سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 31

مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيٗا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 32

وَلَقَدِ ٱخۡتَرۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ عِلۡمٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 33

وَءَاتَيۡنَٰهُم مِّنَ ٱلۡأٓيَٰتِ مَا فِيهِ بَلَـٰٓؤٞاْ مُّبِينٌ

Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 34

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ

Hakika hawa wanasema:



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 35

إِنۡ هِيَ إِلَّا مَوۡتَتُنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُنشَرِينَ

Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 36

فَأۡتُواْ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 37

أَهُمۡ خَيۡرٌ أَمۡ قَوۡمُ تُبَّعٖ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ أَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ

Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa’ na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 38

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا لَٰعِبِينَ

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 39

مَا خَلَقۡنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 40

إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ مِيقَٰتُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 41

يَوۡمَ لَا يُغۡنِي مَوۡلًى عَن مَّوۡلٗى شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 42

إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Isipo kuwa atakaye mrehemu Allah. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 43

إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ

Hakika Mti wa Zaqqum



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 44

طَعَامُ ٱلۡأَثِيمِ

Ni chakula cha mwenye dhambi



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 45

كَٱلۡمُهۡلِ يَغۡلِي فِي ٱلۡبُطُونِ

Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 46

كَغَلۡيِ ٱلۡحَمِيمِ

Kama kutokota kwa maji ya moto



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 47

خُذُوهُ فَٱعۡتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 48

ثُمَّ صُبُّواْ فَوۡقَ رَأۡسِهِۦ مِنۡ عَذَابِ ٱلۡحَمِيمِ

Kisha mwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 49

ذُقۡ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡكَرِيمُ

Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 50

إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمۡتَرُونَ

Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 51

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 52

فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani na chemchem



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 53

يَلۡبَسُونَ مِن سُندُسٖ وَإِسۡتَبۡرَقٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 54

كَذَٰلِكَ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurulaini



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 55

يَدۡعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ

Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 56

لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰۖ وَوَقَىٰهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Allah) atawalinda na adhabu ya Jahannamu



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 57

فَضۡلٗا مِّن رَّبِّكَۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 58

فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Basi tumeifanya nyepesi hii Qur’ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka



سوره: ADDUKHAAN 

آيه : 59

فَٱرۡتَقِبۡ إِنَّهُم مُّرۡتَقِبُونَ

Ngoja tu, na wao wangoje pia