Surah: ANNISAI 

Ayah : 144

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَتَّخِذُواْ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَجۡعَلُواْ لِلَّهِ عَلَيۡكُمۡ سُلۡطَٰنٗا مُّبِينًا

Enyi mlioamini, msiwafanye makafiri marafiki wa ndani badala ya Waumini (wenzenu). Je, mnataka Allah awe na hoja iliyo wazi kwenu (kwamba nyinyi ni waovu na kustahiki adhabu kwa kuwapenda makafiri badala ya Waislamu wenzenu)?



Surah: ANNISAI 

Ayah : 145

إِنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِي ٱلدَّرۡكِ ٱلۡأَسۡفَلِ مِنَ ٱلنَّارِ وَلَن تَجِدَ لَهُمۡ نَصِيرًا

Hakika, wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa la Moto, na hutampata yeyote wa kuwanusuru



Surah: ANNISAI 

Ayah : 146

إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ وَأَصۡلَحُواْ وَٱعۡتَصَمُواْ بِٱللَّهِ وَأَخۡلَصُواْ دِينَهُمۡ لِلَّهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مَعَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ وَسَوۡفَ يُؤۡتِ ٱللَّهُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ أَجۡرًا عَظِيمٗا

Isipokuwa wale waliotubu (unafiki wao) na wakatengeneza (wakarekebisha na kusahihisha itikadi na misimamo yao mibovu) na wakashikamana na (sheri za) Allah na wakaitakasa dini yao kwa ajili ya Allah. Basi hao watakuwa pamoja na waumini. Na Allah atawapa waumini ujira mkubwa sana



Surah: ANNISAI 

Ayah : 147

مَّا يَفۡعَلُ ٱللَّهُ بِعَذَابِكُمۡ إِن شَكَرۡتُمۡ وَءَامَنتُمۡۚ وَكَانَ ٱللَّهُ شَاكِرًا عَلِيمٗا

Allah hatakuadhibuni iwapo mtashukuru na kuamini, na Allah ndiye Mwenye kupokea shukurani na ndiye Mjuzi sana