Surah: ANNAHLI 

Ayah : 82

فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na endapo watakengeuka basi hakika huna jukumu isipokuwa kufikisha (ujumbe) waziwazi tu



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 83

يَعۡرِفُونَ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكۡثَرُهُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ

Wanazijua neema za Allah kisha wanazipinga na wengi wao ni makafiri



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 84

وَيَوۡمَ نَبۡعَثُ مِن كُلِّ أُمَّةٖ شَهِيدٗا ثُمَّ لَا يُؤۡذَنُ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ وَلَا هُمۡ يُسۡتَعۡتَبُونَ

Na (wakumbushe ewe Mtume) siku tutakapofufua shahidi (Mtume wao) kwa kila umma, kisha wale waliyokufuru hawataruhusiwa (kujisahihisha kutokana na waliyoyafanya) na hawata kubaliwa udhuru



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 85

وَإِذَا رَءَا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ ٱلۡعَذَابَ فَلَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمۡ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ

Na wale waliodhulumu watakapoiona adhabu, basi hawata punguziwa (adhabu) na hawatasubiriwa



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 86

وَإِذَا رَءَا ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ شُرَكَآءَهُمۡ قَالُواْ رَبَّنَا هَـٰٓؤُلَآءِ شُرَكَآؤُنَا ٱلَّذِينَ كُنَّا نَدۡعُواْ مِن دُونِكَۖ فَأَلۡقَوۡاْ إِلَيۡهِمُ ٱلۡقَوۡلَ إِنَّكُمۡ لَكَٰذِبُونَ

Na pindi wale washirikina watakapo waona washirika wao (walio washirikisha na Allah), watasema: Mola wetu mlezi, hao ndio washirika wetu ambao tulikuwa tunawaabudu badala yako. Basi watawatupia neno (kwa kusema): hakika ninyi ni waongo kabisa



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 87

وَأَلۡقَوۡاْ إِلَى ٱللَّهِ يَوۡمَئِذٍ ٱلسَّلَمَۖ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Na siku hiyo (washirikishaji) watadhihirisha utii mbele ya Allah, na yatawapotea yote waliyokuwa wakiyatunga



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 88

ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَصَدُّواْ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ زِدۡنَٰهُمۡ عَذَابٗا فَوۡقَ ٱلۡعَذَابِ بِمَا كَانُواْ يُفۡسِدُونَ

(Ama) wale waliokufuru na wakawazuia (watu) njia ya Allah, tutawazidishia adhabu juu ya adhabu kwa yale waliokuwa wakiyaharibu



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 89

وَيَوۡمَ نَبۡعَثُ فِي كُلِّ أُمَّةٖ شَهِيدًا عَلَيۡهِم مِّنۡ أَنفُسِهِمۡۖ وَجِئۡنَا بِكَ شَهِيدًا عَلَىٰ هَـٰٓؤُلَآءِۚ وَنَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ تِبۡيَٰنٗا لِّكُلِّ شَيۡءٖ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٗ وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُسۡلِمِينَ

Na siku tutakayomfufua shahidi (Mtume) katika kila umma kutoka miongoni mwao atakayethibitisha (kuwa aliwafikishia ujumbe wa Allah wakampinga), na tutakuleta wewe kuwa shahidi wa (watu) hawa. Na tumekuteremshia kitabu kikibainisha kila kitu, na rehema na bishara kwa Waislamu



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 90

۞إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُ بِٱلۡعَدۡلِ وَٱلۡإِحۡسَٰنِ وَإِيتَآيِٕ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَيَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِ وَٱلۡبَغۡيِۚ يَعِظُكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ

Kwa hakika Allah anaamuru uadilifu, na ihsani, na kuwapa (sadaka) ndugu wa karibu na anakataza uchafu, na uovu, na uasi. Anawanasihini ili mpate kukumbuka



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 91

وَأَوۡفُواْ بِعَهۡدِ ٱللَّهِ إِذَا عَٰهَدتُّمۡ وَلَا تَنقُضُواْ ٱلۡأَيۡمَٰنَ بَعۡدَ تَوۡكِيدِهَا وَقَدۡ جَعَلۡتُمُ ٱللَّهَ عَلَيۡكُمۡ كَفِيلًاۚ إِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا تَفۡعَلُونَ

Na timizeni ahadi ya Allah mnapoahidi; na msivunje viapo baada ya kuvithibitisha, na hakika mlishamfanya Allah kuwa mdhamini wenu. Hakika Allah anayajua mnayoyafanya



