Surah: AL-KAHF 

Ayah : 70

قَالَ فَإِنِ ٱتَّبَعۡتَنِي فَلَا تَسۡـَٔلۡنِي عَن شَيۡءٍ حَتَّىٰٓ أُحۡدِثَ لَكَ مِنۡهُ ذِكۡرٗا

Akasema: Basi ukinifuata usiniulize kitu mpaka mimi nianze kukutajia



Surah: AL-KAHF 

Ayah : 71

فَٱنطَلَقَا حَتَّىٰٓ إِذَا رَكِبَا فِي ٱلسَّفِينَةِ خَرَقَهَاۖ قَالَ أَخَرَقۡتَهَا لِتُغۡرِقَ أَهۡلَهَا لَقَدۡ جِئۡتَ شَيۡـًٔا إِمۡرٗا

Basi wawili hao wakatoka, hata walipo panda jahazi (yule mtu) akalitoboa. (Mussa) akasema: Unalitoboa uwazamishe watu wake? Hakika umefanya jambo baya



Surah: AL-KAHF 

Ayah : 72

قَالَ أَلَمۡ أَقُلۡ إِنَّكَ لَن تَسۡتَطِيعَ مَعِيَ صَبۡرٗا

Akasema: Sikukwambia hutaweza kuvumilia kuwa pamoja nami?



Surah: AL-KAHF 

Ayah : 73

قَالَ لَا تُؤَاخِذۡنِي بِمَا نَسِيتُ وَلَا تُرۡهِقۡنِي مِنۡ أَمۡرِي عُسۡرٗا

(Mussa) akasema: Usinichukulie kwa niliyo sahau, wala usinipe uzito kwa jambo langu



Surah: AL-KAHF 

Ayah : 74

فَٱنطَلَقَا حَتَّىٰٓ إِذَا لَقِيَا غُلَٰمٗا فَقَتَلَهُۥ قَالَ أَقَتَلۡتَ نَفۡسٗا زَكِيَّةَۢ بِغَيۡرِ نَفۡسٖ لَّقَدۡ جِئۡتَ شَيۡـٔٗا نُّكۡرٗا

Basi wakatoka wawili hao mpaka wakamkuta kijana, akamuuwa. (Mussa) akasema: Ala! Umemuuwa mtu asiye na kosa, na wala hakuuwa! Ama hakika umefanya jambo baya kabisa!