سوره: AL-IMRAN 

آيه : 61

فَمَنۡ حَآجَّكَ فِيهِ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ فَقُلۡ تَعَالَوۡاْ نَدۡعُ أَبۡنَآءَنَا وَأَبۡنَآءَكُمۡ وَنِسَآءَنَا وَنِسَآءَكُمۡ وَأَنفُسَنَا وَأَنفُسَكُمۡ ثُمَّ نَبۡتَهِلۡ فَنَجۡعَل لَّعۡنَتَ ٱللَّهِ عَلَى ٱلۡكَٰذِبِينَ

Na yeyote atakayekuhoji katika hili baada ya kukufikia elimu, basi sema: Njooni, tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wake zetu na wake zenu, na sisi na nyinyi, kisha tuombe kwa unyenyekevu ili laana ya Allah iwashukie waliokadhibisha



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 62

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡقَصَصُ ٱلۡحَقُّۚ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّا ٱللَّهُۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Hakika, hivi ndivyo visa vya kweli, na hakuna wakuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah tu, na hakika Allah ni Mwenye nguvu sana, Mwenye hekima nyingi



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 63

فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُفۡسِدِينَ

Na endapo watapuuza basi Allah anawajua mno waharibifu



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 64

قُلۡ يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ كَلِمَةٖ سَوَآءِۭ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمۡ أَلَّا نَعۡبُدَ إِلَّا ٱللَّهَ وَلَا نُشۡرِكَ بِهِۦ شَيۡـٔٗا وَلَا يَتَّخِذَ بَعۡضُنَا بَعۡضًا أَرۡبَابٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَقُولُواْ ٱشۡهَدُواْ بِأَنَّا مُسۡلِمُونَ

Sema: Enyi Watu wa Kitabu: Njooni kwenye neno la sawa kati yetu na kati yenu ya kuwa, tusimuabudu isipokuwa Allah tu, wala tusimshirikishe na chochote, na tusiwafanye baadhi yetu Miungu badala ya Allah. Na kama watapuuza, basi semeni (muwaambie): Shuhudieni kuwa sisi ni Waislamu



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 65

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تُحَآجُّونَ فِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَمَآ أُنزِلَتِ ٱلتَّوۡرَىٰةُ وَٱلۡإِنجِيلُ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِهِۦٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnaleta mijadala kuhusu Ibrahimu na ilhali Taurati na Injili hazikuteremshwa isipokuwa baada yake? Hivi hamtumii akili?



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 66

هَـٰٓأَنتُمۡ هَـٰٓؤُلَآءِ حَٰجَجۡتُمۡ فِيمَا لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞ فَلِمَ تُحَآجُّونَ فِيمَا لَيۡسَ لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

E nyinyi hawa! Mlihoji yale mnayoyajua, basi kwanini mnahoji msiyoyajua? Na Allah anajua na nyinyi hamjui



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 67

مَا كَانَ إِبۡرَٰهِيمُ يَهُودِيّٗا وَلَا نَصۡرَانِيّٗا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفٗا مُّسۡلِمٗا وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Ibrahimu hakuwa Myahudi na wala (hakuwa) Mnaswara, lakini alikuwa Muongofu, Muislamu na hakuwa miongoni mwa Washirikina



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 68

إِنَّ أَوۡلَى ٱلنَّاسِ بِإِبۡرَٰهِيمَ لَلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُ وَهَٰذَا ٱلنَّبِيُّ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۗ وَٱللَّهُ وَلِيُّ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika, watu walio na haki zaidi kwa Ibrahimu ni wale tu waliomfuata yeye na (kumfuata) Mtume huyu na wale walioamini. Na Allah ni Msimamizi wa Waumini



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 69

وَدَّت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَوۡ يُضِلُّونَكُمۡ وَمَا يُضِلُّونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ

Kundi katika Watu wa Kitabu limetamani kukupotezeni, na hawatampoteza (yeyote) isipokuwa wao wenyewe tu na ilhali hawatambui



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 70

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَأَنتُمۡ تَشۡهَدُونَ

Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnazipinga Aya za Allah ilhali mnashuhudia?



