سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 31

وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَـٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ

Na Hatukuweka walinzi wa moto isipokuwa ni Malaika, na Hatukufanya idadi yao isipokuwa iwe ni mtihani kwa wale waliokufuru; ili wawe na yakini wale waliopewa Kitabu, na iwazidishie Imani wale walioamini; na wala wasitie shaka wale waliopewa Kitabu na Waumini; na ili wale waliokuwa na maradhi nyoyoni mwao (ya unafiki), na makafiri waseme: Allah Amekusudia nini kwa mfano huu? Hivyo ndivyo Allah Anavyompoteza Amtakaye na Anamuongoa Amtakaye. Na hakuna ajuaye majeshi ya Mola wako isipokuwa Yeye Peke yake, na haya hayakuwa isipokuwa ni ukumbusho tu kwa binadamu



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 32

كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ

Sivyo hivyo! Naapa kwa mwezi



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 33

وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ

Na Naapa kwa usiku unapoondoka



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 34

وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ

Na Naapa kwa asubuhi inapoangaza (inapo pambazuka)



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 35

إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ

Hakika huo (Moto) bila shaka ni mojawapo ya majanga makubwa kabisa



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 36

نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ

Ni onyo kwa binadamu



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 37

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ

Kwa atakaye miongoni mwenu atatangulia mbele au atachelewa nyuma



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 38

كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ

Kila nafsi iko katika rehani kwa yale iliyoyachuma.[1]


1- - Kila nafsi itashikwa kwa iliyo yatenda.


سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 39

إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ

Isipokuwa watu wa kuliani



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 40

فِي جَنَّـٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ

Hao watakuwa katika Mabustani ya Peponi, wanaulizana



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 41

عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Kuhusu wakosefu



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 42

مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ

(Watawauliza): Nini kilicho kuingizeni katika Moto?



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 43

قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ

Watasema: Hatukuwa miongoni mwa wanaosali



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 44

وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ

Na wala hatukuwa tunalisha masikini



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 45

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ

Na tulikuwa tukipiga porojo pamoja na wanaopiga porojo



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 46

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na tulikuwa tunaikadhibisha Siku ya malipo



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 47

حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ

Mpaka ikatufikia yakini (mauti)



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 48

فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّـٰفِعِينَ

Basi haitowafaa uombezi wowote wa waombezi



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 49

فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ

Basi wana nini hata wanapuuza ukumbusho huu!



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 50

كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ

Kama kwamba ni punda milia wenye kutimuliwa, (wenye kushtuka)



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 51

فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ

Wamekimbia mbio kutokana na kumkimbia simba



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 52

بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ

Bali anataka kila mtu miongoni mwao apewe nyaraka zilizofunuliwa



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 53

كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Si hivyo! hasha! Bali hawaiogopi Akhera



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 54

كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ

Na sihivyo! Hakika hii (Qur’ani) ni mawaidha



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 55

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anayetaka atawaidhika



سوره: ALMUDDATH-THIR 

آيه : 56

وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ

Na hawatowaidhika isipokuwa Akitaka Allah; Yeye Ndiye mwenye kustahiki kuogopwa, na mwenye kustahiki kusamehe (madhambi)