Utakasifu ni wake (Allah) na ametukuka na yuko mbali na vyote wanavyovishirikisha naye


1- - Allah hapa anamuamuru Mtume wake Muhammad, Allah amshushie rehema na amani, awaambie hawa makafiri washirikishaji kwamba: Allah Mtukufu ndiye mmiliki wa mbingu na ardhi hakifichikani kwake chochote humo. Hivi wanamfundisha na kumueleza vitu visivyokuwepo humo.


سوره: YUNUS 

آيه : 19

وَمَا كَانَ ٱلنَّاسُ إِلَّآ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَٱخۡتَلَفُواْۚ وَلَوۡلَا كَلِمَةٞ سَبَقَتۡ مِن رَّبِّكَ لَقُضِيَ بَيۡنَهُمۡ فِيمَا فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ

Na hawakuwa watu isipokuwa ni Umma mmoja tu, basi wakatofautiana.[1] Na lau kama sio neno lililotangulia[2] kutoka kwa Mola wako Mlezi bila shaka wangekwisha hukumiwa kati yao katika yale wanayo tofautiana humo


1- - Aya hapa inaeleza kuwa binadamu wote walikuwa kitu kimoja wakiwa katika dini moja. Lakini baadae walitofautiana na baadhi yao kupotoka ndio Allah akatuma Mitume ili kuwarudisha katika dini sahihi.


2- - Neno lililokusudiwa hapa ni ule uamuzi wa Allah wa kutowahukumu watu hapa duniani kwa dhambi wanazofanya kama ilivyokuwa kwa mataifa yaliyopita. Amewapa muda hadi Siku ya Kiama. Uamuzi huu umetajwa katika Aya ya 14 ya Sura Ash-shuuraa (42).


سوره: YUNUS 

آيه : 20

وَيَقُولُونَ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ ءَايَةٞ مِّن رَّبِّهِۦۖ فَقُلۡ إِنَّمَا ٱلۡغَيۡبُ لِلَّهِ فَٱنتَظِرُوٓاْ إِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُنتَظِرِينَ

Na wanasema: Si ingekuwa vyema lau kama angeteremshiwa Aya (muujiza) kutoka kwa Mola wake Mlezi? Sema: Mambo ya Ghaibu ni ya Allah tu. Basi subirini, hakika mimi pamoja nanyi ni miongoni mwa wenye kusubiri



سوره: YUNUS 

آيه : 21

وَإِذَآ أَذَقۡنَا ٱلنَّاسَ رَحۡمَةٗ مِّنۢ بَعۡدِ ضَرَّآءَ مَسَّتۡهُمۡ إِذَا لَهُم مَّكۡرٞ فِيٓ ءَايَاتِنَاۚ قُلِ ٱللَّهُ أَسۡرَعُ مَكۡرًاۚ إِنَّ رُسُلَنَا يَكۡتُبُونَ مَا تَمۡكُرُونَ

Na tunapowaonjesha watu rehema yoyote baada ya shida iliyowagusa, ghafla huanza kufanya vitimbi katika Aya zetu. Sema: Allah ni mwepesi zaidi wa (kutengua hila na vitimbi). Hakika, wajumbe wetu (Malaika waandishi) wanaandika vitimbi mnavyovifanya



سوره: YUNUS 

آيه : 22

هُوَ ٱلَّذِي يُسَيِّرُكُمۡ فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۖ حَتَّىٰٓ إِذَا كُنتُمۡ فِي ٱلۡفُلۡكِ وَجَرَيۡنَ بِهِم بِرِيحٖ طَيِّبَةٖ وَفَرِحُواْ بِهَا جَآءَتۡهَا رِيحٌ عَاصِفٞ وَجَآءَهُمُ ٱلۡمَوۡجُ مِن كُلِّ مَكَانٖ وَظَنُّوٓاْ أَنَّهُمۡ أُحِيطَ بِهِمۡ دَعَوُاْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ لَئِنۡ أَنجَيۡتَنَا مِنۡ هَٰذِهِۦ لَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلشَّـٰكِرِينَ

Yeye (Allah) ndiye anaye-kuendesheni bara na baharini, mpaka mnapokuwa kwenye jahazi (mashua) na upepo mzuri ukatembea nao kwa kasi na wakaufurahia, upepo mkali uliijia jahazi hiyo na yakawapiga mawimbi kutoka kila upande, na wakadhani kuwa wamezingirwa, hapo walimuomba Allah wakim-takasia dini (utiifu wakisema kuwa, ewe Mola wetu Mlezi): “Kwa Yakini kabisa, endapo utatuokoa katika haya, bila shaka tutakuwa miongoni mwa wanaoshukuru”



سوره: YUNUS 

آيه : 23

فَلَمَّآ أَنجَىٰهُمۡ إِذَا هُمۡ يَبۡغُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّۗ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّمَا بَغۡيُكُمۡ عَلَىٰٓ أَنفُسِكُمۖ مَّتَٰعَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ ثُمَّ إِلَيۡنَا مَرۡجِعُكُمۡ فَنُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Basi (Allah) alipowaokoa, ghafla wakawa wanafanya uovu katika ardhi bila ya haki. Enyi watu, hakika uasi wenu ni hasara kwenu; ni anasa (fupi) za maisha ya duniani. Kisha kwetu tu ndio marejeo yenu, kwa hiyo tutakuambieni yote mliyokuwa mkiyafanya



