Surah: MARYAM 

Ayah : 85

يَوۡمَ نَحۡشُرُ ٱلۡمُتَّقِينَ إِلَى ٱلرَّحۡمَٰنِ وَفۡدٗا

Siku tutakayo wakusanya wacha Mungu kuwapeleka kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni wageni wake



Surah: MARYAM 

Ayah : 86

وَنَسُوقُ ٱلۡمُجۡرِمِينَ إِلَىٰ جَهَنَّمَ وِرۡدٗا

Na tukawachunga waovu kuwapeleka Jahannamu hali ya kuwa wana kiu



Surah: MARYAM 

Ayah : 87

لَّا يَمۡلِكُونَ ٱلشَّفَٰعَةَ إِلَّا مَنِ ٱتَّخَذَ عِندَ ٱلرَّحۡمَٰنِ عَهۡدٗا

Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale walio chukua ahadi kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema



Surah: MARYAM 

Ayah : 88

وَقَالُواْ ٱتَّخَذَ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَلَدٗا

Na wao ati husema kuwa (Allah) Mwingi wa Rehema amejifanyia mtoto!



Surah: MARYAM 

Ayah : 89

لَّقَدۡ جِئۡتُمۡ شَيۡـًٔا إِدّٗا

Hakika mmeleta jambo kubwa mno!



Surah: MARYAM 

Ayah : 90

تَكَادُ ٱلسَّمَٰوَٰتُ يَتَفَطَّرۡنَ مِنۡهُ وَتَنشَقُّ ٱلۡأَرۡضُ وَتَخِرُّ ٱلۡجِبَالُ هَدًّا

Mbingu zinakaribia kupasuka pasuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande



Surah: MARYAM 

Ayah : 91

أَن دَعَوۡاْ لِلرَّحۡمَٰنِ وَلَدٗا

Kwa kudai kwao kuwa (Allah) Mwingi wa Rehema ana mtoto



Surah: MARYAM 

Ayah : 92

وَمَا يَنۢبَغِي لِلرَّحۡمَٰنِ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا

Na haitakiwi kwa (Allah) Mwingi wa Rehema kuwa na mtoto.[1]


1- - Aya hizi tano 88, 89, 90, 91 na 92 zinakataa kwa ukali itikadi kwamba Mungu ana mtoto. Muislamu hatakiwi kabisa kuikumbatia itikadi hii au kuishabikia. Ni itikadi mbaya mno kiasi kwamba mbingu, ardhi na milima haziivumilii kuisikia.


Surah: MARYAM 

Ayah : 93

إِن كُلُّ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ إِلَّآ ءَاتِي ٱلرَّحۡمَٰنِ عَبۡدٗا

Hapana yeyote aliyomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni mtumwa wake



Surah: MARYAM 

Ayah : 94

لَّقَدۡ أَحۡصَىٰهُمۡ وَعَدَّهُمۡ عَدّٗا

Yeye hakika amewadhibiti na amewahesabu sawa sawa



Surah: MARYAM 

Ayah : 95

وَكُلُّهُمۡ ءَاتِيهِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فَرۡدًا

Na kila mmoja katika wao atamfikia Siku ya Kiyama peke yake



Surah: MARYAM 

Ayah : 96

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ سَيَجۡعَلُ لَهُمُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وُدّٗا

Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi



Surah: MARYAM 

Ayah : 97

فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لِتُبَشِّرَ بِهِ ٱلۡمُتَّقِينَ وَتُنذِرَ بِهِۦ قَوۡمٗا لُّدّٗا

Na hakika tumeifanya nyepesi (Qur’ani) kwa ulimi wako, ili uwabashirie kwayo wacha Mungu, na uwaonye kwayo watu wabishi



Surah: MARYAM 

Ayah : 98

وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا قَبۡلَهُم مِّن قَرۡنٍ هَلۡ تُحِسُّ مِنۡهُم مِّنۡ أَحَدٍ أَوۡ تَسۡمَعُ لَهُمۡ رِكۡزَۢا

Na kaumu ngapi tuziangamiza kabla yao. Je! Unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao



Surah: TWAHA 

Ayah : 1

طه

Twaahaa!



