Surah: TWAHA 

Ayah : 17

وَمَا تِلۡكَ بِيَمِينِكَ يَٰمُوسَىٰ

Na nini hicho kilichomo katika mkono wako wa kulia, ewe Mussa?



Surah: TWAHA 

Ayah : 18

قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّؤُاْ عَلَيۡهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَـَٔارِبُ أُخۡرَىٰ

Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine



Surah: TWAHA 

Ayah : 19

قَالَ أَلۡقِهَا يَٰمُوسَىٰ

(Allah) Akasema: Basi iangushe ewe Mussa



Surah: TWAHA 

Ayah : 20

فَأَلۡقَىٰهَا فَإِذَا هِيَ حَيَّةٞ تَسۡعَىٰ

Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio



Surah: TWAHA 

Ayah : 21

قَالَ خُذۡهَا وَلَا تَخَفۡۖ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا ٱلۡأُولَىٰ

Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza



Surah: TWAHA 

Ayah : 22

وَٱضۡمُمۡ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٍ ءَايَةً أُخۡرَىٰ

Na ukumbatie mkono wako kwenye ubavu wako. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine



Surah: TWAHA 

Ayah : 23

لِنُرِيَكَ مِنۡ ءَايَٰتِنَا ٱلۡكُبۡرَى

Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa



Surah: TWAHA 

Ayah : 24

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka



Surah: TWAHA 

Ayah : 25

قَالَ رَبِّ ٱشۡرَحۡ لِي صَدۡرِي

(Mussa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,



Surah: TWAHA 

Ayah : 26

وَيَسِّرۡ لِيٓ أَمۡرِي

Na uifanye kazi yangu (kuwa) nyepesi,



Surah: TWAHA 

Ayah : 27

وَٱحۡلُلۡ عُقۡدَةٗ مِّن لِّسَانِي

Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,



Surah: TWAHA 

Ayah : 28

يَفۡقَهُواْ قَوۡلِي

Wapate kufahamu maneno yangu



Surah: TWAHA 

Ayah : 29

وَٱجۡعَل لِّي وَزِيرٗا مِّنۡ أَهۡلِي

Na nipe waziri katika watu wangu,



Surah: TWAHA 

Ayah : 30

هَٰرُونَ أَخِي

Harun, ndugu yangu



Surah: TWAHA 

Ayah : 31

ٱشۡدُدۡ بِهِۦٓ أَزۡرِي

Kwake yeye niongeze nguvu zangu



Surah: TWAHA 

Ayah : 32

وَأَشۡرِكۡهُ فِيٓ أَمۡرِي

Na umshirikishe katika kazi yangu



Surah: TWAHA 

Ayah : 33

كَيۡ نُسَبِّحَكَ كَثِيرٗا

Ili tukutakase sana



Surah: TWAHA 

Ayah : 34

وَنَذۡكُرَكَ كَثِيرًا

Na tukukumbuke sana



Surah: TWAHA 

Ayah : 35

إِنَّكَ كُنتَ بِنَا بَصِيرٗا

Hakika Wewe unatuona



Surah: TWAHA 

Ayah : 36

قَالَ قَدۡ أُوتِيتَ سُؤۡلَكَ يَٰمُوسَىٰ

Akasema: Hakika Umepewa maombi yako, ewe Mussa!



Surah: TWAHA 

Ayah : 37

وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَيۡكَ مَرَّةً أُخۡرَىٰٓ

Na hakika tulikwisha kufanyia hisani mara nyengine



Surah: TWAHA 

Ayah : 38

إِذۡ أَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰٓ أُمِّكَ مَا يُوحَىٰٓ

Pale tulipo mfunulia mama yako yaliyo funuliwa,



Surah: TWAHA 

Ayah : 39

أَنِ ٱقۡذِفِيهِ فِي ٱلتَّابُوتِ فَٱقۡذِفِيهِ فِي ٱلۡيَمِّ فَلۡيُلۡقِهِ ٱلۡيَمُّ بِٱلسَّاحِلِ يَأۡخُذۡهُ عَدُوّٞ لِّي وَعَدُوّٞ لَّهُۥۚ وَأَلۡقَيۡتُ عَلَيۡكَ مَحَبَّةٗ مِّنِّي وَلِتُصۡنَعَ عَلَىٰ عَيۡنِيٓ

Ya kuwa mtie katika kisanduku, na kisha kitie mtoni, na mto utamfikisha ufukweni. Atamchukua adui yangu naye ni adui yake. Na nimekutilia mapenzi yanayotoka kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu



Surah: TWAHA 

Ayah : 40

إِذۡ تَمۡشِيٓ أُخۡتُكَ فَتَقُولُ هَلۡ أَدُلُّكُمۡ عَلَىٰ مَن يَكۡفُلُهُۥۖ فَرَجَعۡنَٰكَ إِلَىٰٓ أُمِّكَ كَيۡ تَقَرَّ عَيۡنُهَا وَلَا تَحۡزَنَۚ وَقَتَلۡتَ نَفۡسٗا فَنَجَّيۡنَٰكَ مِنَ ٱلۡغَمِّ وَفَتَنَّـٰكَ فُتُونٗاۚ فَلَبِثۡتَ سِنِينَ فِيٓ أَهۡلِ مَدۡيَنَ ثُمَّ جِئۡتَ عَلَىٰ قَدَرٖ يَٰمُوسَىٰ

Dada yako alipo kwenda na akasema: Je! Nikujuulisheni mtu wa kuweza kumlea? Basi tukakurejesha kwa mama yako ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ulimuuwa mtu, nasi tukakuokoa katika dhiki, na tukakujaribu kwa majaribio mengi. Ukakaa miaka kwa watu wa Madiyana. Kisha ukaja kama ilivyo kadiriwa, ewe Mussa!



Surah: TWAHA 

Ayah : 41

وَٱصۡطَنَعۡتُكَ لِنَفۡسِي

Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu



Surah: TWAHA 

Ayah : 42

ٱذۡهَبۡ أَنتَ وَأَخُوكَ بِـَٔايَٰتِي وَلَا تَنِيَا فِي ذِكۡرِي

Nenda, wewe na ndugu yako, pamoja na ishara zangu, wala msichoke kunikumbuka



Surah: TWAHA 

Ayah : 43

ٱذۡهَبَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka



Surah: TWAHA 

Ayah : 44

فَقُولَا لَهُۥ قَوۡلٗا لَّيِّنٗا لَّعَلَّهُۥ يَتَذَكَّرُ أَوۡ يَخۡشَىٰ

Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa



Surah: TWAHA 

Ayah : 45

قَالَا رَبَّنَآ إِنَّنَا نَخَافُ أَن يَفۡرُطَ عَلَيۡنَآ أَوۡ أَن يَطۡغَىٰ

Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri



Surah: TWAHA 

Ayah : 46

قَالَ لَا تَخَافَآۖ إِنَّنِي مَعَكُمَآ أَسۡمَعُ وَأَرَىٰ

Akasema: Msiogope! Hakika Mimi nipo pamoja nanyi. Nasikia na ninaona