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 71

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَلۡبِسُونَ ٱلۡحَقَّ بِٱلۡبَٰطِلِ وَتَكۡتُمُونَ ٱلۡحَقَّ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnachanganya haki na batili na mnaificha haki na ilhali nyinyi mnajua (kuwa mnachofanya sio sahihi)?



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 72

وَقَالَت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ ءَامِنُواْ بِٱلَّذِيٓ أُنزِلَ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَجۡهَ ٱلنَّهَارِ وَٱكۡفُرُوٓاْ ءَاخِرَهُۥ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na kundi katika Watu wa Kitabu lilisema: Aminini mwanzo wa mchana (asubuhi) kile kilichoteremshwa kwa wale walioamini na kikataeni mwisho wake (jioni), huenda watarudi (nyuma)



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 73

وَلَا تُؤۡمِنُوٓاْ إِلَّا لِمَن تَبِعَ دِينَكُمۡ قُلۡ إِنَّ ٱلۡهُدَىٰ هُدَى ٱللَّهِ أَن يُؤۡتَىٰٓ أَحَدٞ مِّثۡلَ مَآ أُوتِيتُمۡ أَوۡ يُحَآجُّوكُمۡ عِندَ رَبِّكُمۡۗ قُلۡ إِنَّ ٱلۡفَضۡلَ بِيَدِ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ

Na msimuamini (yeyote) isipokuwa tu yule aliyefuata dini yenu Sema: Muongozo (sahihi) ni muongozo wa Allah tu, kwamba kuna yeyote atakayepewa mfano wa mlichopewa au atakuhojini kwacho mbele ya Mola wenu. Sema: Hakika, fadhila zote ziko mkononi mwa Allah, na Allah ni Mkunjufu, Mjuzi mno



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 74

يَخۡتَصُّ بِرَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Anamhusisha kwa (kumpa) rehema zake amtakaye, na Allah ni Mwenye fadhila kubwa



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 75

۞وَمِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ مَنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِقِنطَارٖ يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ وَمِنۡهُم مَّنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِدِينَارٖ لَّا يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ إِلَّا مَا دُمۡتَ عَلَيۡهِ قَآئِمٗاۗ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُواْ لَيۡسَ عَلَيۡنَا فِي ٱلۡأُمِّيِّـۧنَ سَبِيلٞ وَيَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Na miongini mwa Watu wa Kitabu wapo ambao endapo utamuamini (ukaweka kwake amana ya) mali nyingi, atakutekelezea (kwa kukurejeshea). Na miongoni mwao wapo ambao ukimuamini kwa dinari moja tu, haitekelezi (hairejeshi) isipokuwa tu kwa kumsimamia (kumdai na kumfuatilia). Hilo ni kwa sababu walisema: Hakuna lawama kwetu kwa (tunachowafanyia) Umiyina (wasiojuwa kuandika wala kusoma kilichoandikwa)[1] na wanamzulia Allah uongo ilhali wanajua


1- - Wanaokusudiwa hapa ni Waislamu Waarabu ambao kwa wakati huo hawakuwa wanajua kuandika wala
kusoma kilichoandikwa. Ni aina fulani ya dharau, ubaguzi, kejeli na udhalilishaji wa Wayahudi dhidi ya
jamii ya Waislamu; sifa ambazo Wayahudi na washirika wao wanaziendeleza hadi leo.


