Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 4

قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ

Wameangamizwa watu wa mahandaki



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 5

ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ

Yenye moto wenye kuni nyingi,



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 6

إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ

Walipo kuwa wamekaa hapo,



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 7

وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 8

وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Allah, Mwenye nguvu, Msifiwa,



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 9

ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Allah ni shaahidi wa kila kitu



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 11

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 12

إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 13

إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejesha tena,



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 14

وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 15

ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ

Mwenye Kiti cha Enzi,



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 16

فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ

Atendaye ayatakayo



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 17

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ

Je! Zimekufikia khabari za majeshi?



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 18

فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ

Ya Firauni na Thamudi?



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 19

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 20

وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ

Na Allah nyuma yao amewazunguka



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 21

بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ

Bali hii ni Qur’ani tukufu



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 22

فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 1

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ

Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 2

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ

Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinachokuja usiku?



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 3

ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ

Ni Nyota yenye mwanga mkali



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 4

إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ

Hapana nafsi ila inayo mwangalizi



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 5

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ

Hebu na ajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 6

خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 7

يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 8

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ

Hakika Yeye ana uwezo wa kumrudisha



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 9

يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ

Siku zitakapo dhihirishwa siri



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 10

فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 11

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ

Naapa kwa mbingu yenye marejeo!