سوره: YUNUS 

آيه : 24

إِنَّمَا مَثَلُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا كَمَآءٍ أَنزَلۡنَٰهُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ فَٱخۡتَلَطَ بِهِۦ نَبَاتُ ٱلۡأَرۡضِ مِمَّا يَأۡكُلُ ٱلنَّاسُ وَٱلۡأَنۡعَٰمُ حَتَّىٰٓ إِذَآ أَخَذَتِ ٱلۡأَرۡضُ زُخۡرُفَهَا وَٱزَّيَّنَتۡ وَظَنَّ أَهۡلُهَآ أَنَّهُمۡ قَٰدِرُونَ عَلَيۡهَآ أَتَىٰهَآ أَمۡرُنَا لَيۡلًا أَوۡ نَهَارٗا فَجَعَلۡنَٰهَا حَصِيدٗا كَأَن لَّمۡ تَغۡنَ بِٱلۡأَمۡسِۚ كَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَتَفَكَّرُونَ

Hakika ilivyo ni kwamba, mfano wa maisha ya duniani ni kama maji (mvua) tuliyo yateremsha kutoka mawinguni yakachanganyika na mimea ya ardhini, ikiwa ni pamoja na mimea inayoliwa na watu na mifugo mpaka ardhi ilipokamilisha urembo wake na ikapendeza (kwa kustawi vizuri) na watu wake (wamiliki wake) wakadhani kwamba wameyaweza (mazao hayo kufanikiwa kuyafikisha hatua ya kuvuna), likawajia jambo letu usiku au mchana basi tukaifanya imevunwa (na kufyekwa) kana kwamba haikuwepo jana. Hivi ndivyo tunavyo zifafanua Aya (zetu) kwa watu wanaofikiri



سوره: YUNUS 

آيه : 25

وَٱللَّهُ يَدۡعُوٓاْ إِلَىٰ دَارِ ٱلسَّلَٰمِ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Na Allah anaita (watu) kwenye nyumba ya amani na anamuongoza amtakaye kwenye njia iliyonyooka



سوره: YUNUS 

آيه : 26

۞لِّلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ ٱلۡحُسۡنَىٰ وَزِيَادَةٞۖ وَلَا يَرۡهَقُ وُجُوهَهُمۡ قَتَرٞ وَلَا ذِلَّةٌۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Wale waliofanya mazuri (hapa duniani), watapata mazuri (Akhera) na ziada[1] na wala nyuso zao hazitafunikwa na vumbi na madhila. Hao ndio watu wa Peponi; humo watakaa milele


1- - Swahaba wengi, Allah awawie radhi, wametafsiri “mazuri” kwamba ni Pepo na “ziada” kwamba ni kumuona Allah Mtukufu.


سوره: YUNUS 

آيه : 27

وَٱلَّذِينَ كَسَبُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ جَزَآءُ سَيِّئَةِۭ بِمِثۡلِهَا وَتَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ مَّا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِنۡ عَاصِمٖۖ كَأَنَّمَآ أُغۡشِيَتۡ وُجُوهُهُمۡ قِطَعٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مُظۡلِمًاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na wale waliochuma maovu, malipo ya maovu ni uovu kama huo, na yatawafika madhila, hawatakuwa na yeyote wa kuwakinga (dhidi ya) Allah (asiwaadhibu). (Hali yao itakuwa), kana kwamba nyuso zao zimefunikizwa na kipande cha usiku wa giza nene. Hao ndio watu wa motoni, watakaahumo milele



سوره: YUNUS 

آيه : 28

وَيَوۡمَ نَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ مَكَانَكُمۡ أَنتُمۡ وَشُرَكَآؤُكُمۡۚ فَزَيَّلۡنَا بَيۡنَهُمۡۖ وَقَالَ شُرَكَآؤُهُم مَّا كُنتُمۡ إِيَّانَا تَعۡبُدُونَ

Na (kumbuka) siku tutakayo-wakusanya wote, kisha tutawaambia wale washirikina (makafiri kuwa): Simameni hapo hapo mlipo nyinyi na washirika (Miungu) wenu (mliowashirikisha na Allah), hivyo tutatenganisha baina yao. Na washirika wao watasema: Nyinyi hamkuwa mnatuabudu



سوره: YUNUS 

آيه : 29

فَكَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدَۢا بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمۡ إِن كُنَّا عَنۡ عِبَادَتِكُمۡ لَغَٰفِلِينَ

Basi Allah anatosha kuwa shahidi baina yetu na baina yenu. Hakika sisi tulikuwa hatujui chochote kuhusu ibada yenu



سوره: YUNUS 

آيه : 30

هُنَالِكَ تَبۡلُواْ كُلُّ نَفۡسٖ مَّآ أَسۡلَفَتۡۚ وَرُدُّوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ مَوۡلَىٰهُمُ ٱلۡحَقِّۖ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Huko, kila mtu atayatafuta matendo yake aliyoyatanguliza (kuyafanya; yawe ya kheri au ya shari), na watarudishwa kwa (Allah) Mola wao wa haki, na yatawapotea yale waliyokuwa wakiyazusha