سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 121

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 122

إِنَّهُمَا مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 123

وَإِنَّ إِلۡيَاسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 124

إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia watu wake: Hamuogopi?



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 125

أَتَدۡعُونَ بَعۡلٗا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ

Mnamwomba Baali na mnamwacha Mbora wa waumbaji,



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 126

ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Allah, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 127

فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 128

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa waja wa Allah walio safishwa



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 129

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 130

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ

Iwe salama kwa Ilyas



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 131

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 132

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 133

وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Lutwi bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 134

إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tulipo mwokoa yeye na watu wake wote,



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 135

إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 136

ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengineo



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 137

وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ

Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 138

وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 139

وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 140

إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ

Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 141

فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 142

فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 143

فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ

Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Allah,



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 144

لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 145

۞فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٞ

Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 146

وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ

Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung’unye



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 147

وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ

Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 148

فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ

Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 149

فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?



سوره: ASSWAAFFAAT 

آيه : 150

أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ إِنَٰثٗا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ

Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?