Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 52

وَلَا تَطۡرُدِ ٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ رَبَّهُم بِٱلۡغَدَوٰةِ وَٱلۡعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجۡهَهُۥۖ مَا عَلَيۡكَ مِنۡ حِسَابِهِم مِّن شَيۡءٖ وَمَا مِنۡ حِسَابِكَ عَلَيۡهِم مِّن شَيۡءٖ فَتَطۡرُدَهُمۡ فَتَكُونَ مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na usiwafukuze wale wanaomuabudu Mola wao asubuhi na jioni, wakitaka radhi za Allah (kwa ibada zao hizo). Si jukumu lako kuwalipa chochote, na wao hawana jukumu la kukulipa chochote hadi iwe sababu ya kuwafukuza. Basi (ukifanya hivyo) utakuwa miongoni mwa madhalimu (wanaodhulumu nafsi zao kwa kufanya yasiyomridhisha Allah)



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 53

وَكَذَٰلِكَ فَتَنَّا بَعۡضَهُم بِبَعۡضٖ لِّيَقُولُوٓاْ أَهَـٰٓؤُلَآءِ مَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنۢ بَيۡنِنَآۗ أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَعۡلَمَ بِٱلشَّـٰكِرِينَ

Na kama hivyo tuliwatia majaribuni baadhi yao kwa wengine ili waseme: Hivi hawa ndio Allah amewaneemesha kati yetu? Hivi Allah hawajui wenye kushukuru?



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 54

وَإِذَا جَآءَكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِنَا فَقُلۡ سَلَٰمٌ عَلَيۡكُمۡۖ كَتَبَ رَبُّكُمۡ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَ أَنَّهُۥ مَنۡ عَمِلَ مِنكُمۡ سُوٓءَۢا بِجَهَٰلَةٖ ثُمَّ تَابَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَصۡلَحَ فَأَنَّهُۥ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na watakapokujia wale wanao-ziamini Aya zetu sema (uwaambie): Amani iwe kwenu. Mola wenu mwenyewe rehema amejithibitishia kwamba, yeyote miongoni mwenu atakayefanya jambo ovu kwa kutojua, kisha baada yake akatubu na kurekebisha (tabia yake) basi hakika yeye (Allah) ni Msamehevu sana, Mwenye kurehemu



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 55

وَكَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ وَلِتَسۡتَبِينَ سَبِيلُ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Na kama hivyo tunazichambua Aya ili ibainike njia ya waovu



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 56

قُلۡ إِنِّي نُهِيتُ أَنۡ أَعۡبُدَ ٱلَّذِينَ تَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِۚ قُل لَّآ أَتَّبِعُ أَهۡوَآءَكُمۡ قَدۡ ضَلَلۡتُ إِذٗا وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُهۡتَدِينَ

Sema: Hakika, mimi nimeka-tazwa kuabudu wale (Miungu) mnaowaomba badala ya Allah. Sema: Hakika, mimi sifuati utashi wa nafsi zenu. (Nikifanya hivyo) Hakika nitakuwa nimepotea, na sitakuwa miongoni mwa watu walio ongoka



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 57

قُلۡ إِنِّي عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَكَذَّبۡتُم بِهِۦۚ مَا عِندِي مَا تَسۡتَعۡجِلُونَ بِهِۦٓۚ إِنِ ٱلۡحُكۡمُ إِلَّا لِلَّهِۖ يَقُصُّ ٱلۡحَقَّۖ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلۡفَٰصِلِينَ

Sema: Hakika, mimi nipo katika hoja ya wazi itokayo kwa Mola wangu Mlezi, na nyinyi mmempinga. Mimi sina kile mnachokiharakisha. Hakuna hukumu isipokuwa ya Allah tu. Yeye anaeleza haki, na yeye ni mbora zaidi ya wakatao shauri



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 58

قُل لَّوۡ أَنَّ عِندِي مَا تَسۡتَعۡجِلُونَ بِهِۦ لَقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۗ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِٱلظَّـٰلِمِينَ