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 92

وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّتِي نَقَضَتۡ غَزۡلَهَا مِنۢ بَعۡدِ قُوَّةٍ أَنكَٰثٗا تَتَّخِذُونَ أَيۡمَٰنَكُمۡ دَخَلَۢا بَيۡنَكُمۡ أَن تَكُونَ أُمَّةٌ هِيَ أَرۡبَىٰ مِنۡ أُمَّةٍۚ إِنَّمَا يَبۡلُوكُمُ ٱللَّهُ بِهِۦۚ وَلَيُبَيِّنَنَّ لَكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ

Na (msirudi katika viapo vyenu ikawa) kama yule mwanamke aliyekata uzi wake vipandevipande baada ya (kuusokota) kuwa mgumu. Mnavifanya viapo vyenu ni njia ya kudanganyana baina yenu ili lisije likawa kundi moja la watu kuwa na nguvu zaidi kuliko kundi lingine. Hakika Allah anawajaribuni kwa njia hiyo, na bila shaka atawabainishieni Siku ya Kiyama mliyokuwa mkikhitilafiana



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 93

وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَعَلَكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَلَٰكِن يُضِلُّ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَلَتُسۡـَٔلُنَّ عَمَّا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na Allah angelitaka, kwa yakini angeliwafanyeni umma moja; lakini anayetaka (upotevu) anampoteza, na anayetaka (mwongozo) anamwongoza; na hakika mtaulizwa yale mliyokuwa mkiyafanya



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 94

وَلَا تَتَّخِذُوٓاْ أَيۡمَٰنَكُمۡ دَخَلَۢا بَيۡنَكُمۡ فَتَزِلَّ قَدَمُۢ بَعۡدَ ثُبُوتِهَا وَتَذُوقُواْ ٱلسُّوٓءَ بِمَا صَدَدتُّمۡ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ وَلَكُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Wala msivifanye viapo vyenu ni njia ya kudanganyana baina yenu, usije mguu ukateleza baada ya kuuimarisha, na mkaonja ubaya kwasababu ya wale mliowazuia katika njia ya Allah, na nyinyi mna adhabu kubwa mno



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 95

وَلَا تَشۡتَرُواْ بِعَهۡدِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ إِنَّمَا عِندَ ٱللَّهِ هُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na msiuze ahadi ya Allah kwa thamani ndogo. Hakika si vingine (kilicho) kwa Allah ni bora kwenu ikiwa mnajua (hayo)



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 96

مَا عِندَكُمۡ يَنفَدُ وَمَا عِندَ ٱللَّهِ بَاقٖۗ وَلَنَجۡزِيَنَّ ٱلَّذِينَ صَبَرُوٓاْ أَجۡرَهُم بِأَحۡسَنِ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Mlivyo navyo vitakwisha na vilivyoko kwa Allah ndivyo vibakiavyo; na kwa yakini sisi tutawapa waliosubiri ujira wao sawa na matendo mazuri waliyokuwa wakiyatenda



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 97

مَنۡ عَمِلَ صَٰلِحٗا مِّن ذَكَرٍ أَوۡ أُنثَىٰ وَهُوَ مُؤۡمِنٞ فَلَنُحۡيِيَنَّهُۥ حَيَوٰةٗ طَيِّبَةٗۖ وَلَنَجۡزِيَنَّهُمۡ أَجۡرَهُم بِأَحۡسَنِ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Atakayefanya mema, mwana-mume au mwanamke, ilhali ni muumini, basi kwa hakika tutampa maisha mema na kwa yakini tutawapa ujira wao kwa uzuri zaidi kuliko yale waliokuwa wakiyatenda



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 98

فَإِذَا قَرَأۡتَ ٱلۡقُرۡءَانَ فَٱسۡتَعِذۡ بِٱللَّهِ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ

Na pindi unapotaka kusoma Qur’ani, basi jikinge kwa Allah (akulinde) na shetani aliyelaaniwa



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 99

إِنَّهُۥ لَيۡسَ لَهُۥ سُلۡطَٰنٌ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَلَىٰ رَبِّهِمۡ يَتَوَكَّلُونَ

Hakika yeye hana nguvu juu ya wale walioamini na kwa Mola wao mlezi tu wanategemea



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 100

إِنَّمَا سُلۡطَٰنُهُۥ عَلَى ٱلَّذِينَ يَتَوَلَّوۡنَهُۥ وَٱلَّذِينَ هُم بِهِۦ مُشۡرِكُونَ

