Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 7

إِنَّ لَكَ فِي ٱلنَّهَارِ سَبۡحٗا طَوِيلٗا

Kwani hakika mchana una shughuli nyingi



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 8

وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلۡ إِلَيۡهِ تَبۡتِيلٗا

Na litaje Jina la Mola wako, na jitolee Kwake kikamilifu



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 9

رَّبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ فَٱتَّخِذۡهُ وَكِيلٗا

Mola wa Mashariki na Magharibi, hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye. Basi mfanye kuwa ni Mdhamini wako (na Mtegemewa wako)



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 10

وَٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَٱهۡجُرۡهُمۡ هَجۡرٗا جَمِيلٗا

Na subiri juu ya yale wayasemayo, na uwaepuke muepuko wa wema



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 11

وَذَرۡنِي وَٱلۡمُكَذِّبِينَ أُوْلِي ٱلنَّعۡمَةِ وَمَهِّلۡهُمۡ قَلِيلًا

Na Niache Mimi na wanaoka-dhibisha, walioneemeka na wape muhula kidogo



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 12

إِنَّ لَدَيۡنَآ أَنكَالٗا وَجَحِيمٗا

Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unaowaka kwa ukali kabisa!



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 13

وَطَعَامٗا ذَا غُصَّةٖ وَعَذَابًا أَلِيمٗا

Na chakula kinachokwama kooni (hakimezeki) na adhabu inayoumiza sana



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 14

يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ وَكَانَتِ ٱلۡجِبَالُ كَثِيبٗا مَّهِيلًا

Siku ambayo ardhi itatikisika na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 15

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَآ إِلَيۡكُمۡ رَسُولٗا شَٰهِدًا عَلَيۡكُمۡ كَمَآ أَرۡسَلۡنَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ رَسُولٗا

Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 16

فَعَصَىٰ فِرۡعَوۡنُ ٱلرَّسُولَ فَأَخَذۡنَٰهُ أَخۡذٗا وَبِيلٗا

Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 17

فَكَيۡفَ تَتَّقُونَ إِن كَفَرۡتُمۡ يَوۡمٗا يَجۡعَلُ ٱلۡوِلۡدَٰنَ شِيبًا

Basi vipi mtaweza kujikinga, kama mkikufuru Siku itakayowafanya watoto kuwa wenye kutoka mvi?



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 18

ٱلسَّمَآءُ مُنفَطِرُۢ بِهِۦۚ كَانَ وَعۡدُهُۥ مَفۡعُولًا

Hapo ndipo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 19

إِنَّ هَٰذِهِۦ تَذۡكِرَةٞۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلًا

Kwa hakika huu ni ukumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kuelekea kwa Mola wake



Surah: ALMUZZAMMIL 

Ayah : 20

۞إِنَّ رَبَّكَ يَعۡلَمُ أَنَّكَ تَقُومُ أَدۡنَىٰ مِن ثُلُثَيِ ٱلَّيۡلِ وَنِصۡفَهُۥ وَثُلُثَهُۥ وَطَآئِفَةٞ مِّنَ ٱلَّذِينَ مَعَكَۚ وَٱللَّهُ يُقَدِّرُ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّهَارَۚ عَلِمَ أَن لَّن تُحۡصُوهُ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡۖ فَٱقۡرَءُواْ مَا تَيَسَّرَ مِنَ ٱلۡقُرۡءَانِۚ عَلِمَ أَن سَيَكُونُ مِنكُم مَّرۡضَىٰ وَءَاخَرُونَ يَضۡرِبُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ يَبۡتَغُونَ مِن فَضۡلِ ٱللَّهِ وَءَاخَرُونَ يُقَٰتِلُونَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۖ فَٱقۡرَءُواْ مَا تَيَسَّرَ مِنۡهُۚ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ وَأَقۡرِضُواْ ٱللَّهَ قَرۡضًا حَسَنٗاۚ وَمَا تُقَدِّمُواْ لِأَنفُسِكُم مِّنۡ خَيۡرٖ تَجِدُوهُ عِندَ ٱللَّهِ هُوَ خَيۡرٗا وَأَعۡظَمَ أَجۡرٗاۚ وَٱسۡتَغۡفِرُواْ ٱللَّهَۖ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمُۢ

Hakika Mola wako anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Allah ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamuwezi kuweka hesabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qurani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila za Allah, na wengine wanapigana katika Njia ya Allah. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na simamisheni Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Allah mkopo ulio mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Allah, nayo imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Allah. Hakika Allah ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 1

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ

Ewe mwenye kujigubika



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 2

قُمۡ فَأَنذِرۡ

Simama uonye



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 3

وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ

Na Mola wako Mlezi mtukuze



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 4

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ

Na nguo zako zisafishe



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 5

وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ

Na (mambo) machafu yahame (yaache)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 6

وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ

Wala usitoe (usifanye hisani) kwa kutaraji kuzidishiwa (kupata kingi Zaidi)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 7

وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ

Na kwa ajili ya Mola wako tu kuwa na subira (kuwa mvumilivu)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 8

فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ

Basi litakapopulizwa baragumu (Tarumbeta)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 9

فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ

Basi siku hiyo itakuwa ni siku ngumu sana



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 10

عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ

Kwa makafiri haitakuwa nyepesi



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 11

ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا

Niache Mimi peke yangu na yule niliye muumba



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 12

وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا

Na nikamjaalia awe na mali nyingi



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 13

وَبَنِينَ شُهُودٗا

Na watoto wanao onekana



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 14

وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا

Na nikamtengenezea mambo vizuri kabisa



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 15

ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ

Kisha anatumai Nimuongezee!



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 16

كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا

Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi (Na umpinzani) Aya zetu!