Sema: Lau kama ningekuwa na kile mnachokiharakisha, basi lingekwishahukumiwa jambo kati yangu na kati yenu. Na Allah anawajua zaidi madhalimu



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 59

۞وَعِندَهُۥ مَفَاتِحُ ٱلۡغَيۡبِ لَا يَعۡلَمُهَآ إِلَّا هُوَۚ وَيَعۡلَمُ مَا فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۚ وَمَا تَسۡقُطُ مِن وَرَقَةٍ إِلَّا يَعۡلَمُهَا وَلَا حَبَّةٖ فِي ظُلُمَٰتِ ٱلۡأَرۡضِ وَلَا رَطۡبٖ وَلَا يَابِسٍ إِلَّا فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٖ

Na ziko kwake yeye (Allah) tu funguo (hazina) za Ghaibu; hakuna azijuaye isipokuwa yeye tu. Na anajua kilichopo nchi kavu na baharini. Na halidondoki jani lolote ila analijua. Na (haidondoka) punje yoyote katika giza la ardhini na kibichi na kikavu isipokuwa kipo katika kitabu kinachobainisha (kila kitu)



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 60

وَهُوَ ٱلَّذِي يَتَوَفَّىٰكُم بِٱلَّيۡلِ وَيَعۡلَمُ مَا جَرَحۡتُم بِٱلنَّهَارِ ثُمَّ يَبۡعَثُكُمۡ فِيهِ لِيُقۡضَىٰٓ أَجَلٞ مُّسَمّٗىۖ ثُمَّ إِلَيۡهِ مَرۡجِعُكُمۡ ثُمَّ يُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na yeye (Allah) ndiye ambaye anakufisheni usiku (anakutieni katika usingizi) na anajua mliyoyafanya mchana. Kisha atakufufueni humo (katika mchana) ili utimizwe muda uliowekwa. Kisha kwake tu ndio marejeo yenu, kisha atakupeni habari ya yote mliyokuwa mnayafanya



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 61

وَهُوَ ٱلۡقَاهِرُ فَوۡقَ عِبَادِهِۦۖ وَيُرۡسِلُ عَلَيۡكُمۡ حَفَظَةً حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ تَوَفَّتۡهُ رُسُلُنَا وَهُمۡ لَا يُفَرِّطُونَ

Na yeye tu ndiye Mwenye nguvu kubwa juu ya waja wake, na anatuma kwenu (Malaika) waangalizi (wanaowalinda binadamu na kutunza kumbukumbu za matendo yao)[1], mpaka kinapomfikia mmoja wenu kifo wajumbe wetu wanamfisha, na hawafanyi uzembe


1- - Rejea Aya ya 11, Sura Arraad (13).


Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 62

ثُمَّ رُدُّوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ مَوۡلَىٰهُمُ ٱلۡحَقِّۚ أَلَا لَهُ ٱلۡحُكۡمُ وَهُوَ أَسۡرَعُ ٱلۡحَٰسِبِينَ

Kisha watarudishwa kwa Allah, Mola wao wa haki. Ehee, elewa kwamba, hukumu ni yake yeye (Allah) tu, na yeye ni Mwepesi sana wa wanaohesabu



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 63

قُلۡ مَن يُنَجِّيكُم مِّن ظُلُمَٰتِ ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِ تَدۡعُونَهُۥ تَضَرُّعٗا وَخُفۡيَةٗ لَّئِنۡ أَنجَىٰنَا مِنۡ هَٰذِهِۦ لَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلشَّـٰكِرِينَ

Sema: Ni nani anayekuokoeni katika giza la bara na baharini? Mnamuomba kwa unyenyekevu na kwa siri, (mkisema kwamba:) Endapo (Allah) atatuokoa kwenye haya kwa hakika kabisa tutakuwa miongoni mwa wenye kushukuru



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 64

قُلِ ٱللَّهُ يُنَجِّيكُم مِّنۡهَا وَمِن كُلِّ كَرۡبٖ ثُمَّ أَنتُمۡ تُشۡرِكُونَ

Sema: Allah anakuokoeni kwenye hayo na kwenye kila janga, kisha nyinyi mnafanya ushirikina!