Hakika nguvu yake ni juu ya wale tu wanaomfanya kuwa rafiki na wale wanaomshirikisha (Allah)



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 101

وَإِذَا بَدَّلۡنَآ ءَايَةٗ مَّكَانَ ءَايَةٖ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُنَزِّلُ قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مُفۡتَرِۭۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na pindi tunapobadilisha Aya mahali pa Aya (nyingine), Allah ndiye mjuzi zaidi kwa anachoteremsha (na alichokiondoa), walisema: Hakika wewe ni mzushi tu. Bali wengi wao hawajui



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 102

قُلۡ نَزَّلَهُۥ رُوحُ ٱلۡقُدُسِ مِن رَّبِّكَ بِٱلۡحَقِّ لِيُثَبِّتَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَهُدٗى وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُسۡلِمِينَ

Sema: Ameiteremsha Roho mtakatifu (Jibrili) kutoka kwa Mola wako mlezi kwa haki kabisa, ili kuwaimarisha wale walioamini, na kuwa mwongozo na habari njema kwa Waislamu



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 103

وَلَقَدۡ نَعۡلَمُ أَنَّهُمۡ يَقُولُونَ إِنَّمَا يُعَلِّمُهُۥ بَشَرٞۗ لِّسَانُ ٱلَّذِي يُلۡحِدُونَ إِلَيۡهِ أَعۡجَمِيّٞ وَهَٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيّٞ مُّبِينٌ

Na bila shaka tunajua kwamba (washirikina) wanasema kuwa: Hakika (Muhammad) anafundishwa na mtu hii (Qura’ani. Huo ni uongo kwasababu) mtu wanayedai kumfundisha, lugha yake ni ya kigeni na hii ni lugha ya kiarabu kilicho wazi



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 104

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ لَا يَهۡدِيهِمُ ٱللَّهُ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Hakika wale wasioziamini Aya za Allah, Allah hatawaongoza, na wana adhabu iumizayo



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 105

إِنَّمَا يَفۡتَرِي ٱلۡكَذِبَ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَٰذِبُونَ

Hakika sivingine wanaozua uongo ni wale tu wasioziamini Aya za Allah, na hao ndio waongo (hasa)



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 106

مَن كَفَرَ بِٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ إِيمَٰنِهِۦٓ إِلَّا مَنۡ أُكۡرِهَ وَقَلۡبُهُۥ مُطۡمَئِنُّۢ بِٱلۡإِيمَٰنِ وَلَٰكِن مَّن شَرَحَ بِٱلۡكُفۡرِ صَدۡرٗا فَعَلَيۡهِمۡ غَضَبٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Hakika anayezusha uongo ni Yule aliyetamka neno la ukafiri baada ya imani isipokuwa tu yule aliyeshurutishwa, ilhali moyo wake unabaki imara katika imani. Lakini wale ambao mioyo yao imeridhika na ukafiri, basi ghadhabu za Allah zitawashukia, na watapata adhabu kubwa



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 107

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمُ ٱسۡتَحَبُّواْ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا عَلَى ٱلۡأٓخِرَةِ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Hayo ni kwa sababu wame-yapenda zaidi maisha ya dunia kuliko Akhera, na kwa hakika Allah hawaongozi watu makafiri



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 108

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ طَبَعَ ٱللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ وَسَمۡعِهِمۡ وَأَبۡصَٰرِهِمۡۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡغَٰفِلُونَ

Hao ndio Allah amepiga muhuri juu ya mioyo yao (haizingatii haki na kuifuata) na masikio yao (hawasiki neno la haki) na macho yao (hawaoni haki), na hao ndio walioghafilika



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 109

لَا جَرَمَ أَنَّهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Hakuna shaka kwamba hao ndio wataokhasirika Akhera



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 110

ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا فُتِنُواْ ثُمَّ جَٰهَدُواْ وَصَبَرُوٓاْ إِنَّ رَبَّكَ مِنۢ بَعۡدِهَا لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Kisha hakika Mola wako mlezi, kwa wale waliohama baada ya kuteswa, kisha wakajitahidi na wakasubiri, bila shaka Mola wako mlezi baada ya hayo ni msamehevu sana, mwenye rehema



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 111

۞يَوۡمَ تَأۡتِي كُلُّ نَفۡسٖ تُجَٰدِلُ عَن نَّفۡسِهَا وَتُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا عَمِلَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Siku ambayo kila nafsi itakuja kujitetea yenyewe, na kila nafsi itapewa sawa na iliyoyafanya, nao hawatadhulumiwa