Surah: TWAHA 

Ayah : 2

مَآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡقُرۡءَانَ لِتَشۡقَىٰٓ

Hatukukuteremshia Qur’an ili upate mashaka



Surah: TWAHA 

Ayah : 3

إِلَّا تَذۡكِرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰ

Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea



Surah: TWAHA 

Ayah : 4

تَنزِيلٗا مِّمَّنۡ خَلَقَ ٱلۡأَرۡضَ وَٱلسَّمَٰوَٰتِ ٱلۡعُلَى

(Hii Qur’ani ni) uteremsho kutoka kwa Allah Ambaye Ameum-ba ardhi na mbingu zilizo juu



Surah: TWAHA 

Ayah : 5

ٱلرَّحۡمَٰنُ عَلَى ٱلۡعَرۡشِ ٱسۡتَوَىٰ

Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliyestawi juu ya Kiti cha Enzi



Surah: TWAHA 

Ayah : 6

لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَمَا تَحۡتَ ٱلثَّرَىٰ

Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi



Surah: TWAHA 

Ayah : 7

وَإِن تَجۡهَرۡ بِٱلۡقَوۡلِ فَإِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلسِّرَّ وَأَخۡفَى

Na ukinyanyua sauti kwa kusema... basi hakika Yeye anajua siri na kilichofichikana zaidi kuliko siri



Surah: TWAHA 

Ayah : 8

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ لَهُ ٱلۡأَسۡمَآءُ ٱلۡحُسۡنَىٰ

Allah! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa



Surah: TWAHA 

Ayah : 9

وَهَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Na je! Imekufikia habari ya Mussa?



Surah: TWAHA 

Ayah : 10

إِذۡ رَءَا نَارٗا فَقَالَ لِأَهۡلِهِ ٱمۡكُثُوٓاْ إِنِّيٓ ءَانَسۡتُ نَارٗا لَّعَلِّيٓ ءَاتِيكُم مِّنۡهَا بِقَبَسٍ أَوۡ أَجِدُ عَلَى ٱلنَّارِ هُدٗى

Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka (katika) huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto



Surah: TWAHA 

Ayah : 11

فَلَمَّآ أَتَىٰهَا نُودِيَ يَٰمُوسَىٰٓ

Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Mussa!



Surah: TWAHA 

Ayah : 12

إِنِّيٓ أَنَا۠ رَبُّكَ فَٱخۡلَعۡ نَعۡلَيۡكَ إِنَّكَ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوٗى

Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la Tuwa



Surah: TWAHA 

Ayah : 13

وَأَنَا ٱخۡتَرۡتُكَ فَٱسۡتَمِعۡ لِمَا يُوحَىٰٓ

Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa



Surah: TWAHA 

Ayah : 14

إِنَّنِيٓ أَنَا ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱعۡبُدۡنِي وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ لِذِكۡرِيٓ

Hakika Mimi ndiye Allah. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi



Surah: TWAHA 

Ayah : 15

إِنَّ ٱلسَّاعَةَ ءَاتِيَةٌ أَكَادُ أُخۡفِيهَا لِتُجۡزَىٰ كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا تَسۡعَىٰ

Hakika Saa (Kiyama) kitakuja bila ya shaka. Nimekaribia kukificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyo yafanya



Surah: TWAHA 

Ayah : 16

فَلَا يَصُدَّنَّكَ عَنۡهَا مَن لَّا يُؤۡمِنُ بِهَا وَٱتَّبَعَ هَوَىٰهُ فَتَرۡدَىٰ

Kwa hivyo asikukengeushe nacho (Kiyama) yule ambaye hakiamini na akafuata matamanio yake ukaja kuangamia