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 65

قُلۡ هُوَ ٱلۡقَادِرُ عَلَىٰٓ أَن يَبۡعَثَ عَلَيۡكُمۡ عَذَابٗا مِّن فَوۡقِكُمۡ أَوۡ مِن تَحۡتِ أَرۡجُلِكُمۡ أَوۡ يَلۡبِسَكُمۡ شِيَعٗا وَيُذِيقَ بَعۡضَكُم بَأۡسَ بَعۡضٍۗ ٱنظُرۡ كَيۡفَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَفۡقَهُونَ

Sema: Yeye tu ndiye Muweza wa kuleta kwenu adhabu itokayo juu yenu au chini ya miguu yenu, au kukuvalisheni nguo ya mfarakano wa makundi na kukuonjesheni mkong’oto wa (nguvu za) wengine. Ona, namna tunavyozifafanua Aya (hoja) ili wapate kufahamu



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 66

وَكَذَّبَ بِهِۦ قَوۡمُكَ وَهُوَ ٱلۡحَقُّۚ قُل لَّسۡتُ عَلَيۡكُم بِوَكِيلٖ

Na watu wako wameikanusha (Qur’ani), na ilhali ndio haki. Sema: Mimi sio mtetezi wenu (lakini mimi ni muonyaji)



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 67

لِّكُلِّ نَبَإٖ مُّسۡتَقَرّٞۚ وَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ

Kila habari ina sehemu yake (maalumu), na punde tu mtajua



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 68

وَإِذَا رَأَيۡتَ ٱلَّذِينَ يَخُوضُونَ فِيٓ ءَايَٰتِنَا فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ يَخُوضُواْ فِي حَدِيثٍ غَيۡرِهِۦۚ وَإِمَّا يُنسِيَنَّكَ ٱلشَّيۡطَٰنُ فَلَا تَقۡعُدۡ بَعۡدَ ٱلذِّكۡرَىٰ مَعَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na utakapowaona wanaozizungumza vibaya Aya zetu, basi wapuuze (na jitenge nao) hadi waingie katika mazungumzo mengine. Na kama shetani atakusahaulisha, basi baada ya kukumbushwa usikae pamoja na watu madhalimu.[1]


1- - Aya hii inawataka Waislamu wahakikishe kuwa maandiko ya dini yao yanaheshimiwa. Pale watakapo ona yanakejiliwa, yanachezewa, yanabezwa au kupotoshwa wasikae kimya bali wakemee na ikibidi waondoke sehemu inapofanyika kejeli hiyo.


Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 69

وَمَا عَلَى ٱلَّذِينَ يَتَّقُونَ مِنۡ حِسَابِهِم مِّن شَيۡءٖ وَلَٰكِن ذِكۡرَىٰ لَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ

Na wale wanaomcha Allah hawana dhambi yoyote katika dhambi zao (watapojitenga nao), lakini (huu) ni ukumbusho tu, ili waogope



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 70

وَذَرِ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ دِينَهُمۡ لَعِبٗا وَلَهۡوٗا وَغَرَّتۡهُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَاۚ وَذَكِّرۡ بِهِۦٓ أَن تُبۡسَلَ نَفۡسُۢ بِمَا كَسَبَتۡ لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلِيّٞ وَلَا شَفِيعٞ وَإِن تَعۡدِلۡ كُلَّ عَدۡلٖ لَّا يُؤۡخَذۡ مِنۡهَآۗ أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أُبۡسِلُواْ بِمَا كَسَبُواْۖ لَهُمۡ شَرَابٞ مِّنۡ حَمِيمٖ وَعَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ

Na waache wale walioifanya dini yao mchezo na pumbao, na yamewahadaa maisha ya dunia. Na kumbusha kwayo (Qur’ani ili), isije nafsi ikaangamizwa kwasababu ya (madhambi) waliyoyachuma, haina mlinzi yeyote wala muombezi yeyote. Na hata kama (nafsi hiyo) itatoa fidia ya aina yoyote (ili isiadhibiwe) haitachukuliwa. Hao ndio wale walioangamizwa kwa (sababu ya madhambi) waliyoyachuma. Watapata kinywaji cha maji ya moto na adhabu iumizayo sana kwa (sababu) ya walivyokuwa wanakufuru



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 71

قُلۡ أَنَدۡعُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَنفَعُنَا وَلَا يَضُرُّنَا وَنُرَدُّ عَلَىٰٓ أَعۡقَابِنَا بَعۡدَ إِذۡ هَدَىٰنَا ٱللَّهُ كَٱلَّذِي ٱسۡتَهۡوَتۡهُ ٱلشَّيَٰطِينُ فِي ٱلۡأَرۡضِ حَيۡرَانَ لَهُۥٓ أَصۡحَٰبٞ يَدۡعُونَهُۥٓ إِلَى ٱلۡهُدَى ٱئۡتِنَاۗ قُلۡ إِنَّ هُدَى ٱللَّهِ هُوَ ٱلۡهُدَىٰۖ وَأُمِرۡنَا لِنُسۡلِمَ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Sema: Hivi tuwaombe (tuwaa-budu) badala ya Allah (Miungu) ambao hawatunufaishi na hawatudhuru na turudishwe nyuma (kwenye itikadi potofu tulizokwisha ziacha) baada ya Allah kutuongoa kama yule ambaye mashetani wamempagawisha katika ardhi, akiduwaa, akiwa na marafiki wanaomuita aende katika uongofu (wakimwambia): Njoo kwetu?[1] Sema: Hakika, muongozo wa Allah ndio uongofu, na tumeamrishwa tujisalimishe kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote


1- - Aya hapa inamtaka Muumini kuwa na msimamo imara na thabiti katika Imani na itikadi yake. Hatakiwi kuyumba au kuyumbishwa. Sio kila analolisikia au kuliona au kushawishiwa alifuate.


Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 72

وَأَنۡ أَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَٱتَّقُوهُۚ وَهُوَ ٱلَّذِيٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ

Na (tumeamrishwa kwamba): Simamisheni Swala, na mumche yeye (Allah), na yeye ndiye ambaye kwake tu ndiko mtakapokusanywa



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 73

وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۖ وَيَوۡمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُۚ قَوۡلُهُ ٱلۡحَقُّۚ وَلَهُ ٱلۡمُلۡكُ يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِۚ عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ

Na yeye ndiye aliyeumba mbingu na ardhi kwa haki. Na (kumbuka) siku (Allah) anaposema (kuliambia jambo): Kuwa, basi linakuwa. Kauli yake ni haki. Ni wake yeye tu ufalme siku litakapopulizwa baragumu. Ni mjuzi wa Ghaibu (yaliyofichika) na yaliyo bayana. Na yeye ni Mwenye hekima, Mjuzi wa habari (zote)



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 74

۞وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِيمُ لِأَبِيهِ ءَازَرَ أَتَتَّخِذُ أَصۡنَامًا ءَالِهَةً إِنِّيٓ أَرَىٰكَ وَقَوۡمَكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ

Na (kumbuka Mtume) Ibrahimu alipomwambia baba yake Azar (kwamba): Hivi unayafanya masanamu Miungu? Hakika, mimi ninakuona wewe na watu wako kwamba mmo katika upotevu ulio wazi



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 75

وَكَذَٰلِكَ نُرِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ مَلَكُوتَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلِيَكُونَ مِنَ ٱلۡمُوقِنِينَ

Na kama hivyo tunamuonyesha Ibrahimu ufalme wa mbinguni na ardhini, na ili awe miongoni mwa wenye yakini



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 76

فَلَمَّا جَنَّ عَلَيۡهِ ٱلَّيۡلُ رَءَا كَوۡكَبٗاۖ قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَآ أُحِبُّ ٱلۡأٓفِلِينَ

