Surah: HUUD 

Ayah : 96

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ بِـَٔايَٰتِنَا وَسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ

Na kwa hakika tulimtuma Mussa akiwa na ishara zetu na uthibitisho ulio wazi



Surah: HUUD 

Ayah : 97

إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَٱتَّبَعُوٓاْ أَمۡرَ فِرۡعَوۡنَۖ وَمَآ أَمۡرُ فِرۡعَوۡنَ بِرَشِيدٖ

Kwenda kwa firauni na waheshimiwa wake. Lakini wao walifuata amri ya Firauni, na amri ya Firauni haikuwa na busara



Surah: HUUD 

Ayah : 98

يَقۡدُمُ قَوۡمَهُۥ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فَأَوۡرَدَهُمُ ٱلنَّارَۖ وَبِئۡسَ ٱلۡوِرۡدُ ٱلۡمَوۡرُودُ

Siku ya Kiyama (Firauni) atawatangulia watu wake na atawaingiza Motoni (kama alivyokuwa akiwatangulia duniani). Na ubaya ulioje huo wataoingia!



Surah: HUUD 

Ayah : 99

وَأُتۡبِعُواْ فِي هَٰذِهِۦ لَعۡنَةٗ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ بِئۡسَ ٱلرِّفۡدُ ٱلۡمَرۡفُودُ

Na wamefuatishiwa laana hapa duniani na Siku ya Kiyama. Ni mabaya yalioje watakayo pewa!



Surah: HUUD 

Ayah : 100

ذَٰلِكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡقُرَىٰ نَقُصُّهُۥ عَلَيۡكَۖ مِنۡهَا قَآئِمٞ وَحَصِيدٞ

Hizi ni katika habari za miji, tunakusimulia. Mingine ipo bado na mingine haipo tena



Surah: HUUD 

Ayah : 101

وَمَا ظَلَمۡنَٰهُمۡ وَلَٰكِن ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡۖ فَمَآ أَغۡنَتۡ عَنۡهُمۡ ءَالِهَتُهُمُ ٱلَّتِي يَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مِن شَيۡءٖ لَّمَّا جَآءَ أَمۡرُ رَبِّكَۖ وَمَا زَادُوهُمۡ غَيۡرَ تَتۡبِيبٖ

Na sisi hatukuwadhulumu, lakini wao wenyewe wamezidhulumu nafsi zao. Na haikuwafaa chochote Miungu yao waliyokuwa wakiiomba badala ya Allah ilipokuja amri ya Mola wako mlezi. Na hiyo Miungu haikuwazidishia kitu isipokuwa maangamizi tu



Surah: HUUD 

Ayah : 102

وَكَذَٰلِكَ أَخۡذُ رَبِّكَ إِذَآ أَخَذَ ٱلۡقُرَىٰ وَهِيَ ظَٰلِمَةٌۚ إِنَّ أَخۡذَهُۥٓ أَلِيمٞ شَدِيدٌ

Na hivyo ndivyo Mola wako mlezi anawachukulia hatua anapowachukulia hatua watu wa miji wanapodhulumu. Hakika (akikamata) mkamato wake ni mchungu na mkali mno



Surah: HUUD 

Ayah : 103

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّمَنۡ خَافَ عَذَابَ ٱلۡأٓخِرَةِۚ ذَٰلِكَ يَوۡمٞ مَّجۡمُوعٞ لَّهُ ٱلنَّاسُ وَذَٰلِكَ يَوۡمٞ مَّشۡهُودٞ

Hakika katika hilo kuna ishara kwa kila anayeogopa adhabu ya Akhera. Hiyo ni Siku itakayokusanyiwa watukwake, na hiyo ni Siku itakayoshuhudiwa



Surah: HUUD 

Ayah : 104

وَمَا نُؤَخِّرُهُۥٓ إِلَّا لِأَجَلٖ مَّعۡدُودٖ

Na sisi hatuicheleweshi ispokuwa kwa muda tu unao hesabiwa



Surah: HUUD 

Ayah : 105

يَوۡمَ يَأۡتِ لَا تَكَلَّمُ نَفۡسٌ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦۚ فَمِنۡهُمۡ شَقِيّٞ وَسَعِيدٞ

Siku hiyo itakapo fika, hatosema hata mtu mmoja (chochote) isipokuwa kwa idhini yake (Allah). Basi kati yao wapo waovu na walio wema



Surah: HUUD 

Ayah : 106

فَأَمَّا ٱلَّذِينَ شَقُواْ فَفِي ٱلنَّارِ لَهُمۡ فِيهَا زَفِيرٞ وَشَهِيقٌ

Ama wale waovu basi hao Motoni ndio makazi yao humo watasikia sauti za Moto ukivuta pumzi ndani na kutoa nje



Surah: HUUD 

Ayah : 107

خَٰلِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ إِلَّا مَا شَآءَ رَبُّكَۚ إِنَّ رَبَّكَ فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ

Watadumu humo muda wa kuwepo mbingu na ardhi, isipokuwa vile apendavyo Mola wako mlezi. Hakika Mola wako mlezi anatenda apendavyo



Surah: HUUD 

Ayah : 108

۞وَأَمَّا ٱلَّذِينَ سُعِدُواْ فَفِي ٱلۡجَنَّةِ خَٰلِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ إِلَّا مَا شَآءَ رَبُّكَۖ عَطَآءً غَيۡرَ مَجۡذُوذٖ

Na ama wale walio bahatika (kupata maisha mazuri), wao watakuwa Peponi watadumu humo muda wa kuwepo mbingu na ardhi, isipokuwa apendavyo Mola wako mlezi. Hicho ni zawadi (kipawa) kisio na ukomo



Surah: HUUD 

Ayah : 109

فَلَا تَكُ فِي مِرۡيَةٖ مِّمَّا يَعۡبُدُ هَـٰٓؤُلَآءِۚ مَا يَعۡبُدُونَ إِلَّا كَمَا يَعۡبُدُ ءَابَآؤُهُم مِّن قَبۡلُۚ وَإِنَّا لَمُوَفُّوهُمۡ نَصِيبَهُمۡ غَيۡرَ مَنقُوصٖ

Basi usiwe na shaka juu ya wanayo yaabudu hawa. Hawaabudu isipokuwa kama walivyo abudu baba zao zamani. Na hakika sisi tutawatimilizia fungu lao bila ya kupunguzwa



Surah: HUUD 

Ayah : 110

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ فَٱخۡتُلِفَ فِيهِۚ وَلَوۡلَا كَلِمَةٞ سَبَقَتۡ مِن رَّبِّكَ لَقُضِيَ بَيۡنَهُمۡۚ وَإِنَّهُمۡ لَفِي شَكّٖ مِّنۡهُ مُرِيبٖ

Na kwa yakini tulimpa Mussa kitabu (Taurati) wakatofautiana kuna walioiamini na wapo waliyoikataa). Na lau kama si kutangulia neno kutoka kwa Mola wako mlezi, (kwamba hatawaharakishia adhabu) bila ya shaka ingehukumiwa baina yao kwakuwaangamiza. Na hakika wao wamo katika shaka juu yake inayo wahangaisha



Surah: HUUD 

Ayah : 111

وَإِنَّ كُلّٗا لَّمَّا لَيُوَفِّيَنَّهُمۡ رَبُّكَ أَعۡمَٰلَهُمۡۚ إِنَّهُۥ بِمَا يَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Na hakika kila kaumu (zilizotajwa) watalipwa malipo yao kamili. Hakika Yeye kwa yote myatendayo anayo habari



Surah: HUUD 

Ayah : 112

فَٱسۡتَقِمۡ كَمَآ أُمِرۡتَ وَمَن تَابَ مَعَكَ وَلَا تَطۡغَوۡاْۚ إِنَّهُۥ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Basi, simama imara kama ulivyo amrishwa, na wale waliotubu pamoja na wewe, na msichupe mipaka. Hakika Yeye anayaona yote myatendayo



Surah: HUUD 

Ayah : 113

وَلَا تَرۡكَنُوٓاْ إِلَى ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ فَتَمَسَّكُمُ ٱلنَّارُ وَمَا لَكُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ مِنۡ أَوۡلِيَآءَ ثُمَّ لَا تُنصَرُونَ

Wala msiwategemee wale walio dhulumu, na ikasababisha ukakuguseni Moto. na nyinyi hamna walinzi (wengine) badala ya Allah, kisha hamtanusuriwa



Surah: HUUD 

Ayah : 114

وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ طَرَفَيِ ٱلنَّهَارِ وَزُلَفٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِۚ إِنَّ ٱلۡحَسَنَٰتِ يُذۡهِبۡنَ ٱلسَّيِّـَٔاتِۚ ذَٰلِكَ ذِكۡرَىٰ لِلذَّـٰكِرِينَ

Na simamisha swala katika ncha mbili za mchana na nyakati za usiku. Hakika mema huondoa maovu. Huo ni ukumbusho kwa wale wanaokumbuka