سوره: AL-IMRAN 

آيه : 76

بَلَىٰۚ مَنۡ أَوۡفَىٰ بِعَهۡدِهِۦ وَٱتَّقَىٰ فَإِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُتَّقِينَ

Ni hakika; ambaye ametekeleza kikamilifu ahadi yake na akamcha Allah, kwa hakika Allah anawapenda wacha Mungu



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 77

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَشۡتَرُونَ بِعَهۡدِ ٱللَّهِ وَأَيۡمَٰنِهِمۡ ثَمَنٗا قَلِيلًا أُوْلَـٰٓئِكَ لَا خَلَٰقَ لَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ ٱللَّهُ وَلَا يَنظُرُ إِلَيۡهِمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Hakika, wale wanaouza ahadi ya Allah na viapo vyao kwa thamani ndogo, hao hawatakuwa na fungu (la kheri yoyote) Akhera, na Allah hatazungumza nao (mazungumzo ya huruma) na hatawaangalia (kwa huruma) Siku ya Kiama na hatowatakasa (kwa kusamehe dhambi zao) na watapata adhabu kali mno



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 78

وَإِنَّ مِنۡهُمۡ لَفَرِيقٗا يَلۡوُۥنَ أَلۡسِنَتَهُم بِٱلۡكِتَٰبِ لِتَحۡسَبُوهُ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَمَا هُوَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَيَقُولُونَ هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ وَمَا هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ وَيَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Na kwa hakika kabisa, miongoni mwao lipo kundi linalopindisha ndimi zao kwenye kitabu (cha Taurati) ili mdhani hayo (wayapindishayo) yanatoka kitabuni, na (ukweli) si sehemu ya kitabu. Na wanasema: Hayo yanatoka kwa Allah na kamwe hayatoki kwa Allah, na wanamzulia Allah uongo huku wakijua



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 79

مَا كَانَ لِبَشَرٍ أَن يُؤۡتِيَهُ ٱللَّهُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحُكۡمَ وَٱلنُّبُوَّةَ ثُمَّ يَقُولَ لِلنَّاسِ كُونُواْ عِبَادٗا لِّي مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلَٰكِن كُونُواْ رَبَّـٰنِيِّـۧنَ بِمَا كُنتُمۡ تُعَلِّمُونَ ٱلۡكِتَٰبَ وَبِمَا كُنتُمۡ تَدۡرُسُونَ

Haiwi kwa mwanadamu yeyote ambaye Allah amempa kitabu na hukumu (elimu na mamlaka) na Utumekisha awaambie watu: “Niabuduni mimi badala ya Allah”, na lakini (anatakiwa kuwaambia): “Kuweni watiifu kwa Mola mlezi, kutokana na yale mliyokuwa mnayafundisha (yatokanayo na) kitabu na kutokana na yale mliyokuwa mkiyasoma



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 80

وَلَا يَأۡمُرَكُمۡ أَن تَتَّخِذُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ أَرۡبَابًاۚ أَيَأۡمُرُكُم بِٱلۡكُفۡرِ بَعۡدَ إِذۡ أَنتُم مُّسۡلِمُونَ

Na (pia haiwi kwa yeyote ambaye Allah amempa Kitabu, elimu, mamlaka na Utume) akuamrisheni muwafanye Malaika na Manabii kuwa Miungu. Hivi (inawezekana) akuamrisheni ukafiri baada ya kuwa nyinyi ni Waislamu?



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 81

وَإِذۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ لَمَآ ءَاتَيۡتُكُم مِّن كِتَٰبٖ وَحِكۡمَةٖ ثُمَّ جَآءَكُمۡ رَسُولٞ مُّصَدِّقٞ لِّمَا مَعَكُمۡ لَتُؤۡمِنُنَّ بِهِۦ وَلَتَنصُرُنَّهُۥۚ قَالَ ءَأَقۡرَرۡتُمۡ وَأَخَذۡتُمۡ عَلَىٰ ذَٰلِكُمۡ إِصۡرِيۖ قَالُوٓاْ أَقۡرَرۡنَاۚ قَالَ فَٱشۡهَدُواْ وَأَنَا۠ مَعَكُم مِّنَ ٱلشَّـٰهِدِينَ

