Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 23

وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ

Na hakika yeye alimwona [Jibrili] kwenye upeo wa macho ulio safi



Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 24

وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ

Wala yeye si bakhili kwa [kuelezea mambo ya] ghaibu



Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 25

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ

Na hii (Qurani) si kauli ya shetani aliye fukuzwa kutoka kwenye rehema za Allah



Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 26

فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ

Basi mnakwenda wapi?



Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 27

إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Hii (Qurani) haikuwa isipokuwa ni ukumbusho kwa walimwengu wote



Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 28

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ

Kwa yule anaye taka miongoni mwenu kwenda sawa



Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 29

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Allah Mola wa Walimwengu wote



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 1

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ

Mbingu itakapo chanika,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 2

وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ

Na nyota zitakapo tawanyika,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 3

وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ

Na bahari zitakapo pasuliwa,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 4

وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ

Na makaburi yatakapo fukuliwa,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 5

عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ

Hapo kila nafsi itajua ilichotanguliza, na ilicho bakisha nyuma



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ

Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 7

ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ

Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 8

فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ

Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 9

كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 10

وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 11

كِرَامٗا كَٰتِبِينَ

Waandishi wenye hishima,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 12

يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ

Wanayajua mnayo yatenda



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 13

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema,



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 14

وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 15

يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Wataingia humo Siku ya Malipo



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 16

وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ

Na hawatoacha kuwamo humo



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 17

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 18

ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?



Surah: AL-INFITWAAR 

Ayah : 19

يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ

(Ni) Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 1

وَيۡلٞ لِّلۡمُطَفِّفِينَ

Ole wao hao wapunjao!



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 2

ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكۡتَالُواْ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسۡتَوۡفُونَ

Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 3

وَإِذَا كَالُوهُمۡ أَو وَّزَنُوهُمۡ يُخۡسِرُونَ

Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 4

أَلَا يَظُنُّ أُوْلَـٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبۡعُوثُونَ

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa