سوره: AL-FAATIHA 

آيه : 1

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Allah Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu



سوره: AL-FAATIHA 

آيه : 2

ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Kila sifa njema ni ya Allah, Mola wa walimwengu wote



سوره: AL-FAATIHA 

آيه : 3

ٱلرَّحۡمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Mwingi wa Rehema, Mwenye-Kurehemu



سوره: AL-FAATIHA 

آيه : 4

مَٰلِكِ يَوۡمِ ٱلدِّينِ

Mmiliki wa Siku ya Malipo



سوره: AL-FAATIHA 

آيه : 5

إِيَّاكَ نَعۡبُدُ وَإِيَّاكَ نَسۡتَعِينُ

Wewe tu ndiye tunae kuabudu na wewe tu ndie tunae kuomba msaada



سوره: AL-FAATIHA 

آيه : 6

ٱهۡدِنَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ

Tuongoze kwenye njia ilio nyooka



سوره: AL-FAATIHA 

آيه : 7

صِرَٰطَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِمۡ غَيۡرِ ٱلۡمَغۡضُوبِ عَلَيۡهِمۡ وَلَا ٱلضَّآلِّينَ

Njia ya ambao umewaneemesha, na sio yawalio kasirikiwa na sio ya waliopotea[1]


1- - Walioneemeshwa wametajwa katika Sura AnNisaa (4), Aya ya 69. Hapa Aya inaashiria utukufu wa Swahaba wa kiongozwana Abubakar, Umar, Uthman na Ali (Allah awawieradhi) kwasababu wao ni miongoni mwa walioneemeshwa na ambao tunatakiwa kufuata njia yao. Waliokasirikiwa wametajwa kuanzia Aya ya 75 mpaka Aya ya 90 ya Sura Albaqara, na waliopotea wametajwa katika Aya ya 77 ya Sura Almaida (5).