Basi (Mtume Ibrahimu) ulipomjia usiku aliona nyota (na) akasema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. (Nyota) Ilipozama alisema: Siwapendi wanaopotea



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 77

فَلَمَّا رَءَا ٱلۡقَمَرَ بَازِغٗا قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَئِن لَّمۡ يَهۡدِنِي رَبِّي لَأَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلضَّآلِّينَ

Na alipoona mwezi umechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. Na (mwezi) ulipozama alisema: Kama Mola wangu hataniongoza, kwa hakika kabisa nitakuwa miongoni mwa watu waliopotea



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 78

فَلَمَّا رَءَا ٱلشَّمۡسَ بَازِغَةٗ قَالَ هَٰذَا رَبِّي هَٰذَآ أَكۡبَرُۖ فَلَمَّآ أَفَلَتۡ قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ

Na alipoliona jua limechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu. Huyu ni mkubwa zaidi (kuliko wote). Basi (jua) lilipozama, alisema: Enyi watu wangu, mimi najitenga mbali na (Miungu yote) mnayoshirikisha (na Allah).[1]


1- - Nabii Ibrahimu katika mdahalo huu aliofanya na watu wake hakumaanisha kwamba na yeye aliamini kuwa nyota, mwezi na jua ni Miungu kama walivyoamini. Alichofanya ni maelekezo aliyopewa na Allah kama ilivyoelezwa katika Aya ya 83 ya Sura hii. Pia hiyo ni aina fulani ya mbinu za ufundishaji ya kujifanya unayemfundisha uko pamoja naye ili ufike naye kwenye ukweli na autambue kwa kutumia hoja, akili na mazingira. Nabii Ibrahimu hakuwa Mshirikishaji bali alikuwa Muumini safi anayemuamini na kumuabudu Allah tu. Rejea Aya 120-123 ya Sura Annahli (16).


Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 79

إِنِّي وَجَّهۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ حَنِيفٗاۖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Hakika, mimi nimeelekeza uso wangu kwa (Allah) aliyeumba mbingu na ardhi, nikiacha itikadi zote potofu, na mimi si miongoni mwa washirikina



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 80

وَحَآجَّهُۥ قَوۡمُهُۥۚ قَالَ أَتُحَـٰٓجُّوٓنِّي فِي ٱللَّهِ وَقَدۡ هَدَىٰنِۚ وَلَآ أَخَافُ مَا تُشۡرِكُونَ بِهِۦٓ إِلَّآ أَن يَشَآءَ رَبِّي شَيۡـٔٗاۚ وَسِعَ رَبِّي كُلَّ شَيۡءٍ عِلۡمًاۚ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ

Na watu wake wakamuwekea mdahalo. Alisema: Hivi, mnanihoji kuhusu Allah, na ilhali ameniongoa? Na siwaogopi hao mnaowashirikisha naye, isipokuwa kama Mola wangu atapenda jambo lolote (linipate). Mola wangu anajua kila kitu kwa mapana na marefu. Hivi hamuonyeki (na haya ninayokuambieni)?



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 81

وَكَيۡفَ أَخَافُ مَآ أَشۡرَكۡتُمۡ وَلَا تَخَافُونَ أَنَّكُمۡ أَشۡرَكۡتُم بِٱللَّهِ مَا لَمۡ يُنَزِّلۡ بِهِۦ عَلَيۡكُمۡ سُلۡطَٰنٗاۚ فَأَيُّ ٱلۡفَرِيقَيۡنِ أَحَقُّ بِٱلۡأَمۡنِۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na vipi niwaogope wale (Miungu bandia) mliowashirikisha (na Allah) na ilhali nyinyi hamuogopi kwamba mmemshirikisha Allah na vitu ambavyo hakukuteremshieni hoja (yoyote)? Basi ni kundi lipi lililo na haki zaidi ya kuwa katika amani kati ya makundi mawili (ya mimi na nyinyi) ikiwa (kweli) mnajua?