Surah: HUUD 

Ayah : 115

وَٱصۡبِرۡ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na subiri (kuwa mvumilivu), kwani Allah hapotezi ujira wa wafanyao wema



Surah: HUUD 

Ayah : 116

فَلَوۡلَا كَانَ مِنَ ٱلۡقُرُونِ مِن قَبۡلِكُمۡ أُوْلُواْ بَقِيَّةٖ يَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡفَسَادِ فِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا قَلِيلٗا مِّمَّنۡ أَنجَيۡنَا مِنۡهُمۡۗ وَٱتَّبَعَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مَآ أُتۡرِفُواْ فِيهِ وَكَانُواْ مُجۡرِمِينَ

Na lau ingekuwepo katika karine za kabla yenu masalia ya watu wa kheri wanakataza maovu ardhini, (lakini hawakuwepo miongoni mwa watu wa kheri) isipokuwa wachache tu. Miongoni mwa (walioamini) tuliowaokoa kutoka kwenye adhabu. Na wale waliodhulumu wakafuata starehe zao walizoneemeshwa, na wakawa waovu



Surah: HUUD 

Ayah : 117

وَمَا كَانَ رَبُّكَ لِيُهۡلِكَ ٱلۡقُرَىٰ بِظُلۡمٖ وَأَهۡلُهَا مُصۡلِحُونَ

Na hakuwa Mola wako mlezi ni mwenye kuangamiza watu wa miji kwa dhulma tu na hali watu wake ni watenda mema



Surah: HUUD 

Ayah : 118

وَلَوۡ شَآءَ رَبُّكَ لَجَعَلَ ٱلنَّاسَ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗۖ وَلَا يَزَالُونَ مُخۡتَلِفِينَ

Na lau angetaka Mola wako mlezi ange wafanya watu wote kuwa umma mmoja. Na hawaachi kukhitalifiana,



Surah: HUUD 

Ayah : 119

إِلَّا مَن رَّحِمَ رَبُّكَۚ وَلِذَٰلِكَ خَلَقَهُمۡۗ وَتَمَّتۡ كَلِمَةُ رَبِّكَ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ

Isipokuwa tu wale Mola wako mlezi amewarehemu (wakaamini); na Allah amewaumba hivyo. Na neno la Mola wako mlezi litatimia: Kwe hakika nitaijaza Jahannam miongoni mwa majini na watu wote kwa pamoja



Surah: HUUD 

Ayah : 120

وَكُلّٗا نَّقُصُّ عَلَيۡكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلرُّسُلِ مَا نُثَبِّتُ بِهِۦ فُؤَادَكَۚ وَجَآءَكَ فِي هَٰذِهِ ٱلۡحَقُّ وَمَوۡعِظَةٞ وَذِكۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Na yote haya tunakusimulia miongoni mwa habari za Mitume yale yanayoupa nguvu moyo wako. Na katika haya imekujia haki na mawaidha na ukumbusho kwa waumini



Surah: HUUD 

Ayah : 121

وَقُل لِّلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ ٱعۡمَلُواْ عَلَىٰ مَكَانَتِكُمۡ إِنَّا عَٰمِلُونَ

Na waambie wale wasio amini: Fanyeni muwezavyo, nasi pia tunafanya (tuwezavyo)



Surah: HUUD 

Ayah : 122

وَٱنتَظِرُوٓاْ إِنَّا مُنتَظِرُونَ

Na ngojeni, na sisi tunangoja



Surah: HUUD 

Ayah : 123

وَلِلَّهِ غَيۡبُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَإِلَيۡهِ يُرۡجَعُ ٱلۡأَمۡرُ كُلُّهُۥ فَٱعۡبُدۡهُ وَتَوَكَّلۡ عَلَيۡهِۚ وَمَا رَبُّكَ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Na ni vya Allah tu vyote vilivyo fichikana mbinguni na ardhini, na mambo yote yatarudishwa kwake tu. Basi muabudu yeye na umtegemee yeye. Na Mola wako mlezi haghafiliki na yale mnayo yatenda



Surah: YUSUF 

Ayah : 1

الٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Alif Laam Raa[1]. Hizo ni Aya za Kitabu kinachobainisha


1- - Allah ndiye ajuaye zaidi maana ya herufi mkato hizi.


Surah: YUSUF 

Ayah : 2

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ قُرۡءَٰنًا عَرَبِيّٗا لَّعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ

Hakika, sisi tumeiteremsha Qur’ani kwa Kiarabu ili mpate kuelewa