Na (kumbuka) Allah alipochukua ahadi ya Manabii ya kuwa kitabu chochote na hekima yoyote niliyokupeni kisha akakujieni Mtume anayesadikisha kile mlichonacho kwamba kwa yakini kabisa mtamkubali na kumnusuru. (Allah) Akasema: Je, mmekubalina mmechukua ahadi yangu juu ya hilo? Wakasema: Tumeikubali. (Allah) Akasema: Shuhudieni kwamba, na mimi pamoja nanyi ni miongoni mwa wenye kushuhudia



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 82

فَمَن تَوَلَّىٰ بَعۡدَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ

Basi watakaokengeuka baada ya (makubaliano) hayo basi hao ni waovu tu



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 83

أَفَغَيۡرَ دِينِ ٱللَّهِ يَبۡغُونَ وَلَهُۥٓ أَسۡلَمَ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ طَوۡعٗا وَكَرۡهٗا وَإِلَيۡهِ يُرۡجَعُونَ

Hivi wanataka dini isiyokuwa ya Allah, na ilhali vinamtii yeye vyote vilivyomo mbinguni na ardhini kwa hiari na lazima? Na kwake yeye tu watarejeshwa



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 84

قُلۡ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ عَلَيۡنَا وَمَآ أُنزِلَ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَٱلۡأَسۡبَاطِ وَمَآ أُوتِيَ مُوسَىٰ وَعِيسَىٰ وَٱلنَّبِيُّونَ مِن رَّبِّهِمۡ لَا نُفَرِّقُ بَيۡنَ أَحَدٖ مِّنۡهُمۡ وَنَحۡنُ لَهُۥ مُسۡلِمُونَ

Sema: Tumemuamini Allah na kile tulichoteremshiwa na alichoteremshiwa Ibrahimu na Ismaili na Is-haka na Yakubu na Asbaati (watoto wa Yakubu) na alichopewa Musa na Isa na Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao. Hatumbagui yeyote kati yao. Nasisi tumejisalimisha kwake tu



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 85

وَمَن يَبۡتَغِ غَيۡرَ ٱلۡإِسۡلَٰمِ دِينٗا فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡهُ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

Na yeyote atakayetaka dini isiyokuwa Uislamu, hatakubaliwa na Akhera atakuwa miongoni mwa wenye hasara



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 86

كَيۡفَ يَهۡدِي ٱللَّهُ قَوۡمٗا كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ وَشَهِدُوٓاْ أَنَّ ٱلرَّسُولَ حَقّٞ وَجَآءَهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُۚ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Vipi Allah atawaongoa watu waliokufuru baada ya kuamini, na wameshuhudia pasipo shaka kwamba Mtume (Muhammad) ni hakina wamejiwa na ubainifu mbalimbali? Na Allah hawaongoi watu madhalimu



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 87

أُوْلَـٰٓئِكَ جَزَآؤُهُمۡ أَنَّ عَلَيۡهِمۡ لَعۡنَةَ ٱللَّهِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ

Hao malipo yao ni kwamba, watashukiwa na laana ya Allah na ya Malaika na ya watu wote



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 88

خَٰلِدِينَ فِيهَا لَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابُ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ

Watabaki milele humo (kwenye laana); hawatapunguziwa adhabu na hawatangojwa (hawatapewa muda wa kujitetea au kuomba msamaha)



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 89

إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ وَأَصۡلَحُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ

Isipokuwa (watakaoepuka laana ni) wale waliotubu baada ya hapo na wakafanya mema. Basi kwa hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno



سوره: AL-IMRAN 

آيه : 90

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ ثُمَّ ٱزۡدَادُواْ كُفۡرٗا لَّن تُقۡبَلَ تَوۡبَتُهُمۡ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلضَّآلُّونَ

Hakika, wale waliokufuru baada ya kuamini kisha wakazidisha ukafiri, toba zao hazitakubaliwa, na hao ndio hasa wapotevu